Kusikiliza /

Msimamizi Mkuu wa masuala ya kisiasa ndani ya Umoja wa Mataifa Jeffrey Feltman amehitimisha ziara yake nchini Burundi na kupongeza mchango wa nchi hiyo katika ujenzi wa amani na utulivu nchini Somalia. Feltman amesema hayo alipozungumza na waandishi wa habari mjini Gitega nchini Burundi baada ya mazungumzo yake na Rais wa nchi hiyo Pierre Nkurunziza. [...]
02/02/2013 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kufuatia shambulio dhidi ya Ubalozi wa Marekani nchini Uturuki siku ya Ijumaa, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelaani kitendo hicho na kusema kuwa ni cha kinyama huku wajumbe wake wakituma rambirambi kwa wafiwa. Taarifa iliyotolewa na baraza hilo imesema linasikitishwa na shambulio hilo mjini Ankara ambalo limesababisha kifo cha mtu mmoja na majeruhi.. [...]
02/02/2013 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

"Tunataka hatua za haraka za kulinda na kujenga upya maeneo ya kipekee ya urithi wa kiutamaduni nchini Mali". Hiyo ni kauli ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Matiaifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, Irina Bokova, aliyoitoa Jumamosi baada ya kuwasili nchini Mali, ikiwa ni sehemu ya harakati za shirika hilo za kusaidia [...]
02/02/2013 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »