IOM yajiandaa kutoa misaada ya kibinadamu kabla ya uchaguzi wa Kenya

Kusikiliza /

 Shirika la Kimataifa la Uhamiaji, IOM, limesema linaweka mikakati ya kujiandaa kutoa misaada ya kibinadamu nchini Kenya, siku chache kabla ya uchaguzi nchini humo hapo Jumatatu.

Shirika hilo limesema linashirikiana na serikali kuweka mipango ya dharura ambayo itajumuisha sekta mbali mbali, ili kuwa tayari kwa uchaguzi huo, kwa kuandaa bidhaa zisizo chakula.

IOM pia imetambua mashirika ambayo yana uwezo wa kushirikiana nayo, pamoja na kufanya warsha za mafunzo katika utoaji wa miaada ya dharura kwa wafanyakazi wa Shirika la Msalaba Mwekundu la Kenya. Jumbe Omari Jumbe ni msemaji wa IOM

SAUTI YA JUMBE

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031