Quinoa zao la kumkomboa mkulima, lastahimili ardhi kame!

Kusikiliza /

Quinoa

Hatimaye mwaka wa kimataifa wa zao la Quinoa umezinduliwa rasmi kwenye kikao maalum cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani. Shughuli hiyo imeshudiwa na viongozi na wawakilishi wa mataifa na mashirika mbali mbali akiwemo Rais wa Bolivia, Evo Morales ambaye nchi yake ndiyo inaongoza duniani kwa kuuza zao hilo nje ya nchi. Tayari tumeelezwa kuwa zao la Quinoa, ambayo ni nafaka itokanayo na mbegu za mmea huo jamii ya spinachi, limeenea nchi mbali mbali duniani ikiwemo Kenya na kutoa matumaini ya kutokomeza njaa na umaskini miongoni mwa wakulima. Basi kwa taarifa zaidi kuhusiana na zao hilo na manufaa yake fuatana na Assumpta Massoi katika ripoti hii maalum.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031