Nyumbani » 30/11/2012
Entries posted on “Novemba, 2012”
Kusikiliza /

Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya wanawake, UN-WOMEN Michelle Bachelet amesema michango ya mashirika ya wanawake na makundi ya kiraia ya kuzuia na kutatua migogoro duniani ni muhimu katika kuleta amani duniani na hivyo jitihada hizo zinapaswa kuungwa mkono. Amesema hayo wakati akiwasilisha ripoti ya Katibu Mkuu wa umoja wa [...]
30/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Siku ya Ukimwi Duniani ni muda muafaka wa kila jamii, taifa na dunia kwa ujumla kutathmini harakati za kutokomeza ugonjwa huo ambao hadi sasa haujapatiwa tiba, zaidi ya watu kuelimishwa juu ya kinga na wale wanaoishi na virusi vya Ukimwi na Ukimwi kupatiwa dawa za kupunguza makali ya virusi hivyo. Ripoti ya mwaka huu iliyotolewa [...]
30/11/2012 | Jamii: Makala za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa siku ya Alhamisi tarehe 29 Novemba ambayo ni siku ya kimataifa ya kusimama bega kwa bega na Palestina, lilipitisha azimio la kuipatia Palestina hadhi ya uangalizi bila haki ya kupiga kura katika Baraza hilo. Katika kura hiyo ya kupitisha azimio hilo, nchi 138 ziliunga mkono huku Tisa zikipinga na [...]
30/11/2012 | Jamii: Mahojiano | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon, amesema mzozo wa Syria, ambao sasa umeingia mwezi wa 21, umefikia viwango vipya vya kushangaza vya ukatili na machafuko. Bwana Ban amesema hayo wakati akilihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, ambalo pia limehutubiwa na Mwakilishi maalum wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na jumuiya ya [...]
30/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna wa Umoja wa Mataifa juu ya haki za Binadamu Navi Pillay amemtaka rais wa Misri Mohamed Morsi kuangalia upya tamko lililotolewa wiki iliyopita linalohalalisha kuwepo kwa katiba mpya akisema kuwa vipengele vingi kwenye tamko hilo vinakinzana na sheria za kimataifa juu ya haki za binadamu. Kamishna huyo ameonya juu ya jaribio lolote la kupitisha [...]
30/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Jan Eliasson amesema katika kipindi cha miaka 12 iliyopita, Baraza la Usalama la Umoja limeonyesha kuwa maamuzi yanayopitishwa na chombo hicho yanaweza kufanya maisha ya wanawake na watoto wa kike baada ya migogoro kuwa bora zaidi. Bwana Eliasson amesema hayo katika hotuba yake hii leo wakati wa mjadala [...]
30/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Balozi Augustine Mahiga amesema uamuzi wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa wa kuipatia Palestina hadhi ya uangalizi bila haki ya kupiga kura katika Baraza hilo, ni hatua muhimu inayochochea mchakato wa amani Mashariki ya Kati. Balozi Mahiga amesema hayo katika mahojiano na Radio ya Umoja [...]
30/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishina mku wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Navi Pillay ametoa tahadhari kutokana na ghasia zinazoendelea kwenye mji wa Siliana nchini Tunisia ambao ameishauri serikali kuhakikisha kuwa vikosi vya usalama kukoka havitumii nguvu kupita kiasi dhidi ya waandamanaji. Maandamano hayo ya kulalamikia ukosefu wa ajira na kutokuwepo usawa kwenye maendeleo yalianza siku ya [...]
30/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Uchunguzi wa awali uliofanywa kuhusu athari za kiakili kufuatia siku nane za mapigano ya Gaza mapema mwezi Novemba umeonyesha kuwa watoto waliathirika sana kisaikolojia. Zaidi ya watoto mia tano walihojiwa katika uchunguzi huo uliofanyika kati ya Novemba 24 na 25. Zaidi ya asilimia 90 ya watoto chini ya miaka 12 walisema kuwa wanaogopa milio au [...]
30/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kimataifa la Uhamiaji, IOM limesema wahamiaji wanaathirika zaidi na virusi vya ukimwi na Ukimwi hususan katika nchi zenye vipato vya juu. IOM inasema kuwa ripoti ya mwaka huu ya UNAIDS inaonyesha kuwa kwa mara kwanza katika historia ya Ukimwi, maambukizi mapya ya ugonjwa huo katika nchi zilizokuwa na mzigo mkubwa wa maambukizi hayo [...]
30/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la mpango wa chakula duniani WFP linasema kuwa zaidi ya watu milioni 3.5 walio nchini Malawi, Zimbabwe na Lesotho wanahitaji msaada wa chakula kwa muda wa miezi minne ijayo wanapongojea msimu wa mavuno. Kiasi kidogo cha mvua maeneo ya kusini mwa Afrika kimesabisha kushuhudiwa uhaba wa chakula kwenye nchi hizo tatu huku mahitaji yakitarajiwa [...]
30/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kundi la shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR nchini Syria limerejea mjini Damascus baada ya kufanya tathmini ya siku mbili mjini Homs ambapo walisema kuwa maelfu ya watu wanaliohama makwao bado wanaishi kwenye makao yasiyo na njia yoyote ya kupasha joto. Wanasema kuwa nusu ya hospitali hazifanyi kazi na kuna uhaba mkubwa [...]
30/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, limepitisha azimio linaloipatia Palestina hadhi ya uangalizi bila haki ya kupiga kura katika Baraza hilo, azimio ambalo limepitishwa leo siku ambayo ni ya kimataifa ya kusimama bega kwa bega na Palestina. Kazi ya kupiga kura imefanyika Alhamisi jioni ya leo, ambapo nchi 138 ziliunga mkono huku Tisa zikipinga na [...]
29/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mfuko wa kimataifa wa kupambana na Ukimwi, Kifua Kikuu na Malaria umetoa taarifa mpya inayoonyesha ongezeko la idadi ya watu wanaopata dawa za kupunguza makali ya virusi vya Ukimwi duniani pamoja na ikiwemo kutoka kwa mama mjamzito kwenda kwa mtoto. Meneja Mkuu wa mfuko huko Gabriel Jaramillo amenukuu taarifa hiyo mpya inayoonyesha ongezeko la watu [...]
29/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

"Hali ya usalama nchini Syria bado ni mbaya" ni kauli ya mjumbe maalum wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa nchi za kiarabu nchini Syria, Lakhdar Brahimi aliyoitoa mbele ya wajumbe wa Baraza la Usalama la umoja huo mjini New York, Marekani. Bwana Brahimi amewaambia waandishi wa habari kuwa ametoa ujumbe huo alipohutubia [...]
29/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kilimo na mazao la Umoja FAO limeanzisha mpango ambao utawawezesha wenyeji wa taifa la Somalia kunufaika na bidhaa za mifugo kama vile ngozi na mifupa ya ngamia. Baada ya miongo miwili ya vita na ukame, Somalia haijakuwa na viwanda vya nyumbani vinavyoweza kutengeza bidhaa kama vile sabuni. Katika eneo la Somaliland ambalo hakijaathiriwa [...]
29/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto na vita vya silaha, Leila Zerrougui, amepata hakikisho kutoka kwa serikali ya muungano ya Yemen la kukomesha matumizi ya watoto katika jeshi lake. Bi Zerougui ambaye yupo Yemen kukagua hali ya watoto waloathiriwa na mzozo, amekutana na Rais Abd Rabbo Mansour Hadi na Waziri Mkuu, Mohammed Saleh [...]
29/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwenyekiti wa waendesha mazungumzo wa kundi la Afrika Mr. Dlamini Emmanauel ameelezea matumaini kutokana na matokeo ya mkutano kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa yanayoendelea mjini Doha Qatar lakini akasisitiza kuwa kuhudhuriwa kwa vikao na wajumbe kutoka Afrika litakuwa jambo muhimu. Kwenye mkutano wa kwanza na mtaribu wa kituo cha sera kuhusu hali ya hewa [...]
29/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, linatazamiwa kupiga kura ya kuamua kuhusu ombi la Palestina la kutaka kuwa na hadhi ya uangalizi bila haki ya kupiga kura katika Baraza hilo. Kura hiyo muhimu inafanyika leo tarehe 29 Novemba, ambayo ni siku ya kimataifa ya kusimama bega kwa bega na watu wa Palestina. Kabla ya kura [...]
29/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Serikali ya Syria inaripotiwa kutumia mabomu ya kutegwa ardhini kwenye maeneo ya mpaka kati yake na Lebanon pamoja na Uturuki kwa mujibu wa Shirika la kimataifa la kupinga matumizi ya mabomu ya kutegwa ardhini. Mabomu hayo yamekuwa yakilengwa hasa kwa raia wanaojaribu kuvuka mpaka wakikimbia ghasia nchini Syria. Ripoti hiyo inasema kuwa Syria ndilo taifa [...]
29/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la nguvu za atomiki la Umoja wa Mataifa, IAEA, Yukiya Amano leo ametoa ripoti mbele ya bodi ya magavana wa shirika hilo huko Vienna, Austria kuhusu ufuatiliaji wa mipango ya nyuklia huko Iran, Syria na Jamhuri ya Kidemokrasia ya watu wa Korea, DPRK na kueleza wasiwasi wake juu ya mipango ya [...]
29/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakuu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa wamezindua kampeni yenye shabaha ya kulinda na kutetea haki za watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi ambao wanaandamwa na vitendo vya unyanyapaa wawapa kwenye maeneo yao ka kazi. Mkuu wa shirika la kazi ulimwenguni ILO Guy Ryder amesema kuwa kupiga vita vitendo vya unyanyapaa kwenye maene ya kazi [...]
29/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF Anthony Lake amerejelea wito wake wa kutaka pande zote katika mgogoro nchini Syria kuhakikisha zinawalinda watoto nyakati zote. Taarifa ya UNICEF imesema wito wa Bwana Lake unafuatia ripoti za wiki hii kutoka mashirika mbali mbali ikiwemo lile la kutetea haki za binadamu, Human [...]
29/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Majanga na mizozo ya kivita ambayo huathiri zaidi ya watu milioni 200 na kusababisha vifo vya watu zaidi la laki tano duniani kote itakuwa ajenda kuu ya mkutano unaoanza kesho nchini Liberia kuhusu migogoro na hatari za kutumbukia kwenye mizozo . Kongamano hilo likiwa linajikita zaidi kwa bara la Afrika, limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya [...]
28/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, ametangaza leo uteuzi wa Meja Jenerali Leonard Muriuki Ngondi kutoka Kenya kama kamanda wa Ujumbe wa Umoja wa Mataifa Liberia, (UNMIL). Meja Jenerali Ngondi atairithi nafasi ya Meja Jenerali Muhammad Khalid wa Pakistan, ambaye alihitimisha muda wake wa kuhudumu mnamo tarehe 9 Novemba 2012. Bwana Ban ameelezewa [...]
28/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mshindi wa tuzo ya Nobel na mwanaharakati wa haki za Binadamu, Askofu Desmond Tutu, atakabidhiwa tuzo ya heshima kwa mchango wake katika kujenga desturi ya haki za binadamu kote duniani, limetangaza leo Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa, UNESCO. Askofu Tutu alichaguliwa kuipokea tuzo ya mwaka huu ya UNESCO/Bilbao, kwa mchango [...]
28/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Iraq, Martin Kobler ameeleza kusikitishwa kwake na mfululizo wa mashambulizi yanayoendelea dhidi ya raia wasio na hatia ikiwemo waumini nchini humo. Kobler amesema vitendo hivyo visivyo vya kibinadamu vinaongezea machungu na mateso ambayo tayari raia wasio na hatia wanakumbana nayo nchini Iraq. Taarifa ya ujumbe [...]
28/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limepitisha azimio ambalo pamoja na mambo mengine linalaani kitendo cha kikundi cha waasi cha M23 cha kutaka kujaribu kuunda mamlaka isiyo halali na kupuuza serikali ya serikali ya Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo. Azimio hilo limepitishwa bila kupingwa na wajumbe wote 15 wa Baraza hilo la usalama [...]
28/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Maambukizi mapya ya virusi vya HIV miongoni mwa watoto yamepunguwa, lakini kulifikia lengo la kuwa kizazi kisicho na Ukimwi kunahitaji kuwatibu wanawake zaidi waja wazito na watoto, ambao wanaishi na virusi vya HIV, limesema Shirika la Kuhudumia Watoto katika Umoja wa Mataifa, UNICEF, katika ujumbe wake kabla ya siku ya Kimataifa ya Ukimwi, Disemba mosi. [...]
28/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kuyeyuka kwa haraka kwa barafu eneo la kaskazini mwa dunia na hali mbaya ya hewa vyote vinavyoshuhudiwa kote duniani ni ishara tosha kwamba mabadiliko ya hali ya hewa yanaendelea huku ulimwengu ukitazama. Hii ni kwa mujibu Shirika la utabiri wa hali ya hewa duniani WMO kwenye taafira yake ya hivi punde kuhusu hali ya hewa [...]
28/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la Kimataifa la Uchumi likishirikiana na sekritariati ya Umoja wa Mataifa inayohusika na masuala ya mabadiliko ya hali ya hewa, UNFCC, limetangaza uzinduzi wa mkakati wa "Huu ni wakati wa mabadiliko", ambao unahusiana na uwekezaji unaojali mazingira, na ambao unaonyesha mbinu za uwekezaji katika sekta za umma na zile za kibinafsi zinazochangia kujiandaa kwa [...]
28/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mratibu Mkuu wa Masuala ya kibinadamu katika Umoja wa Mataifa Bi. Valerie Amos amesema kuna umuhimu wa jumuiya ya kimataifa kuendelea kusaidia Lebanon wakati huu ambapo inatoa hifadhi kwa maelfu ya wakimbizi wa Syria wanaokimbia mapigano nchini mwao. Bi. Amos amesema hayo leo wakati akizungumza na waandishi wa habari mjini Beirut, Lebanon baada ya mazungumzo [...]
