Mkutano kuhusu chanjo ya watoto wafanyika Tanzania
Kusikiliza /Wataalamun wa afya pamoja na watunga sera kutoka mataifa mbalimbali duniani pamoja na wawakilishi wa Umoja wa Mataifa wameanzisha mkutano wa siku tatu nchini Tanzania kujadilia hali ya utoaji chanjo na namna ya kukabiliana na magonjwa yanayoweza kutibika kwa watoto.
Mkutano huo ambao umewajumuisha wajumbe zaidi ya 600, umehusisha Shirika la idadi ya watu UNFPA , na unafanyika chini ya kivuli cha fuko la kimataifa la chanjo na kinga yaani "Global Alliance for Vaccine and Immunisation (GAVI).
Mkataba wa hivi karibuni wa Umoja wa Mataifa unaotaka haki na usawa kwa maiasha ya watoto ni miongoni mwa maeneo yanayoangaziwa na wajumbe na shabaha iliyoko ni kuona kwamba yale yaliyofafanuliwa kwenye mkataba huo wa kimataifa yanatekelezwa kivitendo.
(SAUTI YA GEORGE NJOGOPA)
