Nyumbani » 31/10/2012
Entries posted on “Oktoba, 2012”

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, amesema anafuatilia kwa karibu hatma ya kimbunga cha Sandy, ambacho kimesababisha vifo na uharibifu mkubwa katika maeneo ya Marekani na Karibi. Akizungumza kutoka Incheon, Korea Kusini siku ya Jumanne, Bwana Ban amesema kimbunga hicho kimeathiri mamilioni ya familia, wakiwemo wafanyakazi wa Umoja wa Mataifa. Amesema anawaza kuhusu [...]
31/10/2012 | Jamii: Habari za wiki, Taarifa za dharura | Kusoma Zaidi »

Mkurupuko wa homa ya manjano umewaua watu 32 katika maeneo ya kati mwa Sudan na Darfur, kwa mujibu wa Shirika la Afya Duniani, WHO. Tangu wiki ya kwanza ya mwezi Oktoba, jumla ya watu 84 wanakadiriwa kuathiriwa na ugonjwa huo. Shirika la Afya Duniani linasema lilijulishwa kuhusu mlipuko wa maradhi hayo na wizara ya afya [...]
31/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Tarehe 24 mwezi Oktoba kila mwaka ni siku ya Umoja wa Mataifa, siku ya kusherehekea kuasisiwa kwa katiba ya kuanzisha Umoja wa Mataifa mwaka 1945 baada ya vita kuu ya pili ya dunia. Ikiwa ni miaka 67 tangu kuanzishwa kwake, Umoja wa Mataifa umepitia vipindi kadhaa vya raha na changamoto ambazo zimefanya Umoja huo kuimarika [...]
26/10/2012 | Jamii: Makala za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa kupitia ofisi yake ya usaidizi nchini Afghanistan, UNAMA, imelaani vikali shambulio la leo kwenye msikiti mmoja huko Maimana katika jimbo la Faryab nchini humo lililosababisha vifo vya 4o na wengine 56 wamejeruhiwa. Mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa nchiniAfghanistan, Ján Kubiš, amesema shambuliohilolimetokea wakati wa sala ya Eid el [...]
26/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la Sayansi, Elimu na Utamaduni UNESCO Bi Irina Bokova amezitaka nchi zilizoko kwenye ukanda wa Kusin Mashariki ya Ulaya kuanzisha agenda ya kukuza mashirikiano kwa shabaha ya kuinua kiwango cha urithi wa utamaduni. Hoja kama hiyo pia imetolewa na Waziri wa Utamaduni wa Bulgaria Vezhdi Rashidov, wakati [...]
26/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchi zilizoendelea zinapaswa kutekeleza ahadi zao za kusaidia kiuchumi nchi zinazoendelea na hiyo ni kauli ya Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Vuk Jeremic aliyoitoa mbele ya kikao cha barazahilojijiniNew York, Marekani. Bwana Jeremic akizungumza kwenye mkutano wa shirika la kimataifa la biashara na mandeleo, UNCTAD, ameonya kwa kutofanya hivyo viwango vya madeni [...]
26/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Haki ya kuabudu dini na imani yoyote hivi sasa inakiukwa na baadhi ya serikali duniani kwa lengo la kuweka udhibiti wa kisiasa. Hiyo ni kauli ya mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu Uhuru wa kuabudu au imani Heiner Bielefeldt aliyoitoa jijini New York Marekani alipozungumza na waandishi wa habari. Bwana Bielefeldt amesema moja ya lengo [...]
26/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon ametaka vurugu zilizoanza upya kwenye jimbo la Rakhine nchini Myanmar zikomeshwe mara moja na amezisihi mamlaka nchini humo kuchukua hatua kumaliza vurugu hizo. Ban amesema hayo kupitia kwa msemaji wake wakati huu ambapo vurugu hizo zimesababisha vifo vya wat 56 na majeruhi kadhaa na nyumba kuchomwa moto. [...]
26/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amelaani vikali mashamublizi yaliotekelezwa leo usiku kwenye nyumba ya Dk Denis Mukwege, mwanzilishi na Mkurugenzi Mkuu wa Hospitali ya Panzi katika mji wa Bukavu ulioko mkoa wa Kivu Kusini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC. Msemaji wa Bwana Ban amemkariri Katibu Mkuu huyo wa Umoja [...]
26/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakati kimbunga Sandy kikipita maeneo ya nchi za Caribbean na kusababisah vifo na mafuriko, shirika la kimataifa la uhamiaji, IOM nchini Haiti limechukua hatua za kinga usaidizi kwa kushirikiana na shirika la kiserikali la huduma za kibinadamu nchini humo DPC na lile la msalaba mwekundu nchini humo. Hatua hizo kwa mujibu wa IOM ni pamoja [...]
26/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limejiandaa kupeleka misaada ya dharura kwa maelfu ya familia za raia wa Syria kwenye maeneo yasiyofikika kutokana na mapigano iwapo makubaliano ya kusitisha mapigano hayo kwa siku nne wakati wa sikukuu tukufu ya Eid El Adha yatafikiwa. Mwakilishi wa UNHCR mjini Damascus, Syria Tarik Kurdi amesema [...]
25/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwendesha Mashtaka Mkuu wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu, ICC, Fatou Bensouda, amesema hakuna mtu yeyote ambaye atatekeleza uhalifu mkubwa na kukwepa mkono wa sheria. Bi Bensouda amesema hayo katika mkutano na waandishi wa habari mjini Nairobi, Kenya. Mapema wiki hii, amefanya mikutano na Rais Mwai Kibaki na Waziri Mkuu, Raila Odinga, na kuwasilisha masikitiko [...]
25/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kushamiri kwa vitendo vya rushwa kwenye mifumo ya kimahakama kunazua kitisho ambacho kinazorotesha haki za binadamu, ameonya mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa. Mtaalamu huyo Gabriela Knaul, amezitolea mwito serikali duniani kote kuanisha na kutekeleza sera zitakazoboresha utawala bora akisema kuwa hatua hiyo itasaidia kubinya mianya ya rushwa. Amesema wakati huu kunashuhudiwa ongezeko kubwa la [...]
25/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa umesema kuwa umekaribisha kwa matumaini makubwa hatua iliyochukuliwa na serikali ya Philippens iliyotiliana saini makubaliano ya amani na kikosi cha waasi cha Moro Islamic Liberation Front (MILF) na hivyo kuzika hali ya vita na uhasama uliodumu kwa miongo kadhaa. Makubaliano hayo yanafungua njia kupatikana kwa amani ya kudumu katika eneo la Kusin [...]
25/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kaimu Mkuu wa ujumbe wa pamoja wa Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika hukoDarfur, UNAMID, Aïchatou Mindaoudou amesisitiza umuhimu wa Umoja wa Afrika kushiriki kikamilifu katika kuendeleza harakati za kuleta amani na utulivu kwenye eneo hilo la Darfur huko Sudan. Mindaoudou amesema hayo wakati wa mazungumzo yake mjini Addis Ababa, Ethiopia na Mwenyekiti mpya [...]
25/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe amani wa Umoja wa Mataifa Stevie Wonder amesema tangu akiwa mdogo alikuwa akifuatilia jinsi Umoja huo unavyojitahidi kuleta amani katika dunia na kusema kuwa alibaini dunia ni sehemu ambapo kila mtu anapaswa kumpenda na kumjali mwenzake kwa hali yoyote ile lakini baadhi ya watu wanaifanya pawe pahala pagumu pa kuishi. Stevie Wonder ambaye anafahamika [...]
25/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya haki za wanawake Rashida Manjoo atakuwa na ziara ya siku nane nchini Bosnia Herzegovina kuanzia Jumapili yenye lengo la kukusanya taarifa kuhusu vitendo vya ukiukwaji wa haki za wanawake nchini humo. Bi. Manjoo ambaye anawajibika kufuatilia vitendo vya ukiukwaji wa haki za wanawake, chanzo na madhara [...]
25/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalam maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu mauaji yasiyo ya kisheria na kunyonga watu kiholela, Christof Heyns, leo amezikumbusha serikali kuhusu masharti yanayohusiana na utoaji wa adabu ya kifo, hususan katika nchi ambazo bado zinashikilia adabu ya kifo katika katiba zao. Bwana Heyns amesema, kwa yale mataifa ambayo bado yanaishikilia adabu ya kifo, sheria ya [...]
25/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la afya duniani, WHO limeomba washirika wake wa maendeleo na wale wa afya wazisaidie dawa nchi zilizokumbwa na njaa kutokana na mafuriko ambayo yanaweka mazingira ya mazalia ya vimelea vinavyosababisha magonjwa kama vile kichocho na trachoma au vikope. Nchi zilizo hatarani zaidi ni zile za eneo la Sahel barani Afrika ambako pia migogoro ya [...]
25/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Televisheni maarufu zaidi nchini Israel, Channel Two News, imetoa taarifa ya kurekebisha madai ya uwongo iliotoa ikisema makombora yalirushwa kutoka kwenye shule zinazoendeshwa na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na wakimbizi wa Kipalestina, UNRWA, wakati wa vita vya Gaza kati ya mwaka 2008 na 2009. Taarifa hiyo inaweka wazi kuwa maafisa wa Israel wenyewe [...]
25/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Jopo la Tume ya Umoja wa Mataifa linalochunguza ukiukwaji wa haki za binadamu nchini Syria, limemwandikia barua Rais Bashar Al-Assad wa Syria ya kuomba kuwa na mazungumzo naye, ikiwa ni mwaka mmoja sasa tangu tume hiyo kuundwa lakini haijaweza kupata kibali kuingia nchini humo kuchunguza ukiukwaji wa haki za binadamu. Mwenyekiti wa tume hiyo Paulo [...]
25/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa umeendelea kuisihi serikali ya Syria na vikundi vya upinzani nchini humo kukubaliana kusitisha mapigano kwa dhati, na kueleza kuwa kusitisha mapigano ni kiashiria chanya kuwa pande zote ziko tayari kupatia mzozo huo suluhisho la amani. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi hii leo, Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa [...]
25/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Vuk Jeremic amesema amani ya kweli haitokani na kutokuwepo kwa vita pekee, bali amani ya kweli ni matokeo ya maridhiano yaletwayo na kuombana msamaha. Bwana Jeremic amesema hayo Jumatano usiku kwenye Makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York wakati wa tamasha maalum la muziki la [...]
24/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi wa Pamoja wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya nchi za Kiarabu kuhusu Syria, Lakhdar Brahimi, amelihutubia Baraza la Usalama wa Umoja wa Mataifa leo kuhusu juhudi zake za kutafuta amani nchini Syria. Akizungumza mjini Cairo, Misri mapema leo, Bwana Brahimi amesema anatarajia tangazo kutoka kwa serikali ya Syria kuhusu pendekezo lake la kusitisha [...]
24/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wanachama wa Baraza la Usalama wamekaribisha mchakato wa mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya nchi za Kiarabu, Lakhdar Brahimi, wa kuomba mapigano na aina zote za ghasia kusitishwa wakati wa kipindi cha Siku Kuu ya Eid al-Adha. Wamerejelea pia wito wa pamoja wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa na Katibu Mkuu [...]
24/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Majaji kutoka mahakama za kijeshi mjini Mogadishu wamekutana na wawakilishi kutoka jamii ya kimataifa mjini Nairobi ili kufanya mazungumzo kwa ajili ya kuelewa vyema zaidi hali katika mfumo wa kijeshi. Mkutano huo ambao umeandaliwa na afisi ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya Somalia, UNPOS, umetambua ni vipi usaidizi wa Umoja wa Mataifa na wafadhili [...]
24/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Huku nchi nyingi zikiwa zinachukuwa hatua kusitisha uharibifu wa rasilmali za jenetikia ya mifugo, ambazo ni muhimu kwa chakula na kilimo, bado kuna mwanya mkubwa ambao unatakiwa kukabiliwa kwa haraka. Hayo ni kwa mujibu wa ripoti za Shirika la Chakula na Kilimo, FAO, ambazo zimewasilishwa leo katika kongamano la kimataifa kufuatia utafiti uliofanywa katika nchi [...]
24/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Maadhimisho ya siku ya Umoja wa Mataifa yamefanyika sehemu mbali mbali duniani ikifahamika kuwa Umoja huo ulioanzishwa mwaka 1945 una wanachama 193 na miongoni mwa wanachama hao ni Burundi ambako sherehe zimefanyika kwenye mji mkuu Bujumbura na wananchi kutoa maoni yao juu ya nafasi ya Umoja huo katika kujenga amani. Mwandishi wetu Ramadhani Kabuga kutoka [...]
24/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa, UNESCO Irina Bokova amelaani vikali mauaji ya mpiga picha wa televisheni wa Syria yaliyofanyika kwenye mji wa mashariki wa Deir Al-Zour nchini humo. Katika taarifa yake, Mkuu huyo wa UNESCO, shirika lenye wajibu wa kulinda uhuru wa vyombo vya habari, pia ametaka [...]
24/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa na ule wa Jumuiya ya nchi za kiislamu OIC ambao ulikuwa nchini Benin kutathmini hali mbaya iliyosababishwa na mafuriko ya hivi karibuni umejadilia haja ya kutumwa misaada ya dharura kuwanusuru mamia ya watu ambao maisha yao yako taabani. Ujumbe huo ulikuwa nchini humo kwa siku tatu na kutathmini hali jumla [...]
24/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Somalia, Augustine Mahiga, amelaani mashambulizi ya hivi karibuni yaliyowalenga waandishi wa habari nchini Somalia. Mnamo siku ya Jumanne, mwandishi wa habari wa Universal TV, Ahmed Saakin Farah Ilyas, alipigwa risasi na kuuawa katika mji wa Las-Anod kwenye eneo la Sool. Mnamo tarehe 21 Oktoba, mwandishi habari mwingine, Mohamed [...]
24/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakati leo ni siku ya kutokomeza Polio duniani, shirika la afya la Umoja wa Mataifa, WHO limesema jitihada za kumaliza ugonjwa huo zinaendelea vizuri licha ya kwamba bado ugonjwa huo ni tishio nchini Nigeria, Afghanistan na Pakistani. WHO imesema kuwa nchi hizo zimekuwa na jumla ya wagonjwa 166 wa Polio kati ya watoto 171 waliougua [...]
24/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchini Tanzania, maadhimisho ya siku ya Umoja wa Mataifa yamefanyika jijini Dar Es Salaam ambapo shughuli mbali mbali zilifanyika kama vile makongamano, maonyesho na uhifadhi wa mazingira. George Njogopa na taarifa zaidi. (SAUTI YA GEORGE NJOGOPA) Maafisa wa Umoja wa Mataifa nchini Tanzania leo wameungana na wale wa serikali pamoja na raia wa kawaida kuadhimisha [...]
24/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amesema wakati taasisi za kimataifa zinakumbwa na majaribu kutokana na migogoro, ukosefu wa usawa na kutokuvumiliana duniani, Umoja wa Mataifa unalazimika kuendeleza kasi yake ya kuleta amani, maendeleo, kusimamia utawala wa kisheria na kuwajengea uwezo wanawake na vijana duniani kote. Ban amesema hayo katika ujumbe wake wa [...]
24/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ametoa ujumbe wa maadhimisho ya siku ya Umoja wa Mataifa na kusisitiza utekelezaji wa ahadi ya umoja huo ya kusitisha vita na kupatia suluhu migogoro isiyoonekana kama vile chuki, njaa, magonjwa na uharibifu wa mazingira. Siku ya Umoja wa Mataifa huadhimishwa kila tarehe 24 ya mwezi Oktoba [...]
23/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »

Wataalam watatu huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu hali ya haki za binadam nchini Iran, hukumu za kunyonga na utesaji, leo wameelezea kughadhabishwa na kunyongwa kwa Saeed Sedighi na watu wengine tisa kwa makosa yanayohusiana na dawa za kulevya. Wataalam hao, ambao ni Ahmed Shaheed, Christof Heyns na Juan E. Menendez, wamelaani vikali mauaji hayo, [...]
23/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalamu wa Umoja wa Mataifa kuhusu masuala ya mateso, Juan Méndez amesema serikali zinapaswa kufikiria iwapo adhabu ya kifo yenyewe imeshindwa kuheshimu hadhi ya binadamu, inasababisha mateso ya kifikra na kimwili. Akiwasilisha ripoti yake mbele ya Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa hii leo mjini New York, Marekani, Mendez amesema mpaka sasa adhabu ya kifo [...]
23/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa vikosi vya ulinzi wa amani vya Umoja wa Mataifa amejadilia kile alichokiita haja ya kubadili mkondo wa mambo pamoja na kuwa na majumuisho ya pamoja kwa duru za kimataifa ili kuzikabili changamoto za ulinzi wa amani ambazo zinakwaza operesheni mbalimbali duniani. Amesema kuna haja ya jumuiya ya kimataifa kuwan na kusudio la pamoja [...]
23/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Maafisa wa serikali ya Sudan na wale wa kundi la waasi wamekubaliana kwa msingi kuendelea na duru la majadiliano na tayari pande zote mbili zimetiliana saini itifaki inayotambulisha utayari wa kukaribisha meza ya majadiliano. Kundi la Usawa na Haki ambalo ni miongoni mwa makundi ya waasi katika eneo la Darfur lilichangia kuzorotesha usalama wa eneo [...]
23/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ripoti mpya ya Umoja wa Mataifa iliyotolewa hii leo inaonyesha kuwa maeneo ya Asia na Pacific ndiyo yanayoathirika zaidi kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa ambayo pia yamesababisha athari kwa maendeleo ya kiuchumi ya eneo hilo. Kulingana na wengi bara la Asia na eneo la Pacific mwaka 2011 utakumbukwa kama mwaka wa majanga makubwa [...]
23/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Uwekezaji wa kigeni ulipungua kwa asilimia 8 kwenye miezi sita ya kwanza ya mwaka 2012 kutokana na misukosuko ya kiuchumi kwenye robo ya pili ya mwaka 2012. Ukuaji wa kujikokota wa uchumi duniani na hatari zinazotokana na kubadilika kwa sera kunayafanya makambuni mengi kuamua kutumia mbinu ya kusubiri na kuona yanapowekeza nje. Katibu mkuu wa [...]
23/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Hali ya ukosefu wa usalama pamoja na kuongezeka kwa misukosuko nchini Lebanon vimelazimu shirika la kuhudumia wakimbii la Umoja wa Mataifa UNHCR kusitisha kwa muda uandikishaji wa wakimbizi wa Syria nchini humo. Kati ya miji ambayo shughuli za uandikishanji zilisimaishwa ni pamoja na mji mkuu Beirut, Tripoli, Akar na Saidia. UNHCR inasema kwamba idadi ya [...]
23/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, leo amemkabidhi tuzo mshindi wa shindano la sanaa kwa ajili ya amani, Bi Haruka Shoji, katika hafla ilofanyika kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York. Shindano hilo la sanaa kwa ajili ya amani liliandaliwa na afisi ya masuala ya kuondoa silaha ya Umoja wa [...]
23/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa, UNHCR, limesema idadi ya wakimbizi wa Syria ambao wameandikishwa nchini Lebanon imeongezeka na kuzidi laki moja. Tayari wakimbizi wa Syria wamezidi idadi hiyo ya laki moja katika nchi za Uturuki na Jordan, huku idadi ya wakimbizi wa Syria katika kanda nzima ikiwa imepanda na kuzidi 358, 000. [...]
23/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkutano wa kimataifa wa teknolojia ya habari na mawasiliano kuhusu kujenga uwezo wa wafanyakazi unafanyika nchini Afrika Kusini ambapo umeangazia zaidi mchakato wa kuhama kutoka mfumo wa utangazaji wa analojia kwenda digitali. Katika mkutano huo Shirika la mawasilano duniani, ITU limetoa chapisho kuhusu masuala ya digitali na maamuzi yanayopaswa kufanya huku likielimisha washiriki juu ya [...]
23/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchi za Algeria, Libya, Mauritania na Morocco zinaweza kukumbwa na baa la nzige wiki chache zijazo kutoka eneo la Sahel Afrika Magharibi na hivyo zimetakiwa kujiandaa kukabiliana na wadudu hao waharibifu. Tahadhari hiyo imetolewa na Shirika la Chakula na Kilimo duniani, FAO ambapo mtaalamu mwandamizi wa utabiri wa mwelekeo wa nzige katika shirika hilo Keith [...]
23/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la mpango wa chakula duniani, WFP limesema idadi ya watu wanaokabiliwa na uhaba wa chakula nchini Madagascar imeongezeka na kufikia asilimia 33 ya wananchi wote nchini humo.. Msemaji wa WFP Elizabeth Byrs amesema hayo mjini Geneva, Uswisi leo alipozungumza na waandishi wa habari ambapo amesema malengo ya shirika hilo ni kuwapatia chakula watu Milioni [...]
23/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Vuk Jeremić leo amekuwa na mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Argentina, Hector Timerman ambapo Waziri huyo amemtaarifu juu ya kushikiliwa kwa meli ya kivita ya nchi hiyo, Libertad kwenye bandari ya Tema nchini Ghana. Katika mazungumzo hayo yaliyofanyika kwenye makao makuu ya umoja huo [...]
22/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa umelaani shambulizi lililotekelezwa dhidi ya kambi ya kijeshi nchini Guinea-Bissau mnamo siku ya Jumapili, na kuelezea kusikitishwa na vifo vilivyotokana na shambulizi hilo. Katika taarifa ilotolewa siku ya Jumatatu, Umoja wa Mataifa umesema unafuatilia kwa karibu hali ilivyo. Mwakilishi maalum wa ofisi ya amani ya Umoja wa Mataifa nchini Guinea-Bissau (UNIOGBIS), Joseph [...]
22/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la chakula na kilimo, FAO, limetangaza kuidhinishwa kwa mkakati wa miaka miwili wa kubuni kanuni za uwekezaji wenye kuwajibika, kuheshimu haki za binadamu, riziki za watu na rasilmali. Mkakati huo umeidhinishwa na Kamati ya FAO kuhusu usalama wa chakula, CFS, mwishoni mwa kikao chake cha 39 kwenye makao makuu ya FAO mjini Roma. Chini [...]
22/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa huduma za kibinadamu wa Umoja wa Mataifa amehimiza kuwepo mabadiliko katika wakati ambapo jumuiya ya kimataifa ikijishughulisha na utoaji wa huduma za dharura ikiwemo pia kuipiga jeki serikali ya Benin inayokabiliwa na hali ya kuwakwamua raia wake waliokumbwa na mafuriko. Bi Valarie Amos amesema kuwa lazima kuchukuliwe njia mujarabu kuwataarifa wananchi wa eneo [...]
22/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mratibu maalum wa Umoja wa Mataifa kwa masuala ya Lebanon Derek Plumbly na mabalozi wa nchi tano zenye ujumbe wa kudumu katika Baraza la Usalama la umoja huo wamekutana na Rais wa Lebanon Michel Sleiman mjini Baada na kuelezea mshikamano wao na nchi hiyo wakati huu wa kipindi kigumu. Taarifa iliyotolewa imesema wakati wa mazungumzo [...]
22/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya nchi za Kiarabu kuhusu Syria, Lakhdar Brahimi, amekutana na kufanya mazungumzo na Rais Bashar al-Assad wa Syria kuhusu hali ilivyo nchini humo, na masuala yote yanayohusiana na mzozo wa Syria. Bwana Brahimi amewaambia waandishi wa habari mjini Damascus kuwa mkutano wake na Rais Assad uliangazia pia [...]
22/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwendesha mashata mkuu kwenye mahakama ya kimataifa ya uhalifu wa kivita ICC Fatou Bensouda yuko nchini Kenya kwa ziara ya juma ambapo anatarajiwa kukutana na mafisa wa ngazi za juu serikalini akiwemo rais na Waziri mkuu. Akihutubia waandishi wa habari mjini Nairobi hii leo , mwendesha mashtaka huyo amesema anataraji kukutana na mashirika ya umma [...]
22/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Jopo la wataalamu 11 wa Umoja wa Mataifa limeitaka serikali na bunge la Colombia kuangalia upya mapendekezo ya marekebisho ya katiba hususan sheria za vitendo vya uhalifu unaofanywa na jeshi, kwa kuwa mapendekezo hayo yanaweza kuwa na madhara makubwa katika utawala wa kisheria na utekelezaji wa haki za binadamu nchini humo. Wito huo umo kwenye [...]
22/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban ki-Moon, ameelezea kushangazwa na mapigano katika mji wa Ban Walid nchini Libya, na hususan ripoti za mauji ya raia wengi kutokana na urushaji makombora kiholela. Bwana Ban amezikumbusha pande zote katika mapigano hayo kuhusu wajibu wao chini ya sheria ya kibinadamu ya kimataifa, na kutoa wito kwa serikali [...]
22/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Homa ya Marburg yaua watu watano nchini Uganda: WHO Mwakilishi wa shirika la Afya duniani WHO nchini UGANDA, Dkt. Joaquim Saweka, amesema watu watano wamekufa kutokana na ugonjwa wa homa ya Marburg uliolipuka katika wilaya ya Kabale, kusini magharibi mwa nchi hiyo. Dkt. Saweka akizungumza na Radio ya Umoja wa Mataifa amesema waliokufa ni kati [...]
22/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, BanKi-Moon na mwakilishi maalum wa UM wa muungano wa nchi za Kiarabu wameziomba pande zote husika katika mgogoro wa Syria kusikia wito uliotolewa kutakiwa kusitisha mapigano wakati wa kipindi cha sikukuu ya Eid El Haji ili kutoa fursa kwa raia wa nchi hiyo kusherehehea siku hiyo takatifu kwa amani na [...]
19/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Naibu Mkuu wa Masuala ya Kibinadam katika Umoja wa Mataifa, Catherine Bragg ametoa wito kwa nchi zilizo kusini mwa bara la Afrika kuimarisha ushirikiano katika juhudi za kuendeleza uwezo wa kujiandaa kwa ajili ya majanga na kukabiliana na uhaba wa chakula. Bi Bragg ametoa wito huo wakati akihitimisha ziara yake ya siku tano kwenye eneo [...]
19/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na uhamiaji IOM, linakusudia kuendesha mafunzo ya siku mbili kwa maafisa wa Iran ikiwajengea uwezo kwenye maeneo ya uhamiaji na maendeleo. Mafunzo hayo ambayo yanafanyika kwa ushirikiano wa pamoja baina ya IOM na serikali ya Kiislamu ya Iran yamepangwa kufanyika Oktoba 22 na 23 katika jimbo la Mazandaran . [...]
19/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kiasi cha raia 261 wa Ufilipino waliokuwa wamejikusanya kwenye ubalozi wa Filipini nchini Syria kwa ajili ya kupata hifadhi ya muda, wamerejea nchini mwao kwa kusafirishwa na ndege ya shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na uhamiaji IOM. Hii ni mara ya pili kwa ndege ya shirika hilo kuwarejesha raia wa Ufilipino na mara ya [...]
19/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kila mwaka Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa huwa na juma moja la bara la Afrika. Katika kipindi hicho hufanyika mjadala wa pamoja wa wazi kuhusiana maendeleo ya Afrika, bara lenye idadi kubwa ya wanachama katika chombo hicho cha dunia chenye wanachama 193. Mwaka huu masuala yaliyomulikwa ni ripoti ya maendeleo ya ushirikiano kati ya [...]
19/10/2012 | Jamii: Makala za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Jan Eliasson, amesema kuwa ni lazima serikali ya Mali isaidiwe kuunda na kutekeleza mfumo wa kisiasa ambao unakabiliana na chanzo cha mzozo wa taifa hilo. Bwana Eliasson amesema hayo wakati wa mkutano baina yake na viongozi wa Muungano wa Afrika, jumuiya ya kiuchumi ya Afrika Magharibi, ECOWAS, ambao [...]
19/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Ravina Shamsadani amelaani vikali mashambulizi ya siku ya Jumatano Kaskazini mwa Darfur shambulizi yaliyolenga msafara wa wanajeshi wa Umoja wa Mataifa, polisi , wafanyikazi wa Umoja wa Matifa pamoja na maafisa wawili wa haki za binadamu.Msafara wa kikosi cha Pamoja cha Umoja wa Mataifa na Muungano [...]
19/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu masuala ya kibinadamu, OCHA, imesema kuwa mfumuko wa bei nchini Syria ambako bado mapigano yanaendelea kati ya majeshi ya serikali na vikosi vya upinzani umeongezeka na kufikia silimia 36 mwezi Julai mwaka huuu. Msemaji wa OCHA, Jens Laerke amewaambia waandishi wa habari mjini Geneva, Uswisi hii leo kuwa [...]
19/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, amesema ulimwengu una chakula cha kutosha kuweza kumlisha kila mtu, na kutoa wito hatua zichukuliwe za kutokomeza njaa. Bwana Ban amesema hayo kwenye hafla ya kutoa tuzo ya kimataifa ya chakula, ambayo imefanyika mjini Des Moines, Iowa. Katibu Mkuu amesema kutokomeza njaa kunahitaji uongozi bora wa kimataifa, [...]
19/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Idadi ya wakimbizi kutoka Somalia wanaoishi kwenye kambi ya wakimbizi ya Dollo Ado kusini mashariki mwa Ethiopiam imepita wakimbizi 170,000 kwa mujibu wa shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR. UNHCR inasema kuwa kambi ya Dollo Ado ndiyo ya pili zaidi kwa ukubwa duniani baada ya kambi ya Daadab nchini Kenya ambayo ni [...]
19/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mtendaji wa Tume ya Umoja wa Mataifa ya uchumi kwa Afrika, UNECA, Carlos Lopes amesema kardi uchumi wa Afrika unavyoimarika, vurugu zitokanazo na chaguzi za kisiasa zitapungua kutokana na kuongezeka kwa uelewa wa raia wake na kutarajia kushiriki zaidi kwenye masuala ya siasa. Amesema japo chaguzi zimekuwa jambo la kawaida lakini bado uhalali na [...]
19/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Tume ya Umoja wa Mataifa ya masuala ya uchumi na kijamii kwa nchi za Asia na Pacific kwa kushirikiana na Jamhuri ya Korea zitatoa tuzo maaluum kwa watu Kumi walio mstari wa mbele kutetea haki za walemavu. Tuzo hiyo itatolewa tarehe Mosi mwezi ujao huko Incheon, Korea Kusini wakati wa mkutano wa ngazi ya juu [...]
19/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Miaka 60 tangu Rais wa zamani wa Marekani, hayati Franklin Delano Roosevelt ataje aina nne za uhuru, mpaka sasa maneno yake hayo yamebakia mwongozo kwa watu duniani kote. Hiyo ni kauli ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon aliyoitoa leo jijini New York, Marekani wakati wa hafla ya kuipatia bustani moja karibu na [...]
18/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Burkina Faso na Niger zimekamilisha kuwasilisha malalamiko yao katika mahakama ya kimataifa ya haki juu ya mzozo wa mpaka ambao unagombewa na pande zote. Mahakama hiyo inatazamiwa kutoa maamuzi yake katika kipindi cha miezi minne hadi sita. Wakati ikiwasilisha madai yake, Burkina Faso ilitaka Mahakama hiyo kuzingatia mpaka ulioasisiwa na koloni la zamani Ufaransa wakati eneo [...]
18/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amepongeza mabunge ya Sudan na Sudan Kusini kwa kuridhia mikataba ya ushirikiano kati ya nchi mbili hizo iliyotiwa saini mwezi uliopita na marais wao Salva Kiir wa Sudan Kusini na Omar Al Bashir wa Sudan.. Ban amekaririwa na msemaji wake akizitaka nchi mbili hizo sasa kutekeleza makubaliano [...]
18/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Jopo la wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa linaloshughulikia suala la unyanyasaji dhidi ya wanawake kisheria na kimatendo limezitaka serikali kufuta sheria zote zinazotambua uzinzi kuwa kosa la jinai na kuweka adhabu kama vile faini, kifo kwa kunyongwa au kupigwa mawe. Mkuu wa jopo hilo linalokutana mjini Geneva, Uswisi Kamala Chandrakirana amesema uzinzi haupaswi kabisa [...]
18/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchi za Rwanda, Argentina, Australia, Luxembourg, na Jamhuri ya Korea, leo zimechaguliwa kama wanachama wasio wa kudumu kwenye Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa. Uchaguzi huo umefanyika katika kikao maalum cha Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York. Wanachama hao wasio wa kudumu watahudumu kwa kipindi cha miaka miwili, kuanzia Januari 1 [...]
18/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wanaume wakiwemo watoto wa kiume wanazidi kuwa waathiriwa wa dhuluma za kingono kwenye mizozo kwa mujibu wa mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu dhuluma za kimapenzi kwenye mizozo Zainabu Hawa Bangura. Akiongea mjini Geneva Bi Bangura amesema kulingamiza suala la dhuluma za kimapenzi kwenye mizozo sio kitu kigumu lakini itahitajika kujitolea kisiasa, kuwepo mabadiliko [...]
18/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ingawa idadi ya maeneo ya hifadhi, na mbuga za wanyama imeongezeka kote duniani, nusu ya maeneo yenye bayo-anuai ya kuaziziwa zaidi hayana ulinzi wowote. Haya ni kwa mujibu wa ripoti ya uchunguzi mpya wa Shirika la Mpango wa Mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP, ambao unafuatilia maendeleo yanayofanywa kuhusu malengo ya kimataifa yaliyoazimiwa kuhusu maeneo [...]
18/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Syria inaweza kutumbukia katika mgogoro wa chuki baina ya makundi yenye misimamo tofauti wakati huu ambapo jumuiya ya kimataifa imegawanyika juu ya hatua za kuchukua kumaliza mzozo huo uliodumu kwa miezi mwaka mmoja na nusu sasa. Hiyo ni kauli ya Mkuu wa Tume ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, Navi Pillay aliyotoa leo [...]
18/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la chakula na kilimo duniani, FAO, Jumuiya ya uchumi ya nchi za Afrika Magharibi, ECOWAS na Ujerumani zimezindua mradi wa pamoja wa kuhakikisha kuna utashi wa kisiasa na ushiriki mkubwa wa serikali na wadau katika kutokomeza njaa Afrika Magharibi. Mkurugenzi Mkuu wa FAO, José Graziano da Silva amesema mradi huo wa miaka mitatu ni [...]
18/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ugonjwa wa Malaria umeelezwa kuwa bado ni tishio barani Afrika kutokana na vikwazo mbali mbali licha ya utashi wa kisiasa wa kutokomeza ugonjwa huo hivyo msaada zaidi wa wataalamu na vifaa tiba unahitajika. Kauli hiyo ni ya Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania, Mahadhi Juma Maalim aliyotoa alipozungumza na Radio ya Umoja wa [...]
18/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amelaani vikali shambulio la kushtukiza huko Darfur, Sudan, dhidi ya msafara wa askari na watumishi wa kiraia walio katika kikosi cha kulinda amani cha Umoja wa Mataifa na Umoja wa Afrika, UNAMID, lililosababisha kifo cha mlinda amani mmoja kutoka Afrika Kusini na kujeruhi wengine wa tatu. Msemaji [...]
17/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »

Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya nchi za Kiarabu, Lakhdar Brahimi, amesema kuwa nchi katika kanda ya Mashariki ya Kati zinafaa kufahamu kuwa mzozo wa Syria hauwezi kubakia ndani ya mipaka ya Syria daima, na kuonya kuwa mzozo huo ama utasuluhishwa au utaenea nje ya mipaka ya Syria na kummeza kila mmoja. [...]
17/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Askari Sita wa kikundi cha kulina amani cha Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC pamoja na mkalimani mmoja wamejeruhiwa katika shambulio la kushtukiza lililofanyika usiku wa kuamkia Jumatano huko Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo, DRC. Taarifa ya MONUSCO imesema shambulio hilo katika eneo la Buganza, jimbo la Kivu Kaskazini [...]
17/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, ameuambia mjadala wa hadhara wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kuhusu amani na haki kuwa, majira ya sasa dunaini ni ya uwajibikaji. Bwana Ban amesema viongozi wa kiimla na wababe wa vita ambao hutekeleza uhalifu hawawezi tena kuacha mamlaka na kupewa hifadhi salama ng'ambo bila [...]
17/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalam maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu umaskini wa kupindukia, Magdalena Sepúlveda, ametoa wito kwa serikali kote duniani kuchukua hatua mara moja kuhakikisha watu maskini zaidi wanapata haki, katika kuadhimisha siku ya kimataifa ya kutokomeza umaskini. Bi Sepulveda amesema kuwa na uwezo wa kupata haki kwenyewe ni haki ya binadamu, na kusema kuwa kila serikali [...]
17/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, Vuk Jeremic, amesema maendeleo ya bara la Afrika yanapaswa kuwa sehemu muhimu ya majukumu ya mfumo mzima wa Umoja wa Mataifa. Bwana Jeremic amesema hayo wakati wa kufungua vikao maalum vya juma la bara la Afrika kwenye Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, chini ya Ushirikiano Mpya [...]
17/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Taifa la Brazil pamoja na shirika la kilimo na mazao la Umoja wa Mataifa FAO wametia sahihi makubaliano ya ushirikiano wa Kusini- Kusini wenye gharama ya dola milioni 20 yaliyo na lengo la kutuma utaalamu kuhusu pamba kutoka nchini Brazil kwenda nchi zingine zinazoendelea. Ushirikiano huo wa miaka minne kati ya FAO na taasisi ya [...]
17/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amesema kuwa kuna haja ya kuwepo kwa mchakato wa haraka wa kisiasa ili kujadilia na kubaini kiini cha kuzuka kwa vita vya kiraia nchini Sri Lank, vilivyomalizika miaka mitatu iliyopita kwa serikali kuibuka mshindi dhidi ya kundi la waasi la Tamil. Ban amesema hayo wakati alipokutana na [...]
17/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa umesema kuwa unatiwa shaka juu ya mwenendo wa vikosi vya kimataifa nchini Afghanistan kufuatia kuwepo uwezekano wa watoto watatu kuwa ni miongoni mwa waliopoteza maisha baada ya vikosi hivyo vya kimataifa kufanya shambulizi la angani . Katika taarifa yake msaidizi wa Katibu Mkuu juu ya masuala ya watoto na maeneo yenye mizozo [...]
17/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakati dunia leo inaadhimisha siku ya kutokomeza umaskini, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon amesema jitihada za kutokomeza umaskini zinakumbwa na tishio la uhaba wa fedha katika kipindi hiki ambacho serikali zinachukua hatua kali za kubana matumizi ili kuinua uchumi. Ban amesema licha ya hatua hizo, huu ni wakati wa kuhakikisha maskini wanapata [...]
17/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia, Balozi Augustine Mahiga amepongeza hatua ya bunge la nchi hiyo kumpitisha Abdi Farah Shirdon kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Somalia. Wabunge wote 215 waliridhia Shirdon kuwa Waziri Mkuu ambapo Balozi Mahiga amesema kitendo hicho ni ushahidi tosha usio na utata kuwa Somalia inasonga mbele. Halikadhalika amesema [...]
17/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkakati mpya wa kutumia teknolojia ya simu za mkononi kusaidia kukabiliana na magonjwa yasiyo ya kuambukiza, umezinduliwa na Shirika la Kimataifa la Mawasiliano, ITU kwa ushirikiano na Shirika la Afya Duniani, WHO, mjini Dubai. Teknolojia hiyo, hususani ujumbe mfupi na apps, inatarajiwa kutumiwa katika kukabiliana na magonjwa kama kisukari, saratani, maradhi ya moyo na mengineyo [...]
17/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la afya duniani, WHO limesema uhaba mkubwa wa fedha unatishia jitihada za kimataifa za kutibu na kuzuia kuenea kwa ugonjwa wa Kifua Kikuu. WHO imesema kwa kipindi cha miaka mitatu ijayo zinahitajika dola Bilioni Nne nukta Nne zaidi kwa ajili ya mipango ya kukabiliana na TB ikiwemo utafiti wa dawa mpya. Shirika hilo limesema [...]
17/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Makubaliano ya hivi karibuni kati ya Sudan na Sudan Kusini yanaonyesha matumaini ya uhusiano mzuri kati ya pande mbili hizo. Huo ni ujumbe wa balozi wa Sudan Kusini Francis Deng aliowaeleza waandishi wa habari kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani mara baada ya mkutano na Baraza la Usalama. Mwezi uliopita [...]
17/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ripoti mpya ya shirika la mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP imetaka mjadala wa usalama wa chakula duniani uzingatie masuala ya mazingira ikiwa ni pamoja na kulinda mazingira ya kiekolojia yanayosaidia uzalishaji wa chakula. Ikiwa imezinduliwa leo wakati wa siku ya chakula duniani, ripoti hiyo iliyoandikwa an wanasayansi na watalaamu 12 imesema kitendo cha kuhifadhi [...]
16/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa hii leo limeombwa kukubali ombi la Umoja wa Afrika, AU, la kuimarisha ulinzi wake eneo la baharini huko Somalia. Ombi hilo limewasilishwa na Mkuu wa ofisi ya Umoja wa Mataifa nchini Somalia, Dkt. Augustine Mahiga alipohutubia kwa njia ya video baraza hilo kutoka mji mkuu wa Somalia, Mogadishu. [...]
16/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la uhamiaji la Umoja wa Mataifa, IOM limewarejesha katika familia zao watoto 51 nchiniUgandaambao walisafirishwa kutoka vijijini hadi mijini hususan mji mkuuKampala. IOM imesema watoto hao waliorejeshwa huko Karamoja, kaskazini mwaUganda, waliletwa mjini na kujikuta wakilazimika kuwa ombaomba mitaani au wezi na hata kutumikishwa majumbani au kuokota vyuma chakavu. Hali hiyo ilifanya watoto hao [...]
16/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Chama cha kimataifa cha mawasiliano ITU kimezindua mipango miwili mipya yenye malengo ya kuboresha teknolojia ya mawasiliano hasa mawasiloano ya matandao kipitia simu za mkononi. Mipango hiyo miwili inayojulikana kama m-Powering Development na Smart Sustainable Development Model ilinzinduliwa mwaka 2012 na sasa iko kwenye maonyesho mjini Dubai. Chama cha ITU kinalenga kuboresha teknolojia na mawasiliano [...]
16/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa Ujumbe wa Umoja wa kimataifa wa kulinda amani katika jimbo lenye mzozo la Darfur nchini Sudan amelaumu upigaji hatua mdogo juu ya utekelezaji wa makubaliano ya amani baina ya serikali na vikosi vya waasi na amezitolea mwito pande zote kufanya juhudi kugharimia hali ya usalama na amani ya eneo hilo. Aïchatou Mindaoudou,anayeongoza ujumbe [...]
16/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na uhamiaji IOM, linashirikiana na mamlaka za kikanda nchini Somalia kwa ajili ya kusambaza huduma za dharura kwa familia zaidi 262 ambazo ziko katika hali mbaya baada ya kuathiriwa na moto katika eneo la Gorowe . Eneo hilo lililoko katika jimbo la Puntland ambalo limeharibiwa na moto limeshuhudia watu [...]
16/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon ametoa ujumbe wake kwa siku ya chakula duniani na kusema kuwa mwelekeo wa pamoja unaochochea vyama vya kilimo vya ushirika ni muhimu katika kufikia lengo la kutokomeza njaa alilozindua wakati wa mkutano wa Rio + 20 nchini Brazil. Ban amesema kutokomeza njaa ni dira ya kuwa na [...]
16/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika kuadhimisha siku hii ya chakula duniani, mashirika mengine ya Umoja wa Mataifa pia yametaja umuhimu wa mashirika katika kuulisha ulimwengu. Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Ajira Duniani, ILO, Guy Ryder, amesema mashirika haya yana mchango muhimu kuhakikisha haki ya kuwa na chakula inafurahiwa na wote, wakati huu ambapo watu milioni 870 wana upungufu wa [...]
16/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Zaidi ya Wasyria 16,000 wametuma maombi ya kutaka kupewa hifadhi kwenye Jumuiya ya Ulaya kwa muda wa miezi 18 iliyopita kwa mujibu wa shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR. Kati ya mataifa yaliyopokea kiwango kikubwa cha maombi ni pamoja na Ujerumani, Sweden na Uswisi. UNHCR inatoa wito kwa wanachama wa Jumuiya ya [...]
16/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la chakula na kilimo, FAO, limesema mashirika ya wakulima, ambayo tayari yanawahusisha mamilioni ya wakulima wadogo, yanaweza kupanuliwa na kuchangia kwa kiasi kikubwa hata zaidi katika kukabiliana na umaskini na njaa, iwapo yataungwa mkono ipasavyo na serikali, mashirika ya umma na wasomi. Kauli hii imetolewa katika kuadhimisha siku ya chakula duniani leo, ambayo inasherehekewa [...]
16/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamati moja kuu ya Umoja wa Mataifa imezindua ukaguzi mpya wa miaka minne wa shughuli za kimaendeleo za Umoja wa Mataifa kuambatana na mabadiliko yanayoendelea kushuhudiwa duniani. Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Jan Eliasson amesema kuwa mifumo ya maendeleo duniani imebadilika zikiwemo changamoto za maendeleo. Eliasson amesema kuwa nchi zaidi zinautaka ulikwengu kufanya [...]
16/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Vijana Milioni 200 katika nchi zinazoendelea wenye umri wa kati ya miaka 15 hadi 24 hawakumaliza elimu ya msingi na hivyo wanahitaji njia mbadala ya kuwapatia stadi za msingi kuweza kuajiriwa au kuwa na maisha bora. Hiyo ni kwa mujibu wa ripoti mpya ya Kumi ya shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na [...]