28/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Kazi Duniani ILO limeelezea mshangao wake kutokana na ajali iliyotokea kwenye kiwanda kimoja cha nguo eneo la Ashulia karibu na Dhaka mji mkuu wa Bangladesh ambapo zaidi ya wafanyikazi 100 waliangamia. ILO inatuma rambi rambi zake kwa familia za waathiriwa wa mkasa huo uliotokea mnamo tarehe 24 mwezi huu na pia kuwatakia nafuu [...]
28/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa unasema kuwa wakazi wa nchi zinazoendelea wako katika hatari kubwa zaidi ya kupata madhara yatokanayo na kemikali hatari ambazo hutelekezwa hovyo bila kujali madhara kwa binadamu. Harakati za kupunguza madhara ya kemikali za sumu hasa kwa nchi hizo maskini zinaendelea kuimarishwa katika mikutano mbali mbali ikiwemo unaomalizika leo mjini New York , [...]
28/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa umezitaka serikali pamoja na viongozi mbali mbali duniani kutekeleza ahadi zao za kuhakikisha vitendo vyote vya unyanyasi dhidi ya wanawake vinatokomezwa, ambapo wito huo unatokana na ujumbe wa mwaka huu usemao Ahadi ni Ahadi. Takwimu zinaonyesha kwa katika baadhi ya nchi wanawake kati ya Saba hadi Kumi hukumbwa na vitendo vya [...]
28/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kupinga Silaha za Kemikali, Ahmet Üzümcü, leo wametoa waraka wa pamoja kwa nchi nane zisizo wanachama wa mkataba kuhusu silaha za kemikali. Waraka wa viongozi hao wawili unasisitiza umuhimu wa mataifa yote kutia saini mkataba wa kupinga silaha za kemikali, [...]
27/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa kwenye mchakato wa amani huko Mashariki ya Kati, Robert Serry amesema mwendelezo wa mapigano ya kusikitisha kwenye eneo hilo inadhahirisha vile mamlaka zilizoko zisivyo na mashiko. Akitoa taarifa yake mbele ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo mjini New York, Marekani kuhusu hali ya usalama Mashariki [...]
27/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu misaada ya kibinadamu OCHA kupitia mfuko wake wa utoaji misaada kwa dharura, CERF, imetoa nyongeza ya dola Milioni Tano nukta Tatu kwa ajili ya watu Elfu 36 waliopoteza makazi yao kutokana na ghasia za mwezi Oktoba kwenye jimbo la Rakhine nchini Myanmar. Fedha hizo zitasaidia jitihada za mashirika matano [...]
27/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkutano wa mabadiliko ya hali ya hewa unafanyika Doha, Qatar suala kubwa likiwa ni hatua za kuchukua kupunguza gesi chafuzi zinazochochea ongezeko la joto duniani. Wakati hilo likijdaliwa, shirika la mpango wa Mazingira katika Umoja wa Mataifa, UNEP, limetoa taarifa inayozungumzia uwezekano wa kuyeyuka kwa kasi kubwa kwa udongo wenye barafu, Permafrost, ulioko kwenye maeneo [...]
27/11/2012 | Jamii: Mahojiano | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la mpango wa Mazingira katika Umoja wa Mataifa, UNEP, limeonya kuwa ongezeko la joto duniani huenda likawa juu zaidi ikiwa udongo wenye barafu ulioko kwenye maeneo ya kaskazini mwa dunia utaendelea kuyeyuka kwa kasi ya sasa. Udongo huo, uitwao Permafrost katika lugha ya Kiingereza, umeenea kwa takriban robo ya eneo lote la kaskazini mwa [...]
27/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Utafiti mmoja umebaini kuwepo kwa ongezeko kubwa la usafirishwaji wa ngozi ya chatu inayosafirishwa kwa wingi toka Kusini mwa Asia na kupelekwa eneo la Mashariki. Wananchi wa bara la Ulaya ndiyo wanatajwa kuhusika kwa kiwango kikubwa katika biashara ya ngozi ya chatu wanaotumia kutengeneza bidhaa zinazokwenda na wakati. Inaelezwa kuwa kila kwama wastani wa nusu [...]
27/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na masuala ya haki za binadamu, inamsihi Rais wa Colombia na kiongozi wa bunge la nchi hiyo kuangalia upya mchango wao kwenye marekebisho ya katiba ya nchi hiyo ambayo yanalenga kubadilisha wigo wa mfumo wa mahakama ya kijeshi nchini humo. Msemaji wa ofisi hiyo Cécile Pouilly amewaambia waandishi wa [...]
27/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA linasema kuwa mashirika ya kutoa huduma za kibinadamu yanafanya jitihada za kuwasaidia watu 140,000 kwenye sehemu 12 waliko wakimbizi wa ndani, nje na ndani mwa mji wa Goma. Shirika la Care International limeendesha tathmini kuhusu dhuluma za kijinsia kwenye kambi za wakimbizi ambapo linatarajiwa [...]
27/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR na washirika wake wamerejelea shughuli zao za kuwasaidia wakimbizi wa ndani kwenye maeneo 12 mjini Goma kwenye Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ambapo misaada inatolewa ikiwemo chakula, sabuni na vyombo vya maji. Usambazaji wa misaada ulianza mwishoni mwa wiki ukiwalenga watu 110,000. Hi ndiyo shughuli ya [...]
27/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Serikali ya Ujerumani imehaidi kutoa kiasi cha Euro milioni 12 kusaidia mfuko unaoratibu majanga ya dharura kwa Syria kiasi ambacho kimetajwa kuwa ni kunakubwa kutolewa na nchi moja. Hii ni mara ya kwanza kwa Ujerumani kuhaidi kuchangia mfuko wa majanga ya dharura unaosimamiwa na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na masuala ya utu wema [...]
27/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la uhamiaji la kimataifa, IOM linasema linahitaja dola Milioni Mbili nukta Nane kwa ajili ya kusaidia mpango wa kurejea nyumbani kwa hiari kwa wakimbizi Elfu 37 wa Burundi walioko bado nchini Tanzania. Wakimbizi hao ni kati ya wakimbizi 39,700 wa Burundi waliokuwa wakiishi kwenye kambi mbili za Mtabila na Nyarugusu tangu vurugu za kikabila [...]
27/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amesema ni muhimu viongozi wa dini na wale wa kisiasa wakatumia ushawishi wao kwa maslahi ya umma huku akigusia matukio ya hivi karibuni huko Mashariki ya Kati na Mali yaliyoonyesha faida ya kuendeleza mahusiano mazuri na ya muda mrefu. Amesema mjini Vienna, Austria wakati wa uzinduzi wa [...]
26/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu kwa wakimbizi wa ndani Chaloka Beyani hii leo ameitaka serikali ya Sudan kuongeza jitihada za kupatia suluhisho la kudumu raia wake kwenye maeneo mbali mbali nchini humo waliopoteza makazi. Akizungumza baada ya kuhitimisha ziara yake ya siku Tisa nchini Sudan iliyomkutanisha na watu kutoka pande [...]
26/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu upataji wa haki ya afya, Anand Grover amehitimisha ziara yake ya takribani wiki mbili huko Japan na kusisitiza umuhimu wa kufuatilia madhara ya miali ya nyuklia iliyotokana na ajali ya Fukushima kwa binadamu na wananchi wenyewe kushiriki kuhakikisha wanapata haki hiyo. Hata hivyo Grover amepongeza jitihada za serikali [...]
26/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na elimu, sayansi, na utamaduni UNESCO Bi Irina Bokova amesema kuwa jamii inapaswa kujengewa mustakabala bora ikiwemo pia kujengewa daraja litalounganisha utamaduni wa watu wote. Bi Bokova ambaye alikuwa akizungumza kwenye ufunguzi tamasha moja la kimataifa lililofanyika Uturuki, amesisitiza ulazima wa kuunganisha utamaduni wa mataifa . Tamasha [...]
26/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Idadi ya raia walioathiriwa na tetemeko la ardhi liliikumba Haiti miaka mitatu iliyopita,ambao bado wanaendelea kuishi kwenye makambi inakadiriwa kufikia 357,785 ikiwa imepungua kwa wastani wa asilimia 70 ikilinganishwa na takwimu za awali. Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na uhamiaji IOM Gregoire Goodste anasema kuwa kiwango hicho ni hadi kufikia mwezi Octoba [...]
26/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kiasi kikubwa cha pesa zinazotumwa nyumbani na wahamiaji wafanyikazi kutoka nchini maskini zaidi duniani zinatumika kusimamia gharama ya kutuma kwa mujibu wa ripoti ya shirika la biashara na maendleo la Umoja wa Mataifa UNCTAD. Ripoti hiyo inasema kuwa gharamna ya kutuma pesa kwenda kwa mataifa ya Afrika nI mara tatu zaidi kulingana nakiwango cha wastani [...]
26/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi katika Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, amerejelea ahadi ya shirika hilo kujitolea kukabiliana na dhuluma za ngono na kijinsia, akisema kwamba UNHCR imeongeza juhudi zake mwaka huu kuwasaidia waathiriwa kupata haki. Bwana Guterres amesema, ingawa kuna ufahamu mkubwa wa dhuluma za ngono na jinsia na juhudi za kuzipinga, [...]
26/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Huko Ukanda wa Gaza, shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada kwa wakimbizi wa kipalestina, UNRWA limetoa taarifa kuhusu hali halisi baada ya makubaliano ya kusitisha mapigano kati ya kikundi cha Hamas na Israel na kusema makubaliano hayo yanaonekana kuzingatiwa licha ya mauaji ya mtu mmoja huko Khan Younis eneo lililoko mpakani. Kwa mujibu [...]
26/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ameunga mkono taarifa ya pamoja ya Marais Yoweri Museveni wa Uganda, Paul Kagame wa Rwanda na Joseph Kabila wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ya kuwataka waasi wa kikundi cha M23 walioingia na kusonga katika mji wa Goma, huko Mashariki mwa DRC kuacha mapigano mara moja. Msemaji [...]
26/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ujumbe wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika huko Darfur, UNAMID umeshiriki katika kuleta maendeleo ya kielimu kwenye eneo hilo kwa kuipatia wizara ya Elimu ya Darfur Kaskazini mahema 12 yatakayokuwa madarasa kwa wafugaji wanaohamahama kwenye vitongoji vitano vya eneo hilo. Taarifa ya UNAMID imesema kuwa msaada huo ni sehemu ya miradi [...]
26/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkutano wa 18 wa kimataifa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa umeng’oa nanga hii leo mjini Doha Qatar. Wakati wa ufunguzi wa mkutano huo rais wa vikao Abdullah Bin HamadAL-Attiyah amewaambia wanaohudhuria kuwa madadiliko ya hali ya hewa ni changamoto kubwa kwa ubinadamu na mkutano huo ni fursa muhimu inayostahili kutumika kwa njiia nzuri. [...]
26/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Jopo la Umoja wa Mataifa la kutathmini haki za binadamu, mapema mwezi ujao litakwenda Bahrain kwa mwaliko wa serikali ya nchi hiyo kujadili mfumo wa mahakama nchini humo na uwajibikaji kwa vitendo vya sasa na vilivyopita vya ukikwaji wa haki za binadamu. Msemaji wa Tume ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa Rupert Colville [...]
23/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna Mkuu wa Tume ya Umoja wa Mataifa ya Haki za binadamu, Navi Pillay ameeleza wasiwasi wake mkubwa juu ya hukumu ya kifo dhidi ya wafungwa 14 nchini Afghanistani iliyotekelezwa tarehe 20 na 21 mwezi huuu. Taarifa ya Tume ya haki za binadamu inasema kuwa Rais Hamid Karzai ameripotiwa kuidhinisha adhabu ya kifo kwa wafungwa [...]
23/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF linasema kuwa karibu wakimbizi wa ndani 140,000 wanaishi kwenye shule tatu za umma, kituo cha Don Bosco na kwa kambi tatu za wakimbizi wa ndani mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. UNICEF inasema kuwa watoto wako kwenye hatari ya maradhi ya kuambukiza yakiwemo kipindupindu kutokana na [...]
23/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Huku hali kwenye mji wa Goma ikibaki kuwa tete , uwanja wa ndge ambao ndio tegemeo la wafanyikazi wa kutoa huduma za kibinaadamu umebaki umefungwa na kufanya utoaji wa huduma na misaada kuwa mgumu. Mapigano makali kati ya makundi ya FARDC na M23 eneo la Masisi Magharibi mwa Goma yamesababisha kuhama kwa watu zaidi . [...]
23/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Huku siku ya kimataifa ya kupinga dhuluma dhidi ya wake ikitarajiwa kuadhimishwa tarehe 25 mwezi huu Shirika la afya duniani linasema kuwa bado wanawake 3 kati ya wanawake 10 wanapitia dhuluma nyingi duniani. WHO inasema kuwa dhuluma ya kimapenzi ndiyo inayotumika zaidi kama silaha. WHO Inasema kuwa hata kama upashaji tohara umepungua duniani bado watoto [...]
23/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la chakula na kilimo duniani, FAO na serikali ya Haiti zinatafuta dola Milioni 74 katika kipindi cha mwaka mmoja ujao kwa ajili ya kurekebisha sekta ya kilimo nchini humo iliyoharibiwa na mfululizo wa majanga ya asili tangu kuanza kwa mwaka huu. Majanga hayo ni vimbunga Sandy na Isaac pamoja na ukame ambayo yamefanya Haiti [...]
23/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalam huru wa Umoja wa Mataifa, Virginia Dandan, ametoa wito kwa serikali zote duniani ziangalie gharama ya mabadiliko ya hali ya hewa kuwa zaidi ya fedha, na kuchukua msimamo wa pamoja wa kimataifa kama sehemu muhimu ya mafanikio ya mijadala ya Umoja wa Mataifa kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa, ambayo itaanza wiki ijayo [...]
