Benki ya Dunia yasema uchumi wa Afrika unaimarika
Kusikiliza /Ripoti ya Benki ya dunia iliyotolewa hivi karibuni imebashiri kukua kwa uchumi wa nchi za Afrika zilizo kusini mwa jangwa la Sahara kwa asilimia 4.8 mwaka huu wa 2012 licha ya kudorora kwa uchumi wa dunia.
Ripoti hiyo itolewayo mara mbili kwa mwaka baada ya kuchunguza masuala yanayotoa mwenendo wa uchumi wa Afrika imesema kiwango hicho hakijatofautiana sana na kile cha mwaka uliotangulia cha asilimia 4.9 na hivyo kuonyesha kuwa Afrika iko katika mwelekeo sahihi. Taarifa zaidi na Alice Kariuki.
(SAUTI YA ALICE KARIUKI)
