Idhaa ya Redio ya UM


Ofisa Mkuu Mtendaji wa Taasisi ya NEPAD azungumzia mwelekeo unaohitajika kusukuma mbele maendeleo Afrika

23/10/2009
Mapema wiki hii, kabla ya kuzungumzia kikao cha Baraza Kuu la UM, kusailia ripoti kadha za KM, na kutoka wajumbe wa kimataifa na mashirika ya UM zilizozingatia huduma za kukuza maendeleo katika Afrika, Dktr Ibrahim Assane Mayaki, Ofisa Mkuu Mtendaji wa Taasisi ya Ushirikiano Mpya wa Maendeleo kwa Afrika (NEPAD), alifanya mahojiano maalumu na waandishi habari waliopo Makao Makuu.

Kadhalika, mtayraishaji vipindi wa Idhaa ya Kiingereza ya Redio ya UM, Derrick Mbatha, naye pia alipata fursa ya kumhoji Dktr Mayaki kuhusu masuala yanayoambatana na miradi ya kukuza maendeleo ya kiuchumi na jamii katika Afrika, kwa ushirikiano na wadau wa kimataifa, ikijumlisha mashirika ya UM.  Tulitaka kujua kama  nchi za KiAfrika zinaelekea mkondo unaoridhisha katika kutekeleza miradi ya maendeleo, kwa hivi sasa, hasa katika kipindi ambacho uchumi wa dunia umezongwa na matatizo aina kwa aina, ikijumlisha mizozo ya kifedha, chakula na athari haribifu zamabadiliko ya hali ya hewa. Kwenye mahojiano na Mbatha, miongoni mwa mada alizogusia  ilijumlisha namna mataifa ya Afrika yanavyotekeleza miradi ya maendeleo; matatizo ya uhamaji wa kutoka mashamba kwenda mijini na umuhimu wa kuimarisha miundombinu, kwa minajili ya kukuza maendeleo ya vijijini.

Sikiliza taarifa kamili kwenye idhaaya mtandao. 


http://www.unmultimedia.org/radio/kiswahili/print/98032.html