Kusikiliza /

Harakati za viwanda kujaribu kuhifadhi mazingira kwa kutumia mabaki ya malighafi za bidhaa zake kuzalisha bidhaa nyingine zinazidi kushika kasi, na viwanda kuwa mifano kwa viwanda vingine kama njia mojawapo ya kuhifadhi mazingira huku zikijiibulia huduma zingine. Miongoni mwa viwanda hivyo ni kile cha sukari cha Mumias nchini Kenya ambacho sasa kinazalisha umeme kwa kutumia [...]
26/12/2012 | Jamii: Mahojiano | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kundi la watu mashuhuri, wakiwemo Rais wa zamani wa Ufaransa Jacques Chirac na Balozi wa mfuko wa Danielle Mitterrand, Valérie Trierweiler ambaye pia ni rafiki wa rais wa sasa wa Ufaransa, wametoa wito kwa Umoja wa Mataifa kupitisha azimio litakaloruhusu askari wa kulinda amani wa Umoja huo huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, MONUSCO kuongezewa [...]
26/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamadunia, UNESCO, Irina Bokova amelaani mauaji ya mwandishi wa habari wa televisheni nchini Syria, Haidar al-Sumudi . Bi. Bokova amesema amesikitishwa na mauaji ya mwandishi huyo pamoja na mashambulizi yanayoendelea dhidi ya waandishi wa habari nchini Syria na kusema uhuru wa kujieleza ni [...]
26/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mpango wa mfuko wa Umoja wa Mataifa wa maendeleo ya Kilimo, IFAD wa kufadhili miradi ya upandaji miti nchini Kenya umeanza kuzaa matunda ambapo tangu mwaka 2005 hadi sasa zaidi ya miche Milioni Moja imepandwa katika maeneo ya vyanzo vya maji kwenye miteremko ya mlima Kenya. Miche hiyo inajumuisha miche Elfu Nne iliyopandwa na shule [...]
26/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kufuatia mazungumzo ya siku kadhaa, Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa limekalimisha sehemu kubwa ya kikao chake cha 67 kwa kupitishwa kwa azimio mbili kutoka kwa kamati za usimamizi na bajeti. Baraza hilo lenye wanachama 193 limechukua maamuzi kutokana na jinsi vile wanachama watakavyoweza kuchangia bajeti za shughuli za kulinda amani kwa muda wa miaka [...]
26/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ikiwa imepita kiasi cha siku 650 tangu kuanza kwa machafuko nchini Syria, idadi kubwa ya watu sasa wameingia kwenye wakati mgumu wa kusaka hali ya joto katika wakati ambapo kiwango cha nyuzi joto kikishuhudiwa kupungua. Kiwango hicho cha nyuzi joto kinatazamiwa kushuka zaidi kuanzia mwezi ujao ambao taifa hilo linakumbwa na hali mbaya zaidi ya [...]
26/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakimbizi wa Burundi waliokuwa wakiishi Tanzania kwa miongo kadhaa pamoja na familia zao na ambao wamerejea nyumbani baada ya amani kupatikana nchini mwao, wamekiri kushuhudia hali ya amani nchini mwao tofauti na taarifa waliozokuwa wakipata wakiwa kwenye kambi.Taarifa zaidi na Alice Kariuki. (SAUTI YA ALICE KARIUKI)
26/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »