Nepal isisamehe makosa makubwa ya ukiukwaji wa haki: Pillay

Kusikiliza /

Navi Pillay

Kamishna Mkuu wa Umoja wa Mataifa juu ya haki za binadamu Navi Pillay amelaani na kupinga hatua ya Nepal ambayo imepitisha sheria ya uanzishwaji wa Tume ya ukweli na maridhiano itakayokuwa na uwezo wa kutoa msamaha kwa watu wanaotuhumiwa kwenda kinyume na misingi ya haki za binadamu nchini humo.  Pamoja na kupinga hatua hiyo, Pillay pia ameitolea wito serikali ya Nepal kuifanyia marekebisho sheria hiyo na vifungo vingine ambavyo utekelezaji wake unakiuka misingi ya kimataifa. George Njogopa na maelezo zaidi

(SAUTI YA GEORGE)

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031