Ushirikiano njia pekee ya kulinda raia: UNAMID

Kusikiliza /

Aïchatou Mindaoudou

Kaimu Mkuu wa kikundi cha pamoja cha Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika kinacholinda amani huko Darfur, UNAMID, Aïchatou Mindaoudou amesema ushirikiano miongoni mwa pande zote husika kwenye eneo hilo ndio njia pekee ya kuwezesha ulinzi wa raia.

Bi. Mindaoudou amesema hayo baada ya ziara yake ya siku mbili katika maeneo ya Kusini na Mashariki mwa Darfur ambapo alipata fursa ya kuzungumza na viongozi wa kijamii, serikali na kuchunguza njia mpya za kuendeleza amani na kuimarisha ushirikiano kati ya UNAMID na washika dau uwote.

Amesema ushirikiano mathalani kati ya mamlaka za serikali na viongozi wa kijamii ni muhimu katika kufanikisha mkakati wa UNAMID wa kulinda raia hususan kwa kuepusha matatizo na kuchukua hatua haraka pindi mgogoro unapojitokeza.

Ziara kama hiyo aliifanya mwezi uliopita huko Darfur ya Kati, Magharibi na Kaskazini.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031