23/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa Tume ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa Navi Pillay amesema mtoto Malala Yousfzai atakuwa ametendewa haki zaidi iwapo harakati zake za kutafuta haki ya elimu kwa mtoto wa kike zitaendelezwa zaidi ya kile kilichofanywa sasa baada ya yeye kunusurika kuuawa. Katika taarifa yake kwa siku ya kimataifa ya kutokomeza aina zote [...]
23/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM limetoa ombi la dola milioni 5.3 kwa jamii ya kimataifa fedha ambazo zitasaidia katika utaoji wa huduma za kibinidamju kwa kati ya wakimbizi wa ndani 120,000 na 140,000 miezi mitatu inayokuja, kwenye eneo ya Orientale na katika mikoa ya Kivu kaskakzini na kusini nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya [...]
23/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema hivi sasa linakusanya zaidi ya vifurushi Laki moja vya nguo za watoto wa wakimbizi huko Syria wakati huu ambapo msimu wa baridi kali unawadia. Msemaji wa UNICEF Marixie Mercado amesema wanakusanya pia mablanketi Laki Moja na Sitini ikiwemo ya watoto hao wa wakimbizi pamoja na [...]
23/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Siku ya Jumanne tarehe 20 mwezi huu iliripotiwa kuwa waasi wa kikundi cha M23 huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC waliingia na kusonga ndani ya mji wa Goma. Siku hiyo hiyo usiku Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lilipitisha azimio kuhusu DRC ambapo pamoja na mambo mengine limetaka waasi wa kikundi cha M23 [...]
22/11/2012 | Jamii: Makala za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, amekaribisha tangazo la kusitisha mapigano katika Gaza na kusini mwa Israel, na kuzipongeza pande zote katika mzozo huo kwa kufanya hivyo, pamoja na Rais Morsi wa Misri kwa uongozi wake mzuri. Akilihutubia Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, ambalo limefanya kikao maalum kuhusu hali ya Mashariki [...]
21/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto na maeneo ya vita vya silaha, Leila Zerrougui, ameelezea kusikitishwa kwake kuhusu hali ya watoto katika mzozo unaoendelea mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, DRC. Kuingia kwa waasi wa M23 katika miji ya Goma na Sake, kumeambatana na ukiukaji mkubwa unaotekelezwa dhidi ya [...]
21/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Tume ya muungano wa Afrika pamoja na Shirika la kilimo na mazao la Umoja wa Mataifa FAO kwa ushirikiano na shirika la Lula nchini Brazil wametangaza leo kuwa wataungana kusaidia kumaliza njaa na ukosefu wa lishe barani Afrika. Uamuzi huo ulafikiwa kwenye mkutano kati ya mweyekiti wa tume ya muugano wa Afrika Nkosazana Dlamini Zuma, [...]
21/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, Irina Bokova amelaani mauaji ya mwandishi wa habari Adrian Silva Moreno wa Mexico na kutaka uchunguzi ufanyike kuhusu chanzo cha mauaji hayo na ya afisa wa zamani wa polisi Misray López González. Bi. Bokova ambaye shirika lake lina wajibu wa kutetea [...]
21/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Juhudi zaidi zinahitajika kuhusu mabadiliko ya hali ya hewa bila kuchelewa ikiwa ulimwengu bado unataka kuwa na nafasi ya kuzuia viwango wastani vya joto kupanda kwa zaidi ya nyzui 2 katika karne hii. Kwa mujibu wa ripoti ya Shirika la Mpango wa Mazingira katika Umoja wa Mataifa, UNEP na Wakfu wa Hali ya Hewa ya [...]
21/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa leo limepokea ripoti ya hali ya usalama na mustakhbali wa amani na maendeleo ya kudumu katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC, ripoti iliyowasilishwa na Mkuu wa kikosi cha umoja wa Mataifa cha kulinda amani na kuweka utulivu nchini humo, Roger Meece. Akiwasilisha ripoti hiyo ya Katibu [...]
21/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mratibu wa masuala ya misaada ya kibinadamu nchini Myanmar, Ashok Nigam, leo amezindua mpango mpya wa kuitikia mahitaji ya dharura ya kibinadamu katika jimbo la Rakhine, Myanmar. Wakati wa uzinduzi huo, Bwana Nigam, ambaye aliandamana na waziri wa masuala ya mipaka Myanmar, Jenerali Thein Htay, ameishukuru jamii ya kimataifa kwa mchango wake kufikia sasa, [...]
21/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mfuko wa kimataifa unaofadhili vita dhidi ya ugonjwa wa Ukimwi, Kifua kikuu na Malaria hii leo umesaini makubaliano na Shirika la maendelo la Umoja wa Mataifa UNDP ya kurejelea tena programu za kupambana na ugonjwa wa Ukimwi hasa matibabu ya ugonjwa huo kwa maelfu ya watu nchini Mali. Kupitia makubaliano hayo mfuko huo uliidhinisha ufadhili [...]
21/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishina mkuu wa Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA Filipo Grandi ametembelea Gaza kujionea mwenyewe uharibifu uliofanywa na pia kukagua huduma za wafanyikzi wa UNRWA. Bwana Grandi amekutana na wakimbizi na kuzungumza na wafanyikazi kwenye kituo cha Jabalia ambapo alielezea kuridhika kwake na kazi inayoendelea. Bwana Grandi alisisitiza kuwa hatua [...]
21/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki- Moon ambaye yuko ziarani Mashariki ya Kati kupatia suluhu mzozo kwenye eneo hilo, ameshutumu vikali shambulio lililotokea leo kwenye basi moja huko Tel Aviv, Israel na kusababisha watu Kumi kujeruhiwa. Msemaji wa Bwana Ban, amemkariri Katibu Mkuu huyo akielezea kusikitishwa na kushtushwa na taarifa za shambulio [...]
21/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la afya duniani, WHO linaomba dola Milioni Kumi kwa ajili ya ununuzi wa vifaa tiba na dawa za kutumika kwenye vituo vya afya huko Ukanda wa Gaza ambako idadi ya wagonjwa imeongezeka kutokana na mapigano yanayoendelea huku vituo vya afya vikiripotiwa kushambuliwa. Mkuu wa ofisi ya WHO huko Gaza Dkt, Mahmoud Daher ameiambia Radio [...]
21/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yanayotoa huduma za kibinadamu Sudan Kusini yamesema yatahitaji dola bilioni 1.1 za kimarekani ili kukabiliana na mahitaji ya kibinadamu yanayozidi kuongezeka nchini humo mwaka ujao wa 2013. Afisi ya mratibu mkuu wa misaada ya kibinadamu katika Umoja wa Mataifa (OCHA) imesema kuwa idadi kubwa ya watu Sudan Kusini bado wamo [...]
21/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »

Suala la udhibiti wa mipaka ya nchi za Umoja wa Ulaya litakuwa ajenda ya kipaumbele wakati wa ziara ya mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za wahamiaji, François Crépeau huko Ugiriki kuanzia Jumapili ijayo. Akizungumzia ziara hiyo ya siku tisa, Crepeau amesema anakwenda Ugiriki kwa kuwa nchi hiyo imekuwa kituo muhimu kinachotumiwa na [...]
21/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limepitisha kwa kauli moja azimio linaloshutumu vikali kitendo cha waasi wa kikundi cha M23 kuingia na kusonga ndani ya mji wa Goma huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na kutishia usalama wa raia. Azimio hilo limepitishwa kwa kauli moja jumanne usiku na wajumbe wote 15 wa [...]
20/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ameitaka Israel kujizuia katika operesheni zake huko Ukanda wa Gaza huku akisema kuwa vifo vya raia havikubaliki katika mazingira yoyote. Bwana Ban amesema hayo katika mkutano na waandishi wa habari mjini Jerusalem baada ya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Israeli, Benjamin Netanyahu, mkutano ambao pia ulihudhuriwa na [...]
20/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Waasi wa kikundi cha M23 wameripotiwa kuingia mji wa Goma, ulioko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo. Msemaji wa Umoja wa Mataifa Eduardo Del Buey amewaambia waandishi wa habari mjini New York, Marekani kuwa hali katika mji wa Goma sasa ni mbaya na kwamba waasi hao wamekuwa wakisonga mbele licha ya wito wa Baraza [...]
20/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »

Ripoti mpya kuhusu mabadiliko ya tabianchi inadokeza kuwa muda unatokomea kuweza kupunguza madhara yatokanayo na mabadiliko ya tabianchi. " Turn down the Heat" au punguza kiwango cha joto, ni jina la ripoti hiyo iliyoandaliwa na taasisi ya mabadiliko ya tabianchi ya Potsdam kwa ajili ya Benki ya Dunia na inaeleza kuwa kiwango cha juu cha [...]
20/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la mpango wa chakula duniani, WFP limesema uhaba wa fedha ulisababisha lishindwe kuandaa kiwango cha kutosha cha msaada wa chakula kwa ajili ya wakazi wa maeneo yaliyoko kwenye mkondo wa kimbunga huko Madagascar. Msemaji wa WFP Elizabeth Byrs amesema kutokana na hali hiyo wanaomba wahisani dola Milioni Sita nukta Moja kwa ajili ya msaada [...]
20/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa juu ya haki za binadamu nchini Mynmar amekaribisha aamuzi wa serikali ya nchi hiyo iliyohaidi kuendesha mageuzi yenye shabaha ya kuleta usawa na kuzingatia masuala yanayohusu haki za binadamu. Tomás Ojea Quintana amesema kuwa uamuzi wa serikali ya Myanmar iliyokubali kupitia upya baadhi ya vifungu na sheria zake ikiwemo zile [...]
20/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mpango wa pamoja wa Umoja wa Mataifa wa kupambana na Ukimwi, UNAIDS umemteua mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel, Aung San Suu Kyi kuongoza harakati za dunia za kupinga vitendo vya unyanyapaa dhidi ya watu wanaoishi na virusi vya Ukimwi na Ukimwi. Taarifa ya UNAIDS inasema tayari Bi. Suu Kyi amekubali jukumu hilo wakati [...]
20/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ukuaji endelevu, wenye usawa na ambao unawahusisha wote unahitajika ili kufikia malengo ya maendeleo ya milenia na malengo ya kichumi na kijamii ya ushirikiano wa maendeleo barani Afrika, NEPAD. Huo ndio ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, leo kwenye siku ya viwanda barani Afrika. Bwana Ban amesema mwaka huu, siku ya [...]
20/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kiwango cha gesi inayochafua mazingira iliyo hewani kilivunja rekodi mwaka 2011 kwa mujibu wa ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa hii leo kabla ya kuanza kwa mazungumzo kuhusu mabadiliko ya mhali ya hewa juma lijalo. Shirika la utabiri wa hali wa hewa duniani WMO ambalo ndilo lilolotoa ripoti hiyo linasema kuwa kati ya mwaka [...]
20/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ripoti mpya ya mpango wa Umoja wa Mataifa wa kupambana na Ukimwi, UNAIDS imeonyesha kupungua kwa zaidi ya asilimia 50 ya maambukizo mapya ya virusi vya Ukimwi katika nchi 25 duniani hususan zile zilizokuwa zikiongoza kwa maambukizi mapya. Kwa mujibu wa ripoti hiyo mafanikio hayo yanatokana na kuimarishwa kwa hatua za kinga dhidi ya maambukizi [...]
20/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mashirika ya kutoa huduma za binadamu yamesitisha kwa muda oparesheni zake kwwenye maeneo ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo wakati mapigano yanapochacha mjini Goma na vitongoji vyake. Mashirika mengi yanayotoa huduma nchini Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo yana vituo vyao mjini Goma. Mapigano yamechacha kwa muda wa juma moja lililopita ambapo wanachama wa [...]
20/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa anaendelea na ziara yake Mashariki ya Kati yenye lengo la kupatia suluhu mzozo kati ya kikundi cha Hamas na Israeli ambapo hii leo amesisitiza tena azma yake ya kuwa mapigano yanayoendelea kati ya pande mbili hizo huko Ukanda wa Gaza hayatafanya upande wowote kuwa salama. Bwana Ban amesema hayo [...]
20/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wataalamu watano wa ngazi za juu katika masuala ya haki za watoto kwenye Umoja wa Mataifa wamezishauri serikali kuchukua hatua zaidi za kulinda haki za watoto kutokana na dhuluma za kila aina, kuzuia ukiukaji wa haki dhidi ya watoto na kuwafikisha mbele ya sheria wale wanao wadhulumu kimapenzi watoto na kuwatumia kwemye mizozo. Kwenye maadhimisho [...]
20/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa Tume ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa Navi Pillay ameelezea wasiwasi wake kuhusu kuzorota kwa hali ya usalama na ukiukwaji wa haki za binadamu huko Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo. Msemaji wa tume hiyo, Rupert Colville amemkariri Bi. Pillay akisema kuwa kitendo cha waasi wa M23 kusonga kwenye mji wa Goma, [...]
20/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu, Navi Pillay, ameelezea masikitiko yake kuhusu hali ya raia waliobaniwa kwenye mzozo kati ya Israel na Palestina Gaza na kusini mwa Israel. Bi Pillay ameelezea kushangazwa kwake na kuongezeka kwa idadi ya raia wa Palestina, wakiwemo wanawake na watoto, ambao wameuawa au kujeruhiwa katika kipindi cha masaa 48 yaliyopita [...]
20/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amesema Yemen ishikilie vyema maendeleo ya amani yaliyopatikana nchini humo kwa kipindi cha mwaka mmoja tangu kutiwa saini kwa makubaliano yaliyosaidia kumaliza ghasia nchini humo na kuelekea kwenye kipindi cha mpito cha demokrasia. Bwana Ban amesema hayo mjini Sana'a, Yemen wakati wa mkutano na waandishi wa habari [...]
19/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon yuko nchini Misri ikiwa ni sehemu ya ziara yake huko Mashariki ya Kati ambayo pamoja na mambo mengine inalenga kushughulikia mapigano yanayoendelea hivi sasa huko Ukanda wa Gaza kati ya Palestina na Israel. Msemaji wa Bwana Ban amewaeleza waandishi wa habari kwa njia ya simu kutoka mji [...]
19/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Jan Eliasson amesisitiza umuhimu wa mataifa yote duniani kushirikiana kukabiliana na vitendo vya uharamia ili kuhakikisha usalama wa mabaharia, wavuvi, abiria na wakati huo huo kulinda sekta ya utalii na uvuvi. Bwana Eliasson amesema hayo leo wakati akitoa taarifa mbele ya Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa [...]
19/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa Tume ya Haki binadamu ya Umoja wa Mataifa, Navi Pillay amesifu hatua ya Umoja wa nchi za kusini-mashariki mwa Asia, ASEAN ya kuridhia azimio la haki za binadamu huku hata hivyo akieleza wasiwasi wake kuwa nyaraka hiyo imetumia baadhi ya maneno ambayo yanaifanya isikidhi viwango vya kimataifa. Kauli ya Pillay imekuja baada ya [...]
19/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Uzalishaji wa mchele kote duniani kwa mwaka 2012 unabashiriwa kuwa utazidi matumizi yake kati ya mwaka huu na mwaka ujao, na hivyo kuwepo tani milioni tano zaidi za nafaka hiyo inayotegemewa na wengi mwaka wa 2013, limesema Shirika la Chakula na Kilimo, FAO. Kwa mujibu wa chombo cha kufuatilia soko la mchele, RMM, maghala ya [...]
19/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Huku ulimwengu ukiadhimisha siku ya choo duniani mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki ya kuwa na maji ya kunywa na usafi wa mazingira Catarina de Albuquerque amesema kuwa huenda suala la usafi lisiafikiwe kuambatana na lango la maendeleo ya milenia la kupunguza umaskini ifikapo mwaka 2015. Mjumbe huyo amesema kuwa suala la usafi [...]
19/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Huku ghasia zikizidi kuchacha kwenye ukanda wa Gaza Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA liwekuwa likitumia mfumo wake wa mawasiliano ya runinga kwa njia ya satellite kuwapa mafunzo karibu watoto 250,000 katika eneo hilo. Runinga hiyo ijulikanayo kama UNRWA TV ni ya kwanza na ya aina yake ya Umoja wa [...]
19/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchini Mauritania, waandishi wa habari wanawake kutoka radio, magazeti na wale wanaochapisha habari kwenye intaneti v wamepatiwa mafunzo kuhusu maadili na kanuni za uandishi wa habari. Mafunzo hayo ya siku nne yaliyoendeshwa na programu ya kimataifa ya kuendeleza mawasiliano, IPDC kwa msaada wa shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, yalilenga [...]
19/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu misaada ya kibinadamu, OCHA imesema hali ya usalama kwenye mji wa Goma ulioko Mashariki mwa Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo, DRC ni mbaya kwa kuwa kikundi cha waasi cha M23 kimetishia kuingia na kufanya vurugu. Afisa wa habari wa OCHA kwa DRC Yvon Edoumou amesema maelfu ya wakazi wa [...]
19/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada na ulinzi kwa wakimbizi wa kipalestina, UNRWA limesema hali ya usalama na kibinadamu huko Ukanda wa Gaza ni mbaya. Msemaji wa UNRWA Christopher Gunnes akizungumza na radio ya Umoja wa Mataifa hii leo amesema wanachoshuhudia hivi sasa ni maroketi yakirushwa kwenye eneo hilo la Gaza ambalo nusu [...]
19/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ametoa taarifa yake kuhusu mapigano yanayoendelea huko Ukanda wa Gaza kati, na kuelezea kusikitishwa kwake na vifo vya raia vinavyoendelea kuripotiwa na kutaka pande husika ziache mara moja mapigano hayo. Bwana Ban amesema kuendelea kwa mapigano hayo kutasababisha ongezeko la machungu kwa raia hususan wanawake na watoto [...]
19/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya duniani, WHO Dkt. Margaret Chan amesema kamwe shirika lake halipokei fedha zozote kutoka kampuni za kutengeneza vyakula na vinywaji ili kusaidia kupambana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama vile saratani na moyo. Dkt. Chan amesema licha ya kwamba magonjwa hayo husababisha asilimia 63 ya vifo vyote vinavyotokea kwa mwaka [...]
19/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wanachama wa Baraza la Usalama, wamelaani vikali mashambulizi ya waasi wa M23 mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo kwenye maeneo ya Kibumba, Mboga na Ruhondo, pamoja na kuendelea kuukaribia mji wa Goma. Katika azimio lililofikiwa baada ya kikao maalum mjini New York siku ya Jumamosi, wanachama hao wa Baraza la Usalama pia wamewataka waasi [...]
17/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Tatizo la watoto kuzaliwa njiti au kabla ujauzito haujatimiza wiki 37 linaongoza kwa kusababisha vifo vya watoto wachanga Milioni Moja duniani kote, wakati ambapo asilimia 75 ya watoto hao wanaweza kuokolewa kwa kutumia teknolojia rahisi na kwa gharama nafuu. Huo ni ujumbe wa leo ambayo ni siku ya kimataifa ya kupambana na vifo vya watoto [...]
17/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la Usalama, leo kwa kauli moja limeazimia kuongeza muda wa kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa katika eneo la Abyei (UNISFA) hadi tarehe 31 Mei 2013. Eneo la Abyei lililoko kwenye mpaka kati ya Sudan na Sudan Kusini, limekuwa likizozaniwa kwa muda na nchi hizo mbili. Baraza hilo la Usalama pia limezitaka [...]
16/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR limesema katika kipindi cha wiki mbili sasa zaidi ya wakimbizi Elfu mbili wa Sudan wamewasili katika makazi ya Yida kukwepa mapigano nchini mwao. UNHCR limesema hivi sasa watumishi wake wanafuatilia njia ya kwenda mpakani na wanasafirisha wakimbizi walio hatarini zaidi kuelekea kambi hiyo ya Yida na [...]
16/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Migogoro inayoendelea sehemu mbali mbali duniani husababisha watu kutafuta hifadhi nchi za jirani kwa ajili ya usalama wao na maisha yaweze kuendelea. Barani Afrika mizozo katika nchi za maziwa makuu imefanya watu kukimbia makwao mathalani huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo. Katika matukio mengi wanaopata matatizo ni wanawake na watoto. Eneo la Cibitoke liko [...]
16/11/2012 | Jamii: Makala za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Jopo kubwa zaidi la wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa hii leo limetaka umoja wa nchi za kusini-mashariki mwa Asia, ASEAN kuhakikisha kuwa azimio la haki za binadamu kwa eneo hilo linalotarajiwa kuridhiwa na nchi hizo kwenye kikao chao cha Jumapili huko Cambodia, linazingatia viwango vya kimataifa vya haki za binadamu. Michael Forst ambaye ni [...]
16/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Lengo la kutokomeza umaskini halitofikiwa bila kufanya mazingira kuwa jambo la kipaumbele, kwa mujibu wa Mshauri Maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu Malengo ya Maendeleo baada ya mwaka 2015, Bi. Amina J Mohammed. Bi Mohammed amesema hayo wakati wa ziara yake kwenye ofisi za Umoja wa Mataifa mjini Nairobi, ambako amehutubia maafisa [...]
16/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la uhamiaji la kimataifa, IOM limechukua hatua kukabiliana na mlipuko wa ugonjwa wa Kipindupindu huko Haiti ulioibuka baada ya kimbunga Sandy. IOM imesema tayari imetoa takribani vitita Elfu Kumi vyenye tembe na vifaa vingine vya tiba ya ugonjwa huo ambavyo vimesambazwa wiki hii katika kambi 31 kwenye eneo la mijini na mikoa mingine huko [...]
16/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amesema maelezo wanayopata wageni kuhusu shughuli za umoja huo pindi wanapotembelea makao makuu yake mjini New York, yamesaidia kutoa picha halisi na kwa wakati muafaka kuhusu chombo hicho na kuepusha taarifa zisizo sahihi. Bwana Ban amesema hayo wakati wa sherehe za kuadhimisha miaka 60 ya shughuli ya [...]
16/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa Navi Pillay amesema mwelekeo uliochukuliwa na utawala wa Cambodia katika wakati mataifa ya eneo la Asia na Pacific yakijiandaa na mkutano wa kilele wa ASEAN unatia shaka. Duru kutoka Cambodia zinasema kuwa maafisa wa serikali wamekuwa wakifuatilia kwa karibu utendaji kazi pamoja na shughuli za mashirika [...]
16/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamshna Mkuu wa haki za binadamu Navi Pillay ameelezea masikitiko yake juu ya taarifa kuwa Pakistani imetekeleza kwa mara ya kwanza adhabu ya kunyonga hadi kifokatika hukumu iliyotolewa miaka minne iliyopita. Hukumu hiyo iliyotolewa mwaka 2008 na mahakama ya kijeshi dhidi ya askari mmoja ambaye alidaiwa kumua bossi wake. Taasisi za kimataifa ikiwemo kamishana ya [...]
16/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Serikali ya Ujerumani imetoa kiasi cha euro 500,000 ili kulipiga jeki shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na uhamiaji IOM ambalo limechukua jukumu la kuzisaidia zaidi ya familia 38,000 zilizoathiriwa na mafuriko huko Kusin na Magharibi mwa Chad. Mafariko hayo ambayo ni mabaya kulikumba taifa hilo yamesababisha vifo vya watu 20 na kuharibu nyumba zinazokadiriwa [...]
16/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa imeelezea wasi wasi wake kutokana na ripoti za kuhangaishwa, kudhulumiwa, kukamatwa na kufungwa kwa watu wanaokisiwa kuwa wasagaji au mashoga nchini Cameroon. Sheria za sasa nchini Cameroon zinaharamisha uhusiano baina ya watu wa jinsia moja na inaruhusu hadi kifungo cha miaka mitano pamoja na faini. Sheria [...]
16/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kimataifa la uhamiaji, IOM leo linazindua kituo cha radio ya kijamii kwenye mji wa Kakuma, kaskazini-Magharibi mwa Kenya kwa lengo la kusaidia kuwepo utengamano miongoni mwa wakimbizi waliko kwenye kambi ya Kakuma na wenyeji wa kabila la kiturkana wanaoishi eneo hilo. Hatua hiyo inatokana na migogoro ya mara kwa mara kati ya wakimbizi [...]
16/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa inasema kuwa ni jambo lisilokubalika kuwa raia ndio wanaondelea kuhangaika kufuatia msukosuko uliopo kati ya serikali ya Israel na utawala wa Palestina. Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Navi Pillay anasema kuwa usalama wa raia ni jukumu la pande zote husika kuambatana na [...]
16/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kundi la kimataifa la kuratibu masuala ya chanjo, ICG limekubali ombi la serikali ya Sudan la kusaidia chanjo kwa ajili ya kinga dhidi ya ugonjwa wa homa ya manjano uliolipuka kwenye vitongoji 23 vya jimbo la Darfur. Ugonjwa huo umejikita katika maeneo ya Kati, magharibi, Kusini, Kaskazini na Mashariki mwa jimbo hilo ambapo hadi Jumanne [...]
16/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Migogoro baina ya nchi za Afrika juu ya matumizi ya pamoja ya maji inaweza kupatiwa muarobaini kwa kutumia mkataba wa uhifadhi na matumizi ya pamoja ya maji ya Tume ya Umoja wa mataifa kwa masuala ya uchumi ya Ulaya, UNECE uliotumika kwa miaka 20 sasa. Mkataba huo ulijadiliwa katika kongamano la pili la Afrika kuhusu [...]
16/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuhusu unyanyasaji wa kingono katika maeneo yenye migogoro, Zainab Hawa Bangura ameshutumu vikali matukio ya kubakwa kwa wanawake na watu kukatwa viungo vyao vya siri huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC. Kauli ya Bi. Bangura inafuatia ripoti ya kuwepo kwa vitendo mbali mbali vya unyanyasaji [...]
15/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Afisa mwandamizi wa Umoja wa Mataifa Susana Malcorra amesisitiza kuwa ripoti kuhusu yaliyojiri nchini Sri Lanka katika miezi ya mwisho ya vita vya wenyewe kwa wenyewe itatumiwa kuimarisha zaidi utendaji wa umoja huo hususani katika kusaidia wale wenye mahitaji. Bi. Malcorra amesema hayo alipozungumza na waandishi wa habari mjini New York, Marekani leo kuhusu ripoti [...]
15/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada na ulinzi kwa wakimbizi wa kipalestina, UNRWA limekanusha madai kuwa watumishi wake wa kimataifa wanaondoka Ukanda wa Gaza. Msemaji wa UNRWA huko Gaza Adnan Abu Hasna amesema hayo huku akiongeza kuwa hali mbaya ya usalama imelazimu wasitishe shughuli zote za elimu ikiwemo kufunga shule hadi hali ya [...]
15/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Jopo la wataalamu wa Umoja wa Mataifa limetaka Iran kufanya uchunguzi huru na wa kina usioegemea upande wowote kuhusu kifo cha bloga mashuhuri Sattar Behesthi kilichotokea akiwa kizuizini na uchunguzi huo uangalie madai ya kuwepo kwa utesaji na ripoti iwekwe hadharani. Mmoja wa wataalamu hao huru wanaochunguza haki za binadamu, uhuru wa kujieleza na utesaji [...]
15/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Leo ni siku ya falsafa duniani, siku inayosherekewa na Shirika la elimu , Sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO kila tarehe 15 mwezi Novemba. Kauli mbiu ya siku ya mwaka huu ni "vizazi vijavyo". Kwenye makao makuu mjini Paris UNESCO inatarajiwa kupanga majadiliano kuhusu vizazi vijavyo na vijana. Vizazi vijavyo ndiyo itakuwa [...]
15/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakimbizi wa Burundi walioko nchini Tanzania katika kambi ya Mtabila wameanza kurejea nyumbani kutii agizo lilitolewa na serikali ya nchi hiyo ambayo inakusudia kuifunga kambi hiyo ifikapo mwishoni mwa mwaka huu. Hadi sasa kiasi cha wakimbizi wapatao 8,9994 wameondoka kwenye kambi hiyo iliyoko mkoani Kigoma na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na wakimbizi UNHCR [...]
15/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika ujumbe mwingine, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, ametoa wito kwa raia wa Sierra Leone wahakikishe kuwa moyo wa amani ambao umekuwepo katika harakati za uchaguzi kufikia sasa, utadumishwa hata kwenye siku ya uchaguzi, kuhesabu kura na wakati matokeo yatakapotangazwa. Taifa la Sierra Leone linajiandaa kufanya uchaguzi wa tatu tangu kumalizika vita [...]
15/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, ameelezea kusikitishwa kwake kuhusu hali inayozidi kuzorota kusini mwa Israel na Ukanda wa Gaza, na ambayo imehusisha makombora kurushwa kiholela kutoka Gaza yakiilenga Israel, na mauaji ya kulenga ya mwanajeshi wa Hamas na jeshi la Israel. Bwana Ban amerejelea ujumbe wake wa kulaani vikali mashambulizi ya makombora [...]
15/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Idadi ya vifo vitokanavyo na homa ya manjano huko Darfur, Sudan imeongezeka na kufikia 110 huku idadi ya wagonjwa nayo pia ikiongezeka na kufikia 374. Takwimu hizo ni kwa mujibu wa shirika la afya duniani, WHO ambalo katika ripoti yake kuhusu hali halisi ya ugonjwa huo hadi juzi inaonyesha kuwa ugonjwa huo umeenea katika vitongoji [...]
15/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kazi duniani ILO limeyataja mataifa ya Argentina, Cambodia, Ethiopia, Fiji na Peru kama mataifa yanayokiuka zaidi haki ya kuhusiana kwenye orodha ya nchi 32 zinazotajwa kuwa zinazokiuka haki ya watu kuhusiana. Kamati ya ILO inayohusika na masusla ya haki ya kuhusiana ilichunguza masuala yanayohusu haki za waajiri na vyama vya wafanyikazi za kupanga [...]
15/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limesema zoezi la kurejesha makwao wakimbizi wa Burundi walioko kwenye kambi ya Mtabila nchini Tanzania linatia moyo ambapo wakimbizi wanajitokeza kwa hiari kutii agizo la serikali ya Tanzania la kuwataka warejee makwao kwa kuwa inakusudia kufunga kambi hiyo mwishoni mwa mwaka huu baada ya amani kurejea [...]
15/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika hatua nyingine, UNEP wiki ijayo itatoa ripoti yake mpya zaidi juu tofauti ya viwango vya utoaji wa gesi chafuzi duniani, ikiwa ni siku chache kabla ya kuanza kwa mkutano wa Umoja wa Mataifa wa mabadiliko ya tabia nchi huko Doha, Qatar. Ripoti hiyo inaweka bayana kuwa viwango vya utoaji gesi chafuzi zinazoharibu tabaka [...]
15/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ripoti mpya iliyoandaliwa na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na mazingira, UNEP na washirika wake imebaini uhusiano kati ya uthabiti wa kiuchumi wa nchi ikiwemo uwezo wake wa kulipa au kurejesha madeni na uharibifu wa maliasili kama vile misitu, mazao ya samaki na ardhi. Ripoti hiyo itakayowasilishwa Jumatatu ijayo wakati wa tukio maaluum huko [...]
15/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu, OCHA limesema kadri siku zinavyosonga, mahitaji ya kibinadamu nchini Syria yanaongezeka huku uwezo wa kifedha kukidhi mahitaji hayo ukipungua. Toleo la leo la jarida la masuala ya kibinadamu la OCHA, limesema watu Milioni nne nchini Syria watahitaji misaada ya kibinadamu mapema mwakani, iwapo hali ya [...]
14/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa hii leo umefanya kumbukumbu ya mwaka kwa wafanyakazi wake waliokufa wakiwa kazini ambapo kipindi husika ni kati ya Novemba Mosi mwaka jana hadi Novemba 30 mwaka huu. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon aliongoza shughuli hiyo akiungwa mkono na Rais wa Baraza kuu la Umoja huo na yule wa Baraza [...]
14/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa ukanda wa Sahel barani Afrika, Romano Prodi amesema jumuiya ya kimataifa inapaswa kuonyesha kuwa inajali eneo hilo ambalo linakumbwa matatizo lukuki ikiwemo ukame, njaa na mzozo huko Mali. Prodi ambaye ni Waziri Mkuu wa zamani wa Italia amesema hayo alipozungumza na waandishi wa habari juu [...]
14/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa ukanda wa Sahel barani Afrika, Romano Prodi amesema jumuiya ya kimataifa inapaswa kuonyesha kuwa inajali eneo hilo ambalo linakumbwa matatizo lukuki ikiwemo ukame, njaa na mzozo huko Mali. Prodi ambaye ni Waziri Mkuu wa zamani wa Italia amesema hayo alipozungumza na waandishi wa habari juu [...]
14/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalam wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa majaji na wanasheria, Gabriela Knaul, leo ameelezea wasiwasi wake kuhusu ripoti za vitisho dhidi ya majaji na maafisa wa sheria nchini Sri Lanka, na kuonya kuwa huenda vitisho hivyo vikawa miongoni mwa mashambulizi na ulipizaji kisasi wanaokumbana nayo wanasheria. Bi Knaul amesema vitisho hivyo ni sehemu ya [...]
14/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mizozo, ukame wa mara kwa mara na mfumuko wa bei ya chakula vimezinasa nchi barani Afrika na Mashariki ya Kati katika lindi la njaa, ingawa kuna njia kujinasua kutoka kwa tatizo hili- amesema Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Chakula na Kilimo, FAO, José Graziano da Silva. Bwana da Silva amesema hayo kwenye mkutano wa kimataifa [...]
14/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa Joy Ngozi Ezeilo amezitaka biashara kote duniani kuacha kutumia wafanyikazi wanaosafirishwa kiharamu na pia kuchunguza na kuzuia wafanyikazi kama hao wanaotumia wa washirika wao. Bi Ezeilo amesema kuwa katika ulimwengu wa sasa ulanguzi wa binadamu unapatikana kwenye sekta zote zikiwemo za kiuchumi na unaathiri mataifa yote yakiwemo wanakotoka , [...]
14/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Zaidi ya wanawake milioni 220 hawana uwezo wa kufikia njia za kupanga uzazi wanazojichagulia kwa mujibu wa mfuko wa idadi ya watu wa Umoja wa Mataifa (UNFPA). Shirika hilo linasema kuwa ukosefu au kutopatikana kwa njia za kupanga uzazi vimesababisha wanawake na familia zao kutumbukia kwenye umaskini, kuwa na afya duni na kukabiliwa na ubaguzi [...]
14/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Takribani raia 264 wakiwemo watoto 83 wameuawa na vikundi vya waasi wenye silaha huko Mashariki wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC, kati ya mwezi Aprili na Septemba mwaka huu. Taarifa hizo ni kwa mujibu wa Ofisi ya Tume ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa ambayo iliendesha uchunguzi wake na kubaini kuwa kikundi [...]
14/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon katika ujumbe wake wa siku ya kupambana na ugonjwa wa Kisukari hii leo amesema ugonjwa huo ni changamoto kwa nchi zilizoendelea na zinazoendelea na unazidi kusambaa kila mwaka kutokana na ongezeko la mifumo ya maisha isiyo ya kiafya pamoja na uzee. Amesema familia maskini zenye mgonjwa wa [...]
14/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakati leo ni siku ya kimataifa ya kupambana na ugonjwa wa Kisukari, Shirika la afya duniani linasema kuwa watu Milioni 347 duniani kote wanasumbuliwa na aina ya kwanza ya ugonjwa wa kisukari. WHO imesema mwaka 2004 watu Milioni 3.4 walikufa kutokana na ugonjwa wa kisukari ambapo zaidi ya asilimia 80 ya vifo hivyo ni katika [...]
14/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kumekuwa na hali ya matumaini juu ya mpango wa kukabiliana na wimbi la matumizi ya bidhaa zitokanazo na tumbaku na biashara haramu ya bidhaa za zao hilo ambapo mataifa wanachama wa shirika la afya duniani yanayokutana huko Seoul Korea Kusini yameridhia itifaki ya kupinga biashara hiyo. Dkt. Haik Nikogosian ambaye anaongoza kitengo cha Umoja wa [...]
13/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo limepitisha azimio la kuitaka Marekani kufuta vikwazo vyake ilivyoiwekea Cuba mwaka 1962. Nchi 188 kati ya 193 wanachama wa Baraza hilo leo walipiga kura kuunga mkono azimi hilo huku nchi Tatu ambazo ni Marekani yenyewe, Israel na Palau zikilikataa huku visiwa vya Marshal na shirikisho la Micronesia [...]
13/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, Balozi Augustine Mahiga amesifu hatua ya bunge la Somaliaya ya kukubali na kupitisha baraza jipya la mawaziri la nchi hiyo. Taarifa ya Ofisi ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Somalia, UNPOS, imemkariri Balozi Mahiga akisema kuwa hiyo ni hatua muhimu na inaonyesha utashi wa uongozi wa Somali wa [...]
13/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wizara ya afya nchini Sudan, imelitaarifu shirika la afya duniani, WHO juu ya mlipuko wa ugonjwa wa homa ya manjano kwenye vitongoji 23 vya jimbo la Darfur ambapo hadi Jumamosi iliyopita, kulikuwepo na wagonjwa 329 ikiwemo vifo 97. WHO imesema maeneo ya kati na kusini mwa jimbo hilo la Darfur yameripotiwa kuwa na wagonjwa wengi [...]
13/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa WFP limesema kuwa zaidi ya raia milioni 1.5 wa Haiti wapo hatarini kukubwa na tatizo la ukosefu wa chakula na limetaka kuchukuliwa kwa hatua za haraka kukwamua kadhia hiyo. Shirika hilo limesema kuwa hali iliyojitokeza hivi karibuni ya mabadiliko ya hali ya hewa iliyoenda na ukame [...]
13/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Kuhudumia Watoto katika Umoja wa Mataifa, UNICEF, limesema kuwa athari za kimbunga Sandy kwenye taifa la Haiti zilikuwa juu zaidi ya ilivyotarajiwa. Shirika hilo limesema mwitikio wa dharura wa sekta mbalimbali unahitajika, ili kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa kipindupindu, na kuepukana na janga la njaa na utapia mlo, ambavyo kwa jumla ni hatari [...]
13/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa Chaloka Beyani kesho ataanza ziara ya siku Tisa nchini Sudan kuangalia hali halisi ya raia waliojikuta wakimbizi ndani ya nchi yao. Ziara hiyo ya Beyani ambaye amepewa jukumu na baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa kuchunguza madhila ya watu ambao ni wakimbizi ndani ya nchi zao [...]
13/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchini Afrika kusini, Shirika la Uhamiaji la kimataifa, IOM kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wanaanzisha kampeni iitwayo, Mimi pia ni mhamiaji yenye lengo la kuhamasisha raia wa nchi hiyo wafahamu kuwa wahamiaji nao pia ni sehemu ya jamii yao na hivyo kuleta utangamano miongoni mwa wakazi wote. Kampeni hiyo itaendelea [...]
13/11/2012 | Jamii: Mahojiano | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna Mkuu wa Haki za Binadamu katika Umoja wa Mataifa, Navi Pillay, ameisifu serikali ya Indonesia kwa kuridhia mikataba ya kimataifa ya haki za binadamu haraka, na wakati huohuo kuitaka itekeleze mikataba hiyo nyumbani. Bi Pillay, ambaye amekuwa kwenye ziara rasmi nchini Indonesia tangu Jumapili, amesema kuwa ameridhishwa kwa kuona kuwa harakati za kuzitafsiri [...]
13/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchini Syria matukio mawili ikiwemo shambulio la bomu na utekaji nyara nchini yamesababisha kuharibiwa kwa vifaa vya misaada vilivyokuwa visambazwe kwa raia wa nchi waliokimbia makazi yao kutokana na ghasia. Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR limesema katika tukio la kwanza mablanketi Elfu Kumi na Tatu yaliyokuwa yamehifadhiwa kwenye ghala la shirika [...]
13/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Umoja wa Wataifa UNHCR limeelezea wasi wasi kutokana na mikasa ya hivi majuzi kwenye Ghuba ya Bengal iliyowakumba watu waliokuwa wakikikimbia ghasia nchini Myanmar. Kwa muda wa majuma mawili yaliyopita kumekuwa na ripoti za kuzama kwa mashua mbili kwenye ghuba ya Bengal zikiwa na takriban watu 240 kutoka [...]
13/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la chakula na kilimo la Umoja wa Mataifa, FAO limetoa ripoti mpya inayosema kuwa mipango yoyote ya uwekezaji mkubwa kwenye sekta ya kilimo katika nchi zinazoendelea inapaswa kufanywa kwa umakini bila kuwaengua wakulima wadogo. Ripoti hiyo iliyochapishwa leo inahusu mwelekeo na athari za vitegauchumi vya kigeni vya kilimo kwa nchi zinazoendelea na inasema kuwa [...]
13/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchini Afrika kusini, Shirika la Uhamiaji la kimataifa, IOM kwa kushirikiana na shirika la kimataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR wanaanzisha kampeni iitwayo, Mimi pia ni mhamiaji yenye lengo la kuhamasisha raia wa nchi hiyo wafahamu kuwa wahamiaji nao pia ni sehemu ya jamii yao na hivyo kuleta utangamano miongoni mwa wakazi wote. Kampeni hiyo itaendelea [...]
13/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchi 18 zimechaguliwa kuwa wajumbe wa Baraza la Haki za binadamu la Umoja wa Mataifa kuanzia leo baada ya uchaguzi uliofanywa na Baraza Kuu la Umoja huo na ambapo utekelezaji wa majukumu utaanza rasmi tarehe Mosi Januari mwakani . Baraza hilo lenye wajumbe 47 liliundwa mwaka 2006 kwa lengo la kuimarisha uendelezaji na ulinzi wa [...]
12/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ujumbe wa Shirika la fedha duniani, IMF umehitimisha ziara yake ya wiki mbili nchini Algeria iliyohusisha mashauriano na mijadala kuhusu hali ya uchumi wa nchi hiyo ambapo imebainika kuwa jitihada zaidi zinahitajika ili kuimarisha uchumi wake. Mijadala hiyo ilijikita katika sera za muda mfupi, muda wa kati na za muda mrefu kwa kuzingatia mazingira ya [...]
12/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Naibu Mkuu wa ofisi ya kuratibu misaada ya kibinadamu katika Umoja wa Mataifa, Catherine Bragg, leo amezindua ombi la dola milioni 39, kama marekebisho ya ombi la awali la ufadhili wa misaada ya dharura nchini Haiti, ili kukabiliana na athari za kimbunga Sandy. Fedha hizo zinahitajika ili kukabiliana na matatizo ya uhaba wa chakula, makazi, [...]
12/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »

Naibu Mkuu wa ofisi ya kuratibu misaada ya kibinadamu katika Umoja wa Mataifa, Catherine Bragg, leo amezindua ombi la dola milioni 39, kama marekebisho ya ombi la awali la ufadhili wa misaada ya dharura nchini Haiti, ili kukabiliana na athari za kimbunga Sandy. Fedha hizo zinahitajika ili kukabiliana na matatizo ya uhaba wa chakula, makazi, [...]
12/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ametaka pande zote kwenye mzozo wa milima ya Golan kujizuia kufanya mashambulizi wakati huu ambapo walinzi wa amani wa Umoja huo wanaendelea kusimamia mkataba wa mwaka 1974 wa kusitisha mapigano kati ya Israeli na Palestina. Ametoa wito huo kufuatia taarifa kuwa mapigano kati ya majeshi ya Syria [...]
12/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la linalohusika na nguvu za atomiki Yukiya Amano amekutana na waziri Mkuu wa Iraq Nouri al-Maliki mjini Baghdad wakati wa ziara yake nchini humo ambayo imekusudia kutoa ujumbe wa pongezi kwa serikali ya nchi hiyo iliyoridhia itifaki ya nyongeza. Bwana Amano ameisifu serikali ya Baghdad juu ya hatua [...]
12/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalam maalum wa Umoja wa Mataifa, Anand Grover, ataizuru Japan tokea Novemba 15 hadi 26 ili kufuatilia masuala yanayohusiana na haki ya kuwa na afya nzuri katika nchi hiyo, katika muktadha wa tetemeko la ardhi lililotokea mashariki mwa nchi hiyo mnamo Machi 2011. Katika taarifa, Bwana Grover amesema atazingatia uhusiano kati ya haki ya kuwa [...]
12/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkutano wa tano wa nchi wanachama wa mkataba wa kimataifa wa kudhibiti matumizi ya tumbaku umeanza huko Seoul, Korea Kusini ambapo Mkurugenzi Mkuu wa shirika la afya duniani, WHO Dkt. Margaret Chan amesifu jitihada za nchi hizo za kutekeleza mkataba huo licha ya changamoto zitokazo kwa wafanyabiashara wa tumbaku. Dkt. Chan ametaja changamoto hizo kuwa [...]
12/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, leo linafanya kikao maalum cha kuchagua nchi 18 zitakazokuwa wanachama wapya wa Baraza la haki za Binadamu, ili kuchukuwa nafasi ya zile ambazo muda wao umemalizika. Kulingana na kanuni za Baraza Kuu, Baraza la Haki za Binadamu linatakiwa kuwa na nchi 47 wanachama, ambazo huchaguliwa moja kwa moja kwa [...]
12/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ripoti mpya ya tathmini ya uzalishaji wa chakula huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya watu wa Korea, DPRK iliyoandaliwa baada ya ziara ya maafisa wa Shirika la chakula duniani FAO na lile la mpango wa chakula WFP nchini humo imebaini kuwepo kwa lishe duni miongoni mwa wananchi wa nchi hiyo licha ya ongezeko la mavuno. Imebainika [...]
12/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Afrika na Umoja wa Mataifa Darfur, UNAMID kimeeleza wasiwasi wake kuhusiana na kuendelea kwa mapigano kati ya vikosi vya jeshi la Sudan, SAF na kikundi cha waasi huko Shangil Tobaya na kutaka mapigano hayo yakomeshwe mara moja. Taarifa ya UNAMID imemkariri Kaimu mwakilishi maalum wa pamoja wa [...]
12/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kampeni kabambe kupitia vyombo vya habari imezinduliwa katika Jamhuri ya Afrika ya Kati katika juhudi za kuongeza ufahamu kuhusu ugonjwa wa numonia, ambao unaongoza katika kusababisha vifo vya watoto chini ya miaka mitano. Kampeni hiyo ambayo imezinduliwa leo kwenye Siku ya Numonia Duniani na Shirika la Kuhudumia Watoto katika Umoja wa Mataifa, UNICEF, likishirikiana na [...]
12/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mara kwa mara, watu wengi hujipata wakihitaji kuongezewa damu kwa dharura. Mara nyingi, wengi huwa wamepungukiwa damu mwilini kwa sababu mbali mbali, zikiwemo ajali zinazosababisha uvujaji damu, au hata wakati wanapofanyiwa upasuaji hospitalini. Lakini ili kuongezewa damu mwilini, damu anayoongezewa mtu inapaswa kuwa salama, yaani bila magonjwa ya kuambukiza, yakiwemo magonjwa hatari kama UKIMWI. Lakini [...]
09/11/2012 | Jamii: Makala za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mfumo wa kwanza wa aina yake duniani wa kufuatialia baadhi ya magonjwa yasiyo ya kuambukiza ambayo yanayoongoza duniani kwa vifo umeridhiwa huko Geneva, Uswisi na nchi wanachama wa shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO. Mwenyekiti wa mkutano huo Dkt. Bjørn-Inge Larsen amesema mfumo huo umeweka malengo Tisa na viashiria 25 vya kuzuia na [...]
09/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ametoa wito kwa watu wote duniani kushiriki kampeni ya kumuunga mkono mtoto wa kike wa kipakistani Malala Yousfzai aliyejeruhiwa kwa kupigwa risasi mwezi uliopita na watalibani kutokana na utetezi wake kwa elimu. Katika ujumbe wake, Bwana Ban amesema tarehe 10 mwezi huu ambayo ni siku ya kampeni [...]
09/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalam maalum wa Umoja wa Mataifa, Pablo de Greiff, ataizuru Tunisia tokea kesho Novemba 10 hadi 16, ili kufuatilia hatua zilizochukuliwa na serikali kuhusu ukiukaji wa haki za binadamu zamani na kuendeleza mfumo wa haki baada ya mabadiliko. Ziara hiyo ndiyo ya kwanza kufanywa na mtaalam huru ambaye ameteuliwa na Baraza la Haki za Binadam [...]
09/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika kuelekea kuadhimisha siku ya numonia duniani tarehe 12 mwezi huu, Shirika la afya WHO limesema kwa sasa kuna chanjo ya numonia inayosababishwa na bakteria pekee wakati asilimia 30 ya visa vya numonia duniani ni mchanganyiko wa maambukizi ya bakteria na virusi. Tarik Jasarevic ambaye ni msemaji wa WHO ameeleza kuwa kutokana na hali hiyo [...]
09/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amelihutubia Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuhusu madhara ya kimbunga Sandy kilichokumba maeneo ya Caribbean na pwani ya Mashariki ya Marekani mwishoni mwa mwezi uliopita na kusema kuwa mataifa yatumie kimbunga hicho kuwa fursa ya kuangalia upya mambo yanayochangia mabadiliko ya tabia nchi. Pamoja na kuelezea [...]
09/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »

Kisiwa cha Papua New Guinea kinatazamia kuboresha vitengo vyake vinavyohusika na uhamiaji pamoja na ustawi wa kiraia kufuatiwa kuzinduliwa kwa mpango mpya wa kitaalamu unaoratibiwa na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na uhamiaji IOM. Kuzinduliwa kwa mpango huo kunafuatia mkutano uliofanyika juma hili ukiwakutanisha wataalamu wa ngazi za juu kutoka pande zote waliokutana katika [...]
09/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ripoti ya Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na uhamianji IOM limefichua kile ilichokieleza kukithiri kwa vitendo korofi vilivyowaandama raia wa Sri Lank walioenda nchi za nje kwa ajili ya kusaka kazi. Ripoti hiyo imesema kuwa kiasi kikubwa cha raia hao sasa wamepatwa na magonjw ambalimbali na wengine kupoteza maisha kwa kujinyonga na kufariki kwa [...]
09/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mashirika ya Umoja wa Mataifa yamesema mafuriko nchini Nigeria yameathiri zaidi ya watu milioni 7.7. Mafuriko hayo ambayo yameelezewa kuwa mabaya zaidi katika kipindi cha miaka 40, yamesemekana kuwaua zaidi ya watu mia tatu, huku wengine zaidi ya milioni mbili wakiwa wamejiandikisha kama wakimbizi wa ndani. Shirika la Afya Duniani, WHO limesema visa vya maambukizi [...]
09/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika hatua nyingine mkuu wa shirika la mpango wa chakula duniani, WFP Ertharin Cousin amehitimisha ziara yake ya siku tatu huko Mashariki ya Kati iliyompeleka hadi nchi za Lebanon na Jordan kujionea hali halisi ya wakimbizi wa Syria waliokimbia nchi yao kutokana na mapigano yanayoendelea. Pamoja na kuzungumza na viongozi, alikutana pia na wakimbizi mathalani [...]
09/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Hali ya kibinadamu imezidi kuzorota huku machafuko nchini Syria yakiwa yameongezeka, kwa mujibu wa mratibu wa huduma za kibinadamu wa Umoja wa Mataifa katika kanda ya Mashariki ya Kati, Radhouane Nouicer, wakati wa kongamano la kibinadamu kuhusu Syria, ambalo linaendelea mjini Geneva, Uswisi. Afisa huyo wa Umoja wa mataifa amewaambia waandishi wa habari kwamba mahitaji [...]
09/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkutano wa aina yake uliofanyika wiki hii kwenye mji mkuu wa Ethiopia Addis Ababa umeimarisha jitihada za kuendeleza hatua za lishe bora kwa watoto kwa mujibu wa mkakati wa kuondoa njaa kwa watoto uitwao REACH. Wataalamu na maafisa wa mashirika ya Umoja wa Mataifa kutoka nchi 12 zinazotekeleza mpango huo wa REACH, pamoja na Ethiopia [...]
09/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataiafa, UNHCR, limesema kuwa uwezo wa kudhibiti kusambaa kwa ugonjwa wa Hepatitis E nchini Sudan Kusini ni mdogo kwa sababu ya ufadhili mdogo. Shirika hilo limeonya kuwa hatari ya maambukizi zaidi itaongezeka ikiwa idadi ya wakimbizi wanaowasili kutoka majimbo ya Kordofan Kusini na Blue Nile katika nchi jirani [...]
09/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Kimataifa la uhamiaji kwa kushirikiana na serikali ya Tanzania wiki ijayo wataandaa mkutano wa mashauriano kuhusu athari za uhamiaji zitokanazo na itifaki ya soko la pamoja la nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki, EAC. Mkutano huo wa siku tatu utakaoanza jijini DSM tarehe 13 utajumuisha maafisa wa IOM, na wale wa kutoka wizara [...]
09/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amesema umoja huo uko tayari kusaidi jitihada zinazofanywa na serikali ya Guatemala ya kutoa misaada ya kibinadamu kufuatia tetemeko la ardhi lililokumba nchi hiyo jana na kusababisha vifo vya watu 48 na wengine 150 kujeruhiwa. Akizungumza na waandishi wa habari mjini New York, msemaji wa Umoja wa [...]
08/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeshindwa kuridhia maazimio thabiti kuhuusu Syria, kwa mujibu wa katiba ya Umoja huo inayolipa baraza mamlaka ya kusimamia amani na utulivu duniani. Balozi wa Colombia katika Umoja wa Mataifa Néstor Osorio ametoa kauli hiyo wakati akitambulisha rasimu ya ripoti ya mwaka ya Baraza la Usalama itakayowasilishwa kwenye Baraza [...]
08/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Serikali ya Libya pamoja na wananchi wake katika kipindi cha mwaka mmoja uliopita wamepiga hatua kubwa kurejesha utulivu nchini humo licha ya changamoto zilizopo. Hiyo ni kauli ya Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa nchiniLibya, Tarek Mitri aliyoitoa kwa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa hii leo wakati alipolihutubia kuhusu hali ilivyo nchini Libya [...]
08/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada ya kibinadamu, OCHA limesema hali ya kibinadamu nchini Mali si nzuri na kwamba watu Milioni Nne nukta Sita nchini humo bado hawana uhakika wa chakula. Msemaji wa Umoja wa Mataifa, Martin Nesirky amewaambia waandishi wa habari mjini New York, Marekani kuwa uwezo wa wakazi wa kaskazini mwa [...]
08/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO linaendesha mafunzo ya siku tano kwa waandaji wa vipindi vya radio wa nchi za Afrika Mashariki kwa ajili ya kuongeza ubora wa vipindi vya elimu kuhusu kinga dhidi ya Ukimwi na kuimarisha ushirikiano baina ya Radio katika Jumuiya ya Afrika Mashariki. Katika mafunzo hayo [...]
08/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Afya Duniani, WHO, limetoa zaidi ya tembe milioni tano za kuuwa minyoo inayosababisha ugonjwa wa kichocho kwa serikali ya Nigeria, ili kusaidia kuzuia maambukizi ya ugonjwa huo unaoainishwa miongoni mwa magonjwa ya kitropikali yalosahaulika. Idadi ya watu watakaolindwa kutokana na ugonjwa huo inakadiriwa kuwa milioni tatu. Ugonjwa wa kichocho huzuia ukuaji wa [...]
08/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada na ulinzi wa wakimbizi wa kipalestina, UNRWA Fillipo Grandi ametaka suluhisho la haki kwa zaidi ya wakimbizi Milioni Tano wa kipalestina. Akiwasilisha ripoti yake mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani, Grandi ameelezea pia wasiwasi wake mkubwa kwa hali [...]
08/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Uhuru wa kuwa na usemi kupitia kwa njia ya Intaneti umepata uungwaji mkono wa dhati katika kongamano la Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO kuhusu udhibiti wa mfumo wa Intaneti mjini Baku, Azerbaijan. Akizungumza katika kongamano hilo, Mkurugenzi wa kitengo cha uhuru wa kuwa na usemi na maendeleo ya vyombo vya habari, Guy Berger, [...]
08/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada na ulinzi kwa wakimbizi wa kipalestina, UNRWA imezieleza mamlaka ya Syria juu ya hofu yake kuu kwa madhara wanayopata wakimbizi wa kipalestina kutokana na mgogoro unaoendelea nchini humo. Hofu hiyo inafuatia mauaji ya Jumatatu ya Dkt. Rehab Awadallah, mwalimu wa UNRWA nchini Syria pamoja na mpwa wake [...]
08/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna Mkuu wa Tume ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, Navi Pillay amesifu kongamano la Bali kama fursa muhimu ya kuendeleza utawala bora, utawala wa kisheria na haki za binadamu miongoni mwa nchi wanachama wa Umoja wa nchi za Kusini- Mashariki mwa Asia, ASEAN huku akitaka viongozi wa nchi hizo kuweka muda [...]
08/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Bei ya chakula ilishuka kwa asilimia moja ya kipimo wastani cha Shirika la Chakula na Kilimo, FAO mnamo mwezi Oktoba mwaka huu. Aidha katika kipindi cha miezi kumi ya kwanza mwaka huu, bei ya chakula ilikuwa asilimia 8 wastani, na hivyo kuwa chini ya ilivyokuwa katika kipindi sawa na hicho mwaka 2011. Bei ya kapu [...]
08/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kaimu Mkuu wa ujumbe wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika huko Darfur, UNAMID, Aichatou Mindaoudou ametaka serikali ya Sudan kuharakisha mchakato wa uchunguzi wa ghasia zinazoripotiwa kutokea kijiji cha Sigili. Ametoa agizo hilo kufuatia ripoti za hivi karibuni zinazodai kuwepo kwa shambulio dhidi ya raia siku ya Ijumaa kwenye kijiji cha [...]
08/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwendesha Mashtaka mkuu wa mahakama ya kimataifa ya uhalifu, ICC, Fatou Bensouda ameitaka jumuiya ya kimataifa kusaidia Libya kuondoka na vitendo vya kukwepa kuchukua mkono wa sheria na badala yake kusimamia utawala wa kisheria. Bi.Bensouda amesema hayo leo mbele ya Baraza Kuu la Usalama la Umoja wa Mataifa wakati akiwasilisha ripoti yake ambapo ameeleza kuwa [...]
07/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mtendaji wa shirika la mpango wa chakula duniani, WFP Ertharin Cousin, amehitimisha ziara yake nchini Lebanon na kuipongeza serikali ya nchi hiyo na wananchi wake kwa kuwasaidia wakimbizi kutoka Syria wanaotafuta hifadhi salama. Bi. Cousin ambaye amewaeleza waandishi wa habari mjini Beirut kuwa kitendo hicho cha serikali ya Lebanon kinarahisisha kazi ya WFP ya [...]
07/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Miaka mitatu tangu kumalizika kwa vita vya wenyewe kwa wenyewe nchini Sri Lanka, changamoto mpya zimeibuka wakati watu wakiendelea kurejea nyumbani. Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Wakimbizi, UNHCR, limekuwa likishirikiana na viongozi wa kitaifa na wadau wengine ili kusaidia kuhakikisha wakimbizi hao wanarejea kwa njia endelevu kwa kuzishughulikia baadhi ya changamoto hizo, zikiwemo [...]
07/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na wakimbizi UNHCR limepongeza serikali ya Philippines kwa kuwa nchi ya kwanza katika eneo la Asia-Pasifik kuanzisha mpango wenye shabaha ya kuwalinda wakimbizi na jamii ya watu wasiokuwa na ukazi maalumu. Idara ya haki na sheria ya Philipenes hivi karibuni ilichapisha mwongozo ambao pamoja na mambo mengine umekusudia kuboresha [...]
07/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeongeza kwa miezi minne zaidi muda wa kuwepo nchini Somalia kwa vikosi vya kimataifa vya kulinda amani nchini humo, AMISOM. Uamuzi huo umeazimiwa leo wakati wa kikao cha baraza hilo mjini New York Marekani ambapo muda wa awali wa wiki moja ulioongezwa wiki iliyopita ulikuwa unamalizika leo. Rais [...]
07/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Sera za kibiashara huathiri kwa njia tofauti sehemu mbali mbali za jamii, kama vile wanaume na wanawake, wakaazi wa vijijini na mijini, watu tajiri na maskini. Hayo ni kwa mujibu wa utafiti uliofanywa na Kamati ya Umoja wa Mataifa kuhusu Biashara na Maendeleo, UNCTAD, wa hali katika nchi za Cape Verde, the Gambia na Lesotho. [...]
07/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni UNESCO, Irina Bokova na Rais Asif Al Zardani wa Pakistani watakuwa wenyeji wa tukio mkutano maalum wa ngazi ya juu wa kutetea haki ya elimu kwa mtoto wa kike. UNESCO imesema mkutano huo ukiwa na maudhui, Mtetee Malala, tetea hali mtoto wa [...]
07/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kenya inafaa kuidakia fursa maalum ilotolewa na katiba yake mpya, pamoja na maoni ya umma ili kukomesha uharibifu wa misitu katika maeneo yake ya maji, ambao husababisha hasara ya dola milioni sabini kila mwaka kwa uchumi wake, na kuweka hatarini asilimia sabini ya vianzo vya maji nchini humo. Hayo ni kwa mujibu wa wajumbe waliohudhuria [...]
07/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la afya duniani, WHO limesema idadi ya watu waliokufa kutokana na ugonjwa homa ya manjano kwenye jimbo la Darfur, huko Sudan imefikia 67 huku idadi ya wagonjwa ikiongezeka maradufu kutoka 84 wakati ugonjwa huo uliporipotiwa hadi 194. Kwa mara ya kwanza ugonjwa huo unaoenezwa na mbu, uliripotiwa mwezi Oktoba na umeshaenea katika vitongoji 17 [...]
07/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon amemtumia salamu za pongezi kwa Rais Barack Obama wa Marekani kwa kuchaguliwa tena kuongoza nchi hiyo kwa kipindi cha miaka minne na kusema ni matarajio yake kuendelea kufanya kazi na Rais Obama na serikali yake kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kati ya Marekani na Umoja wa Mataifa. [...]
07/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mafuriko yaliyokumba Nigeria kutokana na mvua zilizonyesha kati ya mwezi Julai na Oktoba mwaka huu yameanza kupungua wakati huu ambapo mamlaka ya hali ya hewa nchini huumo imetangaza kuwepo kwa mvua zaidi mwezi ujao zenye uwezekano mdogo wa kuleta madhara. Ripoti ya awali ya hali halisi ya mafuriko nchini Nigeria iliyotolewa na shirika la Umoja [...]
07/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la mpango wa chakula la Umoja wa Mataifa, WFP limeanza kusambaza chakula kwa zaidi ya wakazi Elfu 27 wa vitongoji vilivyokumbwa na mgogoro wa kikabila kwenye jimbo la Rakhine nchini Myanmar mwezi uliopita. Msemaji wa WFP Elisabeth Byrs amewaeleza waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi kuwa idadi hiyo ya wat wanaopatiwa msaada ambao [...]
06/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Takriban tani bilioni 1.3 za taka huzalishwa mijini kila mwaka, na kiwango hiki kinatarajiwa kuongezeka hadi tani bilioni 2.2 ifikapo mwaka 2025, kwa mujibu wa takwimu za Benki ya Dunia. Kwa sababu hii, hatua za haraka zinahitajika ili kukabiliana na athari za tatizo hili kwa maisha ya mwanadamu, limesema Shirika la Mpango wa Mazingira la [...]
06/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Uhuru wa kujieleza unaweza kuchangia kuwepo kwa mazingira bora ya kuwepo kwa mazungumzo ya kukosoana hasa katika masuala ya kidini amesema mtalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu uhuru wa kujieleza Frank La Rue. Kupitia kwa ripoti yake kwa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjumbe huyo amezungumzia masuala ya lugha inayozua chuki na hatua za [...]
06/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la chakula na kilimo duniani, FAO na serikali ya HAITI zinahitaji zaidi ya dola Milioni 74 katika kipindi cha miezi 12 ijayo kwa ajili ya kurekebisha sekta ya kilimo nchini humo iliyoharibiwa na kimbunga Sandy. Kimbunga hicho kilichopiga mwishoni mwa mwezi uliopita kimeharibu miundombinu maeneo ya vijijini pamoja na mazao, ardhi, mifugo, mashamba ya [...]
06/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkutano wa Shirika la Afya Duniani kuhusu mkataba wa kudhibiti bidhaa za tumbaku unatazamiwa kufanyika mjini Seoul, Korea Kusini wiki ijayo, ukiwa ni mkutano wa tano wa mataifa wanachama wa mkataba huo. Mkutano huo wa wanachama unatazamiwa kurejelea, kufanyia marekebisho na kuendeleza utekelezaji wa mkataba huo. Inatarajiwa kuwa mwishoni mwa mkutano huo, mkakati wa kwanza [...]
06/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la mpango wa chakula duniani, WFP limesema linahitaji dola Milioni 20 kwa ajili ya msaada wa chakula kwa watu Laki Mbili na Elfu Ishirini na Tano nchini Haiti wanaokabiliwa na matatizo kutokana na kimbunga Sandy kilichokumba nchi hiyo. Msemaji wa WFP Elizabeth Byrs amesema hivi sasa watu hao wamepoteza makazi yao, mazao na kwamba [...]
06/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM limezindua makao makuu mapya ya idara ya uhamiaji katika mji mkuu wa Somaliland Hargeisa. Mradi huu unatarajiwa kuwezesha idara ya uhamiaji eneo la Somaliland kutoa usimamizi wa mipaka unaohitajika. Uzinduzi wa makao hayo ulihudhuriwa na maafisa wa ngazi za juu serikalini wakiongozwa na rais wa Somaliland Ahmed Mohamed Mohamoud [...]
06/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa kwa kushirikiana na serikali za Sudan na Sudan Kusini zimeanza kusafirisha raia Elfu Moja Mia Tatu Sabini wa Sudan Kusini kutoka mji mkuu wa Sudan, Kharthoum kwenda mji wa Aweil ulioko jimbo la Bahr El Ghazal, Sudan Kusini. Raia hao pamoja na familia zao ni wale walioko katika mazingira magumu zaidi na [...]
06/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon ametaka hatua zaidi zichukuliwe kuepusha migogoro katika nchi inayochochewa na kuwepo kwa maliasili na badala yake utajiri huo utumike vyema kujenga amani. Bwana Ban amesema hayo leo ikiwa ni siku ya kimataifa ya kuepusha mizozo itokanayo na matumizi mabaya ya maliasili ambapo ameongeza kuwa laana ya kumiliki [...]
06/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe maalum wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa nchi za kiarabu, Lakhdar Brahimi amesema Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa libadilishe kuwa azimio, makubaliano ya mwezi Juni kuhusu hatua za kuweka kipindi cha mpito nchini Syria kwa lengo la kusaidia kumaliza mzozo unaoendelea nchini humo. Brahimi amesema hayo leo huko Cairo, [...]
05/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa leo limeelezwa kuwa nishati ya nyuklia bado ni mbadala muhimu wa kukidhi mahitaji ya nishati duniani licha ya ajali iliyokumba mtambo wa nyuklia wa Fukushima Daiichi nchini Japan mwaka jana. Afisa wa India kwenye Ubalozi wa nchi hiyo katika Umoja wa Mataifa Annu Tandon ametoa kauli hiyo wakati baraza [...]
05/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi wa Operesheni wa shirika la kuratibu masuala ya kibinadamu la Umoja wa Mataifa, OCHA. John Ging amezungumza na waandishi wa habari mjini New York, Marekani na kusema kuwa hali ya kibinadamu huko Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC ni mbaya wakati huu ambapo zaidi ya watu Milioni Mbili wamekimbia makazi yao ndani ya nchi [...]
05/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa Sudan Kusini, Hilde Johnson, amesema hatua ya serikali ya Sudan Kusini kumfukuza afisa wa haki za binadamu wa Umoja wa Mataifa ni kinyume na wajibu wa serikali hiyo chini ya mkataba wa Umoja wa Mataifa. Wizara ya Mambo ya Nje ya Sudan Kusini iliiandikia afisi ya ujumbe wa Umoja wa [...]
05/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mataifa 39 ya Asia-Pasifiki yameridhia kuanzisha muundo wenye lengo la kujenga jamii inayojumuisha watu wenye ulemavu kwenye ukanda huo wenye walemavu zaidi ya Milioni 650. Makubaliano hayo yanayoitwa mkakati wa muongo mmoja wa Incheon yamefikiwa mwishoni mwa mkutano wa aina yake wa masuala ya Umoja wa mataifa kwenye ukanda huo huko Korea Kusini ambapo ulitathmini [...]
05/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa umesema kuwa yapata watu milioni 1.6 nchini Haiti wameathirika vibaya sana na kimbunga Sandy, ambacho kilipita pwani ya mashariki mwa Marekani na maeneo ya Karibi wiki moja iliyopita. Serikali ya Haiti imetoa wito kwa Umoja wa Mataifa, mashirika ya kimataifa na wafadhili kutoa misaada ya dharura ili kuwasaidia manusura na waathirika wa [...]
05/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkutano wa siku Tatu wa kuhitimisha kilele cha maadhimisho yaa miaka 40 ya mkataba wa kimataifa wa urithi wa dunia utafanyika mjini Kyoto Japan kuanzia kesho ambapo pamoja na mambo mengine utajumuisha mijadala kuhusu utekelezaji wa mkataba huo. Tukio hilo linatarajiwa kushuhudia kuingizwa kwa eneo la 1000 la urithi wa dunia kwa mujibu wa mkataba [...]
05/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Watalaamu kuhusu nishati asilia wamesema kuna umuhimu wa kuwa na mfumo mmoja na wa uwazi zaidi wa kutathmini na kufahamu idadi ya vyanzo asilia vya nishati kwa uwazi wakati huu ambapo sekta hiyo na nishati asilia inakuwa ya kibiashara zaidi. Jopo la wataalamu hao lilikuwa na mkutano huko London, Uingereza kwa siku tatu kuanzia tarehe [...]
05/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kenya ilipoteza jumla ya shilingi bilioni 5.8 au dola milioni 68 mwaka 2010 na shilingi bilioni 6.6 mwaka 2009 kutokana na ukataji wa miti kwa mujibu wa ripoti ya pamoja ya shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa UNEP na idara ya misitu nnchini Kenya KFS. Utafiti unoaendeshwa na na idara ya misitu nchini Kenya [...]
05/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Idadi ya watu waliolazimika kuhama makwao kutokana na ghasia za kisiasa kwenye mkoa wa Rakhine nchini Myanmar imefikia watu 110,000 kwa mujibu wa shirika la kuratibu masuala ya kibinadamu la Umoja wa Mataifa OCHA. Takriban watu 89 wameuawa tangu kuanza kwa kwa mzozo mwezi Oktoba huku zaidi ya nyumba 5,300 na maeneo ya kuabudu vikiharibiwa. [...]
05/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeongeza kwa siku saba zaidi muda wa kuwepo kwa vikosi vya kimataifa vinavyolinda amani nchiniSomalia. Muda wa vikosi hivyo ulikuwa umalizike tarehe 31 mwezi uliopita. Taarifa iliyotolewa imesema kuwa azimio la Barazahilolililopitishwa kwa kauli moja mjiniNew York, Marekani baada ya kikao chake, limeongezwa muda huo kwa kuzingatia mazingira [...]
02/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa anayehusika na utetezi wa haki za binadamu na uhuru wa kujieleza wakati wa harakati zozote za kupinga ugaidi, Ben Emmerson amelitaka Baraza la Usalama la Umoja huo kuhakikisha vikwazo vyake dhidi ya kikundi cha kigaidi cha Al Qaeda vinazingatia haki za binadamu. Emmerson amesema hayo leo mbele ya Baraza [...]
02/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Jopo la majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Kivita, ICC, limeamua leo Novemba 2 kuwa aliyekuwa rais wa Ivory Coast, Laurent Gbagbo yu bukheri wa afya na hivyo anaweza kusimama mashtaka mbele ya mahakama hiyo. Majaji hao wataweka tarehe karibuni ya kusikiliza kuthibitishwa kwa mashtaka katika kesi dhidi ya Bwana Gbagbo. Kwa mujibu wa uamuzi [...]
02/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na uhamiaji IOM, limeshindwa kuendesha juhudi za kuwakwamia mamia ya raia wa Pakistan waliokumbwa na mafuriko kutokana na kukabiliwa na uhaba wa fedha. Takwimu kutoka serikali zinasema kuwa kiasi cha watu milioni 3.4 wameathiriwa na mafuriko huku wengine zaidi ya 386,000 hawana makazi maalumu kutokana na nyumba zao kubomolewa [...]
02/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »

Umoja wa Mataifa umesema idadi kubwa ya watoto wachanga nchini Syria wanafariki dunia kutokana na uhaba wa mashine za kuwawezesha kupumua pindi wanapozaliwa kabla ya wakati. Shirika la Umoja wa mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limesema jopo la wataalamu wake lilitembelea jimbo la Al Raqqah nchini Syria ambapo hospitali kuu ya eneo hilo ina mashine [...]
02/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limesema wafanyakazi wake wameweza kufika katika vijiji vilivyokumbwa na mapigano kwenye jimbo la Rakhine, magharibi mwa Myanmar ambako serikali ya nchi hiyo imesema watu 35, 000 wamepoteza makazi kutokana na vurugu hizo za hivi karibuni. Msemaji wa UNHCR Adrian Edwards, amesema ziara ya wafanyakazi hao inafuatia [...]
02/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kuendelea kuwepo kwa misukosuko kwenye mkoa wa Kivu Kaskazini kwenye Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kumechangia kuongozeka kwa idadi ya watu wanaohama makwao nayo mahitaji ya chakula yakizidi kupanda. Zaidi ya watu 260,000 wamalazimika kuhama makwao kwenye mkoa wa Kivu kaskazini tangu kuanza kwa mzozo mwezi Aprili mwaka huu. Juma hili shirika la mpango wa [...]
02/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Takwimu kutoka nchini Mali zinaonyesha kuwa kuna idadi ya juu ya wakimbizi wa ndani nchini kuliko ilivyoripotiwa awali.Kulingana na tume unayohusika na kuhama kwa watu nchini Mali nchini ya uongozi wa shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR ni kwamba watu 203,845 wamelazimika kuhama makwao. Pia kumekuwa na dalili za watu kuhama ambapo [...]
02/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kuratibu masuala ya kibinadamu la Umoja wa Mataifa OCHA linasema kuwa kimbunga Sandy kinaripotiwa kuwaua watu 60 nchini Haiti na kuwaathiri wengine milioni 1.8 ambapo pia nyumba 18,000 ziliharibiwa. Kwa upande wake shirika la afya duniani WHO linasema kuwa hali mbaya ya usafi nchini Haiti huenda ikachangia kuwepo kwa magonjwa ya kuambukiza ukiwemo [...]
02/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mauaji ya wanajeshi wa serikali ya Syria kwa kufyatuliwa risasi na vikosi vya upinzani, na ambayo yalinaswa kwenye video, huenda yakaainishwa kama uhalifu wa vita, kwa mujibu wa afisi ya Kamishna Mkuu wa Haki za Binadam katika Umoja wa Mataifa. Afisi hiyo ya haki za binadam imetoa wito kwa pande zote katika mzozo wa Syria [...]
02/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Zaidi ya watu Bilioni 2.2 katika nchi za Asia-Pasifiki wako hatarini kukumbwa na ugonjwa wa Malaria, ugonjwa ambao kwa kiasi kikubwa umekuwa ukitajwa kuwa tishio barani Afrika pekee. Taarifa hizo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya mpango wa ushirikiano wa kimataifa wa kudhibiti Malaria, RBM ambayo imesema nchi za India, Myanmar, Papua New Guinea [...]
02/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuratibu misaada kwa ajili ya wakimbizi wa kipalestina, UNRWA limeendelea kuonyesha wasiwasi wake juu ya madhara ya mgogoro wa Syria kwa wakimbizi wa kipalestina na raia wa nchi zingine na hivyo kutaka pande zote katika mgogoro huo kujizuia kufanya mashambulizi ya kiholela kwa mujibu wa sheria za kimataifa. Wito [...]
02/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Watalamu wa kimatibabu wanasema magonjwa ya akili ni moja wapo wa maradhi yanayopuuzwa sana, hasa katika nchi zinazoendelea. Asilimia sabini na tano ya watu wanaokumbwa na magonjwa ya akili wanaishi katika nchi zinazoendelea na wengi wao hawapati matibabu. Mara nyingi, usumbufu wa akili huwapunguzia watu uwezo wa kukabiliana na changamoto za maisha za kila siku, [...]
02/11/2012 | Jamii: Makala za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoratibu misaada ya kibinadamu, OCHA imesema kadri mzozo unavyozidi kuimarika nchini Syria, hali ya kibinadamu inazidi kudorora wakati huu ambapo idadi ya wanaohitaji misaada ya kibinadamu nchini humo ikiongezeka na kufikia watu Milioni Mbili na Nusu. Jarida la hali ya kibinadamu linalotolewa na OCHA limesema misaada ya kibinadamu wakati wa [...]
02/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa umeitaka China kushughulikia haraka iwezekanavyo vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu vinavyochochea maandamano na vurugu huko Tibet ikiwemo watu kujiua kwa kujichoma moto. Mkuu wa Tume ya Haki za Binadamu ya Umoja wa Mataifa Navi Pillay amesema tangu mwaka 2011 kumekuwepo na matukio zaidi ya 60 ya watu kujiua kwa kujichoma [...]
02/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchini Libya, Tarek Mitri amempongeza Waziri Mkuu wa Libya Ali Zeidan na baraza lake la mawaziri kufuatia kuundwa kwa serikali mpya nchini humo. Mitri, katika taarifa iliyotolewa na ujumbe wa Umoja wa Mataifa wa kusaidia Libya, UNSMIL amelipongeza pia bunge la Libya kwa kuidhinisha serikali hiyo na [...]
01/11/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu, OCHA nchiniHaiti, Johan Peleman amesema wanasubiri ripoti ya majumuisho ya tathmini ya madhara yaliyotokana na kimbungaSandykilichopiga nchi hiyo wiki iliyopita ili waweze kufahamu msaada unaohitajika na idadi kamili ya watu walioathiriwa wakati huu ambapo inakadiriwa watu Elfu Ishirini hawana makazi. Peleman ameiambia Radio [...]
01/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalamu mpya wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu nchiniBelarus, Miklós Haraszti ametaka kufanyika kwa mjadala wa wazi kati yake na serikali ya nchi hiyo pamoja na vyama vya kijamii wenye lengo la kuendeleza na kulinda haki za binadamu nchini humo. Haraszti amesema hayo leo ikiwa ni siku anayoanza rasmi jukumu hilo alilokabidhiwa na [...]
01/11/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Jopo la wataalam huru wa Umoja wa Mataifa limetoa wito kwa serikali ya Iran iwaachilie huru mara moja wakili maarufu wa kutetea haki za binadamu, Nasrin Sotoudeh na Jafar Panahi, ambaye ni mtengenezaji filamu mwenye umaarufu wa kimataifa. Wawili hao walipewa tuzo ya uhuru wa dhana ya Sakharov hivi karibuni na bunge la Jumuiya ya [...]
01/11/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limesema wakati wa sikukuu ya Eid El Adha lilifanikiwa kwa kiasi fulani kuwasilisha misaada ya kibinadamu kwa baadhi ya maelfu ya familia nchini Syria ambazo awali zilikuwa haziwezi kupatiwa misaada hiyo. Msemaji wa UNHCR Ron Redmond amesema ghasia ziliendelea kwa kuwa makubaliano ya kusitisha mapigano hayakuzingatiwa [...]
01/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la Haki za Binadamu la Umoja wa Mataifa limemtuma mtaalamu huru kuhusu masuala ya usafirishaji haramu wa binadamu kwenda nchini Ufilipino kuchunguza hali halisi usafirishaji haramu wa binadamu nchini humo na athari za mikakati ya kupambana na vitendo hivyo. Mtaalamu huyo Joy Ngozi Ezielo ataanza ziara hiyo tarehe Tano mwezi huu hadi tarehe Tisa [...]
01/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO, Irina Bokova, ameelezea kusikitishwa kwake kuhusu usalama wa waandishi habari nchini Somalia, na kutaka uchunguzi ufanywe kufuatia mauaji ya Mohammed Mohamud Tuuryare na Ahmed Farah Ilyas mnamo Oktoba 28 na Oktoba 23 mfululizo. Bi Bokova amelaani mauaji hayo, na kusema kuwa idadi ya waandishi habari [...]
01/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la afya duniani, WHO limesema ugonjwa wa homa ya Marburg umeendelea kusambaa nchini Uganda ambapo hadi sasa watu Kumi na Mmoja wamefariki dunia kutokana na ugonjwa huo. Wagonjwa 20 wameripotiwa katika wilaya Tano nchini humo ikiwemo kwenye mji mkuu Kampala. Homa ya Marburg iliripotiwa kulipuka katika wilaya ya Kabale Kusini Magharibi mwa Uganda tarehe [...]
01/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ugonjwa wa kupooza, yaani polio, hautatokomezwa nchini Pakistan pasi mpango wa kitaifa kuwafikia wazazi kutoka makundi ya jamii ambayo yamo hatarini zaidi, kama vile jamii za kipato cha chini za Pashtun, ambazo huathiriwa zaidi na ugonjwa huo. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya utafiti iliyochapishwa kwenye taarifa ya habari ya Shirika la Afya Duniani, [...]
01/11/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »