Ban akaribisha mazungumzo ya Kachin

Kusikiliza /

KM Ban Ki-moon

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amekaribisha na kupongeza hatua ya kuwepo kwa mazungumzo yenye shabaha ya kutanzua mkwamo wa eneo la Kachin la China na Mynmar.

Pande zote mbili zimetoa taarifa ya pamoja iliyoelezea namna zilivyodhamiria kuanzisha majadiliano ili kuepusha uwekekano wa kuzidisha machafuko katika jimbo la Kachin linalowaniwa na pande zote mbili.

Akizungumzia hiyo ya pamoja iliyotolewa na pande zote mbili, Ban pamoja na kuzipongeza lakini amezihimiza kuendelea kukaribisha majadiliano ili kupatikana kwa suluhu ya kudumu.

Katika taarifa yake Ban amesema kuwa ni matumaini yake kuona kwamba yale yaliyofikiwa wakati huu yataendelea kulindwa na hatimaye kufikia shabaha ya kutanzua jumla mzozo huo.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031