Mtuhumiwa wa makosa ya uhalifu wa kivita DRC Mathiew Ngudjolo Chui hana hatia: ICC

Kusikiliza /

Mathieu Ngodjolo Chui, ICC

Mahakama ya kimataifa ya makosa ya jinai, ICC imeamuru kuachiwa huru kwa mtuhumiwa wa makosa ya uhalifu wa kivita dhidi ya binadamu, Mathieu Ngudjolo Chui baada ya kumuona kuwa hana hatia.

Uamuzi huo umepitishwa kwa kauli moja na jopo la majaji watatu wakiongozwa na Jaji Bruno Cotte kutoka Ufaransa ambapo wamesema upande wa mashtaka umeshindwa kuthibitisha madai dhidi ya mtuhumiwa na hivyo kuamuru msajili wa mahakama kuchukua hatua muafaka kumuachia huru Ngudjolo.

(SAUTI YA JAJI BRUNO COTTE)

Hata hivyo upande wa mashtaka unataka kukata rufaa na uamuzi utatolewa baadaye leo. Mathieu Ngudjolo Chui, raia wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo alishtakiwa kwa makosa matatu ya uhalifu dhidi ya binadamu, na makosa saba ya uhalifu wa kivita ambayo anadaiwa kutenda wakati wa mgogoro huko Ituri mwezi Februari mwaka 2003.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031