Wahamiaji wa Ethiopia waliokuwa wamekwama Yemen warejeshwa makwao: IOM
Kusikiliza /Shirika la kimataifa la uhamiaji, IOM limewarejesha makwao kwa ndege raia 210 wa Ethiopia waliokuwa wamekwama huko Yemen baada ya kushindwa kuingia Saudi Arabia kutafuta ajira.
IOM inasema imegharimu dola Milioni Mbili nukta Moja ambazo ni msaada kutoka Uholanzi kusafirisha raia hao ambao wanafikisha idadi ya raia 9,500 wa Ethiopia waliorejeshwa nyumbani kutoka Yemen kwa msaada wa IOM tangu mwaka 2010.
Waethiopia hao wanajumuisha wanawake, watoto, wazee ambapo baadhi yao ni wagonjwa. Jumbe Omari Jumbe ni msemaji wa IOM.
(SAUTI YA JUMBE OMAR JUMBE)
