Hali ya kibinadamu nchini Syria yazidi kuzorota

Kusikiliza /

mama na mtoto nchini, Syria

Shirika la mpango wa chakula duniani, WFP limesema hali ya kibinadamu nchini Syria inazidi kuzorota ambapo mahitaji ya chakula yanazidi kuongezeka, halikadhalika idadi ya watu wanaopoteza makazi yao.

Msemaji wa WFP Elizabeth Byrs amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi kuwa hivi sasa wanahudumia watu Milioni Moja na Nusu kwa mwezi nchini Syria. Hata hivyo kuendelea kusambaa kwa mapigano kunasababisha washindwe kufikia maeneo kama vile yale ya kaskazini. Amesema katika maeneo ya mapigano, bei za vyakula zimeongezeka maradufu.

Wakati huo huo shirika la afya duniani WHO limesema hali ya utoaji wa huduma ya afya inazidi kudorora kwa kuwa wagonjwa na watoa huduma wanashinda kufika vituo vya afya kwa sababu ya hofu ya usalama.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Juni 2013
T N T K J M P
« mei    
 12
3456789
10111213141516
17181920212223
24252627282930