Nyumbani » 07/12/2012
Entries posted on “Disemba 7th, 2012”
Kusikiliza /

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo limepatiwa mapendekezo ya awali ya kile ambacho kinapaswa kufanywa ili kuimarisha uwezo wa kikosi cha umoja huo kinacholinda amani huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC, MONUSCO, suala ambalo linatokana na azimio 2076 lililopitishwa mwezi uliopita na baraza hilo. Azimio hilo lilipitishwa baada ya waasi wa [...]
07/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa ambaye yuko ziarani nchini Uturuki, hii leo ametembelea kambi ya Islahiye nchini humo inayohifadhi wakimbizi wa Syria na kuelezea kushtushwa na kuguswa na kwake na simulizi kutoka kwa wakimbizi hao wakiwemo watoto. Akizungumza na waandishi wa habari baada ya ziara kwenye kambi hiyo iliyoko jimbo la Gaziantep, nchini humo, [...]
07/12/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Siko seli au seli mundu ni miongoni mwa magonjwa yanayoendelea kutikisa nchi mbali mbali duniani ambapo kila mwaka watoto Laki Tatu huzaliwa na ugonjwa huo wa kurithi, na hizo ni takwimu za Shirika la afya duniani, WHO. Kati ya hao, asilimia 80 wanatoka barani Afrika, ambako Tanzania inashika nafasi ya nne kwa kuwa na idadi [...]
07/12/2012 | Jamii: Makala za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ripoti ya shirika la kazi Ulimwenguni ILO imeonyesha kuwepo kwa ongezeko ndogo la ukuaji wa ujira na wakati huo hali katika nchi zilizoendelea siyo ya kuridhisha licha maeneo hayo kushuhudia kuanza kuimarika kwa hali ya uchumi baada ya kukubwa na misuko suko ya kuanguka kwa uchumi. Ripoti hiyo ya mwaka 2012-2013 iliyotolewa leo inaonyesha kuwa [...]
07/12/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Takribani watu Laki Tatu na Nusu wanaishi katika vituo vya hifadhi huko Mashariki mwa kisiwa cha Mindanao nchini Ufilipino baada ya kimbunga Bopha kuharibu makazi, mali na miundombinu pamoja na kusababisha majeruhi na vifo vya watu takribani 500. Shirika la kimataifa la Uhamiaji IOM linasema kuwa idadi ya vifo inaweza kuongezeka na kiwango cha uharibifu [...]
07/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-moon, amewasili nchini Uturuki ambako anatarajiwa kufanya mashauriano na Waziri Mkuu wa nchi hiyo, Tayyip Erdogan na Waziri wa Mambo ya Nje, Ahmet Davutoglu. Katika ziara hiyo, Bwana Ban anatarajiwa kuzuru baadhi ya kambi za wakimbizi wa Syria ambao wamekimbilia usalama wao nchini Uturuki, kufuatia machafuko yalodumu miezi [...]
07/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa kupitia sekretarieti yake ya mabadiliko ya tabia nchi kwa kushirikiana na Kongamano la kidunia la uchumi, WEF wamezindua mpango mpya ujulikanao kama Msukumo wa mabadiliko,uwekezaji fedha katika vitegauchumi rafiki kwa mazingira. Ushirikiano huo umetangazwa huko Doha, Qatar ambako mkutano wa kimataifa wa mabadiliko ya Tabia nchi umemalizika leo na lengo la mpango [...]
07/12/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika muktadha huo, mkuu wa Shirika la kuratibu masuala ya kibinadamu la Umoja wa Mataifa OCHA Valerie Amos yuko nchini Myanmar kutathmini hali ya kibinadamu nchini humo pamoja na athari za mizozo kwenye majimbo ya Kachim na Shan Kaskazini ambayo yamewalazimu watu 75,000 kukimbia makwao tangu kuanza kwa mapigano mwaka 2011. Amos pia atatathmini athari [...]
07/12/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kampeni ya dharura ya kutoa chanjo kwa sasa inaendelea nchini Syria kuwakinga watoto dhidi ya ugonjwa wa surua na polio ikiwa inawalenga watoto milioni 1.4. Kampeni hiyo inaongozwa na Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF na jumla ya chanjo milioni 1.5. UNICEF inasema kuwa hakujakuwa na hakikisho kutoka kwa pande zinazozozana iwapo [...]
07/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Navi Pillay ameelezea wasi wasi wake kutoakana na kunelea kwa kizozo na mauaji kwenye maanbamano ya kupinga katiba nchini Misri ambayo inatarajiwa kuadhinishwa tarehe 15 mwezi huu. Bi Pillay amekaribisha wito wa rais Muhammed Morsi wa kutaka kufanyika kwa mazungumzo lakini akajutia kwamba hakuna hatua yoyote [...]
07/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Idara ya mikasa na masuala ya dharura ya Shirika la Kimataifa la Atomiki, IAEA, imesema inawasiliana na mamlaka husika nchini Japan kufuatia tetemeko la ardhi lililopima kiwango cha 7.3 kwenye chombo cha kupima ukubwa wa tetemeko la ardhi. IAEA imesema viwanda vya nguvu za nyuklia katika maeneo ya karibu na uti wa tetemeko hilo vimeripoti [...]
07/12/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kampeni ya dharura ya chanjo dhidi ya ugonjwa wa homa ya Manjano inaendelea huko Darfur nchini Sudan kwa lengo la kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa huo. Shirika la afya duniani, WHO limesema mlipuko wa sasa wa ugonjwa huo Darfur ni mkubwa kuwahi kutokea sehemu yoyote duniani kwani watu 165 wamefariki dunia hadi sasa tangu mlipuko wa [...]
07/12/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Miezi sita baada ya ghasia za wenyewe kwa wenyewe kuzuka katika jimbo la Rakhine magharibi mwa Myanmar, yapata watu 115, 000 walolazimika kuhama makwao bado wanaishi katika mazingira yenye matatizo, kwa mujibu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi katika Umoja wa Mataifa, UNHCR. Shirika hilo limesema limesambaza vifaa vya misaada kwa takriban thuluthi mbili za jamii [...]
07/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kimataifa la uhamiaji, IOM limepokea dola Elfu 55 kutoka shirika la maendeleo la Uswisi, SDC kwa ajili ya kuanza kazi ya ujenzi wa makazi ya dharura kwa watu 800 waliopoteza makazi yao huko Kivu Kaskazini, Mashariki mwa Jamhuri ya Kideomokrasi ya Congo, DRC. Ujenzi wa makazi hayo unafuatia watu hao kukimbia makwao kutokana [...]
07/12/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »