UNRWA yazindua programu mpya ya elimu
Kusikiliza /Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA limezinfdua programu mbili mpya kwenye kituo chake cha elimu ya sayansi eneo la Naour magharibi mwa Amman kama sehemu ya mikakakati yake ya kuyafanyia mabadiliko masuala ya elimu. Kwenye taarifa iliyotolewa hii leo UNRWA imesema kuwa programu hizo mbili zilizozinduliwa wakati wa maadhimisho ya siku ya waalimu duniani ni maendeleo ya uongozi kwa walimu wakuu siku zijazo.
Mkurugenzi mkuu wa UNRWA Caroline Pontefract amesema shirika hilo linapanga kuboresha elimu akiongeza kuwa mikakati yote imetambuliwa na kupangwa. UNRWA inapanga mbinu za kutumia walimu na walimu wakuu ambao ndio msingi wa kuwepo elimu bora.
