Unyanyasaji wa kijinsia bado ni tatizo kubwa Jamhuri ya Afrika ya Kati: Bangura
Kusikiliza /Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu unyanyasaji wa kingono kwenye migogoro, Hawa Bangura amehitimisha wiki moja ya ziara yake huko Jamhuri ya Afrika ya Kati na kueleza kuwa unyanyasaji wa kingono bado ni tatizo dhahiri nchini humo hasa maeneo yanayodhibitiwa na vikundi vya kisiasa au kijeshi.
Amesema kwa muda wote aliokuwepo nchini humo pamoja na fursa ya kutembelea maeneo mbali mbali amebaini kuwa matukio ya unyanyasaji wa kingono uko bayana ambapo wanawake na watoto wanakamatwa na kunyanyaswa kijinsia na vikundi hivyo.
(SAUTI YA HAWA BANGURA)
