UNESCO kupokea msaada wa dola milioni 20 kutoka Norway
Kusikiliza /Taifa la Norway limetangaza kuwa litatoa jumla ya dola milioni 20 kufadhili miradi ya shirika la elimu , Sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO ikiwa ni sehemu ya kuzipa kipaumbele programu za elimu na masuala ya kitamaduni na uhuru wa kujieleza.
Makubaliano ya ushirikiano huo yatatiwa sahihi na Waziri wa maendeleo ya kitaifa wa Norway Arvinn Eikeland Gadgil na mkuu wa shirika la UNESCO Irina Bokova kwenye makao makuu wa shirika hilo mjini Paris nchini Ufaransa. Baada ya kusainiwa kwa makubalino taifa siku ya Alhamisi Norway itaandaa mjadala kuhusu masuala ya wanawake wenye kauli mbiu 'Nora's Sisters, Women Worlwide: Challenges of Freedom.
