26 Juni 2009
TBD
Siku ya Ushikamano wa Kimataifa na Walioathirika Mateso
26/06/2009
Tarehe ya leo, 26 Julai, inaadhimishwa na UM kuwa ni Siku ya Ushikamano Kimataifa na Wathirika wa Mateso.
Kwenye risala ya KM kuihishimu siku hii ametilia mkazo kauli inayosisitiza kwamba hakuna kanuni inayokubalika inayoweza kuhalalisha au kutetea vitendo vya mateso au ule mfumo wa kikatili, usio wa kiutu, wenye kudhalilisha wanadamu, hali ambayo alisisitiza haina msingi wa kimaadili ya kiutu, wala haikubaliki katika mazingira ya aina yoyote, wakati wowote, kote ulimwenguni.