16/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Zaidi ya raia Milioni 1.4 wa Syria wanategemea msaada wa chakula unaotolewa na Shirika la mpango wa chakula duniani, WFP kutokana na uhaba wa chakula na kupanda maradufu kwa bei ya vyakula katika maeneo yenye mapigano nchini Syria. Mathalani WFP imesema uhaba wa mafuta umefanya vyakula muhimu kama mikate kutokapatikana kwa sababu viwanda vya kuoka [...]
16/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon ametuma salamu za rambi rambi kwa serikali na wananchi wa Cambodia kufuatia kifo cha mfalme wa zamani wa nchi hiyo Norodom Sihanouk aliyefariki dunia nchini China akiwa na wa miaka 89 kutokana na mshtuko wa moyo. Taarifa ya msemaji mkuu wa Ban imesema Katibu Mkuu huyo [...]
15/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Uwezekano wa kuwa na taifa la Palestina na Israeli kama suluhisho la mgogoro kati yao unaonekana kupungua. Hiyo ni kauli ya afisa mwandamizi wa Umoja wa Mataifa, Jeffrey Feltman aliyoitoa mbele ya kikao cha Baraza la Usalama la Umoja huo jijini New York, Marekani hii leo. Feltman ambaye ni mkuu wa masuala ya siasa ndani [...]
15/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayohusika na udhibiti wa madawa ya kulevya na uhalifu, UNODC imezungumzia vitendo vya uhalifu unaopangwa ikiwemo usafirishaji wa madawa ya kulevya, na kutaka nchi zote duniani kuwa makini na kuchukua hatua za mapema za kubadilishana taarifa juu ya kupambana na vitendo hivyo. Riikka Puttonen ambaye ni afisa kutoka kitengo cha [...]
15/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wataalamu wa masuala ya utalii barani afrika leo wanaanza kongamano la siku tano nchini Tanzania ambalo pamoja na mambo mengine linatazamiwa kujadilia usimamizi wa utalii endelevu katika hifadhi za taifa. Kongamano hilo ambalo limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Tanzania na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na utalii linahudhuriwa na wajumbe zaidi ya [...]
15/10/2012 | Jamii: Mahojiano | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa na Jumuiya ya nchi za kiarabu katika mzozo wa Syria, Lakhdar Brahimi, amehitimisha ziara Uturuki kwa kuwa na majadiliano na rais Abdullah Gul na waziri wa Mambo ya Nje Ahmet Davutoglu. Viongozi wamekubaliana haja ya kukomesha uhasama wa pande mbili ambazo hivi karibuni zilifurumishiana makombora ikiwa jitihada za kila [...]
15/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamati inayohusika na usalama wa chakula ya Shirika la Kilimo na Chakula, FAO, imeanza mikutano yake ya wiki moja hii leo katika makao makuu ya FAO mjini Roma, Italia, siku moja kabla ya Siku ya Chakula Duniani, ambayo huadhimishwa kila tarehe 16 Oktoba. Kamati hiyo ndilo jukwaa la jumla serikali za kimataifa, mashirika ya umma, [...]
15/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa katika mzozo wa Syria, Lakhdar Brahimi ameiomba Iran isaidie kufanikishwa kwa usitishaji wa mapigano nchini Syria wakati wa sikukuu ya Eid El Haji, wiki ijayo, siku ambayo amesema ni moja ya tukufu zaidi miongoni mwa waumini wa dini ya kiislamu duniani kote. Bwana Brahimi ametoa rai hiyo baada ya [...]
15/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wanawake wa vijijini ndio huzalisha asilimia kubwa ya chakula, ndio hutunza mazingira kusaidia katika kupunguza hatari ya majanga miongoni mwa jamii zao. Hii ni kwa mujibu wa katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenye ujumbe wake wakati wa maadhimisho ya siku ya kimataifa ya wanawake wa vijijini inayoadhimishwa tarehe 15 mwezi oktoba kila mwaka. Ban [...]
15/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wataalamu wa masuala ya utalii barani afrika leo wanaanza kongamano la siku tano nchini Tanzania ambalo pamoja na mambo mengine linatazamiwa kujadilia usimamizi wa utalii endelevu katika hifadhi za taifa. Kongamano hilo ambalo limeandaliwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Tanzania na shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na utalii limehudhuriwa na wajumbe zaidi ya [...]
15/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe wa Umoja wa Mataifa katika mpango wa amani wa Mashariki ya Kati, Robert Serry ameeleza kushtushwa kwake na ripoti kuwa walowezi wa kiisraeli wamekuwa wakishambulia mara kwa mara wakulima wa kipalestina katika Ukingo wa Magharibi wa mto Jordan na kuharibu miti ya mizeituni wakati huu wa msimu wa mavuno. Serry amesema kitendo hicho hakifai [...]
15/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakati dunia inaadhimisha mwaka wa tano wa kimataifa wa kunawa mikono kwa sabuni, Shirika la kuhudumia watoto duniani, UNICEF limesema kitendo hicho kinaweza kuokoa maisha ya maelfu ya watoto wanaokufa kila mwaka. Takwimu za mwezi uliopita za UNICEF kuhusu vifo vya watoto zinaonyesha kuwa watoto Elfu Mbili wenye umri wa chini ya miaka mitano walikufa [...]
15/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi mkuu wa shirika la kilimo na mazao la Umoja wa Mataifa FAO Jose Graziano da Silva amesema kuwa ikiwa mataifa yataweka jitihada zao katika kumaliza njaa lengo la maendeleo ya milenia la kupunguza kwa nusu idadi ya watu wenye njaa duniani ifikapo mwaka 2015 bado litatimizwa. Akizungumza wakati wa ufunguzi wa mkutano kuhusu usalama [...]
15/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la afya duniani, WHO limelaani vikali kitendo cha mashambulizi katika vituo vya afya nchini Syria na kueleza wasiwasi wake juu ya madhara ya mashambulizi hayo kwa wahudumu wa afya, wagonjwa na miundombinu ya afya. Taarifa ya WHO imesema kuwa mpaka sasa asilimia 67 ya hospitali za umma nchini humo zimeathiriwa na mgogoro huo na [...]
15/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi mkuu wa shirika la elimu, sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO Irina Bokova hii leo ameelezea wasi wasi wake kutokana na ghasia zinazoendelea nchini Syria hasa zile zinazolenga sehemu za kitamaduni nchini humo. Bokova pia anarejelea wito wake alioutoa tarehe 30 mwezi machi mwaka huu wa kuzitaka pande husika kulinda itikadi na [...]
12/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na UKIMWI, UNAIDS, limehimiza wajibu wa pamoja katika kukabiliana na upungufu wa ufadhili kwa mahitaji ya UKIMWI katika nchi zinazoongea lugha ya kifaransa. Ripoti mpya ya UNAIDS inaonyesha kwamba hatua zimepigwa katika nchi zinazoongea kifaransa, lakini bado kuna upungufu katika kuitikia tatizo la UKIMWI, na hivyo kutoa wito kwa [...]
12/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mgogoro wa Syria umekuwa ajenda ya mazungumzo kati ya mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Syria Lakhdar Brahimi na msimamizi wa misikiti miwili mitakatifu nchini Saudi Arabia, Mfalme Abdallah Bin Abdelaziz al Saud. Katika mazungumzo yao huko Jeddah, wawili hao wamekubaliana kuwa hali ya usalama nchini Syria inazorota siku hadi siku na kusababisha madhila [...]
12/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ameupongeza Umoja wa Ulaya, EU kwa kushinda tuzo ya amani ya Nobel kwa mwaka huu wa 2012 na kusema kuwa EU imekuwa ikizingatia misingi ya kuanzishwa kwake ambayo ni kujenga amani na umoja katika bara hilo lililosambaratishwa na vita kuu mbili za dunia. Katika taarifa yake, Ban [...]
12/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Jopo la wataalamu huru wa Umoja wa Mataifa wanaotetea haki za binadamu, uhuru wa kujieleza, elimu na kupinga mauaji , wameitaka serikali ya Pakistani kuhakikisha wanafunzi hususan wa kike wanalindwa na kwamba makundi yenye msimamo mkali hayazuii uwezo wa raia wa kawaida kutekeleza haki zao za kibinadamu. Wametoa kauli hiyo mjini Geneva, Uswisi kufuatia kitendo [...]
12/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi mkuu wa shirika la elimu Sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO Irina Bokova anatarajiwa kumuakilisha katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa kwenye mkutano wa 14 wa mataifa yanayozungumza lugha ya kifaransa mjini Kinshasa kwenye Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo ukiwa ndio mkutano wa kwa kwanza kuandaliwa eneo la Afrika ya kati. Akizungumzia [...]
12/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika hatua nyingine ofisi ya IOM nchini Afrika Kusini Jumatatu itakabidhi makazi mapya na yaliyokarabatiwa kwa ajili ya wahamiaji wavulana wanaosafiri wenyewe pamoja na wasichana walio katika mazingira hatarishi ikiwa ni sehemu ya mradi wa kuweka amani na mtangamano baina ya jamii zenye asili tofauti. IOM imesema makazi hayo huko Musina mpakani kwa Afrika Kusini [...]
12/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Maafisa wa shirika la Umoja wa Mataifa wanaohusika na uhamiaji IOM wataendesha mafunzo ya siku tatu kwa watendaji wanaoratibu ofisi zinazojihusisha na raia wa Ethiopia waliko nchi za ng'ambo. Mafunzo hayo yanayotazamiwa kuanza Oktoba 15 yanatazamiwa kuendeshwa mjini Addis Ababa yatakuwa na lengo la kuwajengea uwezo watendaji hao.Washiriki wa mafunzo hayo ni kutoka majimbo ya [...]
12/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa shirika la fedha duniani, IMF, Christine Lagarde, amesema mbali na kujikwamua kutoka kwenye mdororo wa uchumi uliopo sasa, siku za baadaye za uchumi wa kimataifa zitategemea ushirikiano zaidi na kurekebisha mfumo wa fedha. Bi Lagarde amesema hayo katika mikutano ya IMF na Benki ya dunia inayoendelea mjini Tokyo, Japan. Amesema kuwa ulimwengu una [...]
12/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakati duniani inaadhimisha siku ya kimatafa ya kupunguza madhara ya majanga duniani, shirika la kimataifa la wahamiaji, IOM limetangaza kuanza kwa mpango mkubwa barani Asia wa kusaidia jamii zilizo hatarini kujiandaa ili kupunguza athari za majanga pindi yanapotokea. Tayari shirika hilo limepokea dola Milioni 17 kwa kiasi kikubwa kutoka Marekani na Australia ambazo zitatumika kuzijengea [...]
12/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Huko Kusini mwa C, mafuriko yamelazimu Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, pamoja na washirika wake kuwahamishia maeneo yaliyo kwenye mwinuko wakimbizi wapatao Elfu Kumi na Saba kutoka kambi za Yaroungou na Moula. Mathalani katika kambi ya Yaroungou mafuriko yameharibu asilimia 85 ya mahindi na mpunga na hifadhi ya chakula na mbegu [...]
12/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Tume ya Umoja wa Mataifa kuhusu uchumi barani Ulaya, UNECE, imetoa wito kwa serikali za ulaya kufanya juhudi zaidi ili kuongeza usafiri wa maji, kwani ni njia inayolinda mazingira, ya kutegemewa, salama na gharama nafuu. Bara la Ulaya lina hadi kilomita 29, 000, za maji yanayoweza kuwa na mikondo ya usafiri, na bandari 400, lakini [...]
12/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mashirika ya Umoja wa Mataifa wanakusanya misaada ambayo itasaidia zaidi ya wakimbizi 340,000 wa Syria kukabiliana na msimu wa baridi unaokuja. Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR linasema kuwa wakimbizi walio nchini Jordan, Lebanon, Uturuki na Iraq watahitaji mahema, nguo za joto, mablanketi mazito, mafuta pamoja na chakula na maji. Melissa Fleming [...]
12/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Karibu watu milioni 5 wameathiriwa na mafuriko kwenye mikoa ya sindh, Punjab na Balochistan nchini Pakistan kwa mujibu wa shirika la kuratibu masuala ya kibinadamu OCHA. Mafuriko hayo yaliayoanza karibu mwezi mmoja uliopita yamesababisha zaidi ya ekari milioni moja ya ardhi ya kilimo kuzama na kuua karibu mifugo 10,000. OCHA inasema kuwa kutokana na kiasi [...]
12/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kimataifa la uhamiaji, IOM na serikali ya Zimbabwe wanazindua kituo kilichokarabatiwa cha kupokea wahamiaji wanaovuka mpaka wa Msumbiji kuingia nchini humo wakielekea Afrika Ksini kwa ajili ya kutafuta kazi na hifadhi ya kisiasa. Kituo hicho Nyamapanda kilichopo kilometa 300 Mashariki mwa mji mkuu wa Zimbabwe, Harare kitawezesha wahamiaji kupata huduma kama vile za [...]
12/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika mkutano wa 67 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa, suala moja ambalo liliorodheshwa katika masuala muhimu kujadiliwa lilikuwa saratani, au kansa ya wanawake. Mamilioni ya wanawake kote duniani huathiriwa na saratani ya aina moja au nyingine, mara nyingi zikiwa ni ile ya maziwa ya mama na ile ya mfuko wa uzazi. Akizungumza wakati [...]
12/10/2012 | Jamii: Makala za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa, Calin Georgescu amesifu hatua ya serikali ya Hungary ya kushughulikia madhara ya mtambo wa kiwanda cha chuma cha Ajka mwaka 2010 huku akitaka hatua zaidi zichukuliwe ikiwemo kurekebisha sera za uchafuzi wa mazingira ili kampuni zinazohusika na uchafuzi wa aina hiyo ziwajibishwe zaidi. Georgescu amesema hayo wakati wa ziara [...]
11/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Askofu Mkuu Desmond Tutu amesema haileti maana yoyote kuwaengua wanawake ambao ni zaidi ya asilimia 50 ya watu wote duniani huku akisema kuwa ni hivi karibuni tu ambapo wanawake wameanza kutambuliwa kuwa na uwezo na wanashika nyadhifa mbali mbali kwenye ofisi ikiwemo zile za kidini. Kauli hiyo ya Tutu ameitoa leo katika makao makuu ya [...]
11/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa Mfuko wa Fedha wa Kimataifa, IMF, Christina Lagarde, ametoa wito kwa viongozi duniani kukabiliana mara moja na hali ya hatari inayoendelea kuukabili uchumi wa kimataifa. Bi Lagarde amesema hatua za ushirikiano zinatakiwa kuchukuliwa na nchi zote wanachama wa IMF, wakati taasisi hiyo ikifungua mikutano yake ya kila mwaka. Mikutano ya Benki ya [...]
11/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon amesifu kitendo cha Nigeria na Cameroon cha kuheshimu uamuzi uliotolewa miaka Kumi sasa juu ya mgogoro wa mpaka baina yao kwenye rasi ya Bakassi. Taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Ban imemkariri Katibu huyo akisema kuwa kitendo cha kukubali uamuzi huo uliotolewa na mahakama ya kimataifa ya haki, [...]
11/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kongamano la 25 la Shirika la kimataifa la posta, UPU limefanyika Doha, Qatar kuanzia tarehe 7-11 Oktoba mwaka huu ambapo pamoja na mambo mengine nchi 192 wanachama wa shirika hilo waliangalia nafasi ya huduma za posta duniani kwenye maendeleo ya sasa ya teknolojia ya mawasiliano na kumulikia hasa anwani za makazi na utashi wa kisiasa [...]
11/10/2012 | Jamii: Mahojiano | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Watalaamu wa tajriba ya juu kutoka kwa baraza la haki za binadamu la Umoja wa Mataifa na tume ya Afrika ya kibinadamu na haki za watu wameahidi kuungana katika kupigania haki za binadamu barani Afrika. Akihutubia mkutano wa wawakilishi wa mataifa ya Afrika , mashirika ya umma waliokusanyika mjini Yamoussoukro nchini Ivory Cost mjumbe maalum [...]
11/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Rais wa Tume ya Ulaya José Manuel Barroso amekutana na Mkurugenzi mkuu wa shirika la kilimo na mazao la Umoja wa Mataifa FAO José Graziano da Silva mjini Brussels ambapo wawili hao walikubaliana kuwa Jumuiya ya Ulaya ndiyo mshirika mkuu wa FAO na hivyo ni lazima itekeleze wajibu wake kikamilifu. Wawili hao pia walizungumzia suala [...]
11/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Idadi ya watu wanaotumia simu za mkononi kote duniani imefikia bilioni sita, kwa mujibu wa Shirika la Kimataifa la Mawasiliano, ITU. Idadi hii, inamaanisha kuwa, kwa kila watu mia moja kote ulimwenguni, watu themanini na sita wana simu za mkononi. Shirika hilo la ITU linasema, zaidi ya watu bilioni 2.3, ambao ni zaidi ya thuluthi [...]
11/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nalo shirika la Umoja wa Mataifa la mawasiliano, ITU, pamoja na washirika wake linazindua tuzo ya aina yake kwa ajili ya kushawishi mtoto wa kike kupenda teknolojia na kuwa mbunifu kwa ajili ya maisha ya baadaye. ITU inasema asilimia 95 ya ajira zote zinahitaji fani ya teknolojia ya habari na mawasiliano na kwamba maisha ya [...]
11/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nayo mashirika ya Umoja wa Mataifa yanaadhimisha siku hii kwa kulimulikia suala la ndoa za wasichana wenye umri mdogo, ambazo hukiuka haki za binadamu na kuathiri vibaya mno nyanja zote za maisha ya mtoto wa kike. Shirika la Kuhudumia Watoto la UNICEF, limesema siku hii inaonyesha haja ya kuweka mahitaji ya mtoto wa kike kwenye [...]
11/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Balozi maalum wa anwani za makazi wa Umoja wa Mashirika ya posta duniani, UPU, Profesa Anna Tibaijuka, amesema kongamano la 25 la umoja huo limekubaliana kuwa huduma za posta zitaendelea kuwa na umuhimu mkubwa duniani licha ya maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano. Profesa Tibaijuka ameiambia Radio ya Umoja wa Mataifa kuwa katika kongamano hilo, utashi [...]
11/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ikiwa leo ni maadhimisho ya kwanza ya kimataifa ya siku ya mtoto wa kike, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ametaka serikali duniani kuchukua hatua kuwaepusha watoto wa kike na ndoa za umri mdogo. Katika taarifa yake, amesema ndoa za watoto hufanyika zaidi vijijini kwenye maskini na iwapo hali ya sasa itaendelea idadi [...]
11/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la afya duniani, WHO, limesema kuwa hadi sasa hakuna ushahidi kuwa kirusi kipya kinachosababisha uambukizo mkali kwenye njia ya hewa na kushindwa kufanya kazi kwa figo kinaweza kuambukizwa kutoka kwa binadamu mmoja kwenda kwa mwingine. Kauli hiyo ya WHO inakuja baada ya hapo mwezi uliopita mgojwa wa pili kubainika kuwa na kirusi hicho kiitwacho [...]
10/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, leo amelaani vikali shambulizi lililotekelezwa dhidi ya msichana mwenye umri wa miaka 14 ambaye amekuwa akipigania haki ya wasichana na wanawake nchini Pakistan kupata elimu, na kutaka walotekeleza kitendo hicho cha kikatili wafikishwe mara moja mbele ya vyombo vya sheria. Kwa mujibu wa vyombo vya habari, msichana [...]
10/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon amelaani vikali mashambulio ya kigaidi yaliyofanyika kwa wakati mmoja katika mji mkuu wa Syria, Damascus, yaliyosababisha vifo na majeruhi kadhaa na amerejelea msimamo wake wa kuzisihi pande zote husika kuingia katika meza ya majadiliano ili kupatia suluhu ya kisiasa ya mzozo huo. Taarifa iliyotolewa na msemaji wa [...]
10/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa umelazimika kuhamisha wafanyakazi wake kutoka jimbo la Kordofani Kusini nchini Sudan kufuatia mashambulizi ya hapa na pale kwenye mji wa Kadugli jimboni humo ambayo yanakwamisha juhudi za wafanyakazi hao za kutoa misaada kwa wanaohitaji. Wafanyakazi hao wamehamishiwa katika kituo cha kikosi cha muda cha Umoja wa Mataifa kwa ulinzi wa Abyei, UNIFSA [...]
10/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Karibu watu milioni 1.3 nchini Nigeria wamelazimika kuhama makwao huku wengine 431 wakiwa wameaga dunia kufuatia mafuriko ambayo yanatajwa na serikali kuwa mabaya zaidi kuwai kushuhudiwa kwa kipindi cha miaka 40 iliyopita. Kulingana na halmashauri ya kitaifa inayohusika na majanga ya dharura NEMA, Majimbo 30 kati ya majimbo 36 yameathiriwa tangu mwezi Julai. Kufuatia mvua [...]
10/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Hata baada ya kuwepo changamoto nyingi zikiwemo za uongozi na usalama nchini Afghanistan taifa hilo bado liko kwenye mkondo wa matumaini wa siku za baadaye, amesema mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa nchini humo. Akiongea kwenye mkutano wa waaandishi wa habari mjini Kabul Jan Kubis amezungumzia ziara ya juzi mjini New York ambapo alihutubia baraza [...]
10/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakati Brazil inajiandaa kuwa mwenyeji wa mashindano ya kombe la dunia mwaka 2014 na yale ya Olimpiki mwaka 2016, Shirika la Mpango wa Mazingira la Umoja wa Mataifa, UNEP, limetoa ripoti inayoonyesha ufanisi wa kulinda mazingira ulotokana na kombe la dunia Afrika Kusini mwaka 2010, na kile kinachoweza kuigwa kutokana nao ili uendelezwe kwenye michuano [...]
10/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, amesema usumbufu wa akili ni tatizo la kimataifa, katika ujumbe wake wa siku ya afya ya akili duniani, ambayo huadhimishwa kila Oktoba 10. Takriban watu milioni 350 wenye umri, vipato na uraia mbali mbali, wana usumbufu wa akili, na kwamba mamilioni ya wengine, ambao ni jamaa, marafiki [...]
10/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wawakilishi kutoka mataifa 23 ya Asia na Pacific leo wameanza mkutano wao wa siku tatu huko Bangkok, Thailand unaojadili ushirikiano katika ujenzi wa mtandao bora na wa uhakika wa barabara baina ya nchi hizo ambao utachochea ukuaji wa uchumi huku ukitoa fursa kwa wananchi wote kushiriki shughuli za kiuchumi na kijamii. Mkutano huo umeandaliwa na [...]
10/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO limesema hatua zozote za kudhibiti usalama katika mitandao ya kompyuta duniani zisitumike kuminya uhuru wa kujieleza kwa watumiaji wa mitandao hiyo. Hiyo ni kauli ya Mkurugenzi wa kitengo cha masuala ya uhuru wa kujieleza na maendeleo ya vyombo vya habari katika UNESCO, Guy Berger [...]
10/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkutano wa siku mbili wa mataifa Kumi na Nne ambayo ni visiwa katika bahari ya Pacific umemalizika huko Fiji kwa kutambua umuhimu wa nchi hizo kuunganisha sera zao za uchumi mkuu na zile za usalama wa nishati ili kuwa na maendeleo endelevu na kuepuka uchumi wao kutikiswa na athari za nje. Maafisa zaidi ya 50 [...]
10/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mojawepo pingamizi katika kutibu matatizo ya akili ni kwamba watu huwa hawajitambulishi na kutafuta msaada. Kauli hiyo imetolewa na Dr. Shekar Saxena kutoka Shirika la Afya Duniani, WHO, katika kuadhimisha siku ya afya ya akili duniani, leo tarehe kumi Oktoba. Dr. Saxena, ambaye ni mkurugenzi wa afya ya akili na matumizi mabaya ya dawa, amesema [...]
10/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu watoto na vita vya silaha, Leila Zerrougui, amelaani vikali shambulizi lililotekelezwa na watu wenye silaha kutoka kundi la Taliban dhidi ya wasichana wa shule kwenye bonde la Swat, kaskazini magharibi mwa Islamabad, nchini Pakistan. Msemaji wa kundi la Tehrik-i-Taliban Pakistan (TTP) amedai kuwa ni wao walitekeleza shambulizi hilo, [...]
09/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Waziri Mkuu wa zamani wa Italia, Romano Prodi ameteuliwa kuwa mjumbe maalum wa Katibu Mkuu uwa Umoja wa Mataifa huko Sahel, barani Afrika. Martin Nesirky ambaye ni msemaji wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, amesema Prodi ataongoza harakati za Umoja wa Mataifa na kimataifa katika kupatia suluhu matatizo yanayokumba watu wa eneo la Sahel [...]
09/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mahakama maalum ya Sierra Leone inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa imesema iko katika hatua za mwisho za kumaliza kesi yake ya mwisho ambayo ni ile inayomhusu Rais wa zamani wa Liberia, Charles Taylor. Rais wa mahakama hiyo Jaji Shireen Avis Fisher ametoa taarifa hizo leo mbele ya kikao cha Baraza la usalama la Umoja [...]
09/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kundi la wataalamu 35 wa afya, elimu na jamii limekuwa la kwanza kujiunga na kozi ya madhara ya vita kisaikolojia na kijamii iliyoanzishwa na shirika la kimataifa la Uhamiaji, IOM kwenye chuo kikuu cha Tripoli nchini Libya kwa msaada wa Italia. Kozi hiyo ya miezi sita itawapatia mafunzo wataalamu hao ambao watawasaidia watu waliopata madhara [...]
09/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ametangaza kuunga mkono mpango wa usitishaji miongo kadhaa ya mapigano baina ya kundi la waasi na vikosi vya serikali nchini Philippines. Serikali ya Philippnes imetiliana saini ya kuanzisha duru jipya la maelewano baina yake ya kundi la lijulikanalo the Moro Islamic Liberation Front (MILF) lenye ngome yake [...]
09/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakuu wa vitendo vya operesheni ya amani vya Umoja wa Mataifa ambao wamekutana huko Dakar Senegal kwa ajili ya kujadilia hali ya mambo katika eneo la afrika magharibi wamehimiza haja ya kuongeza mashirikiano kwa ajili ya kutanzua mkwamo unaolikumba eneo hilo. Wakuu hao walikutana kwa shabaha ya kupeana taarifa za namna ya kuboresha hali ya [...]
09/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kundi la wakimbizi wa Iraq wapatao 105 wakiwa na familia zao wamesafirishwa kwa ndege hii leo kuelekea nchini Ujerumani ambako wanatazamia kuanzisha maisha mapya katika eneo la Hanover. Wakimbizi hao ambao walikuwa wakiishi katika kambi mbalimbali ikiwemo zile za Kayseri, Bilecik walifuzu mahojiano yaliyoendeshwa na maafisa uhamiaji wa Ujerumani mapema mwezi July mwaka huu. Mjini [...]
09/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Pakistani kwa kushirikiana na UNICEF, WHO pamoja na ushirikiano wa kimataifa wa utoaji chanjo, GAVI imeanzisha chanjo mpya kwa ajili ya kuwakinga watoto dhidi ya ugonjwa wa Numonia, na hivyo kuwa nchi ya kwanza barani Asia kutoa chanjo hiyo. Nchini Pakistani zaidi ya watoto Laki Tatu na Nusu hufariki dunia kabla ya kutimiza umri wa [...]
09/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Ali Al-Za'tari, amelani mashambulizi ya mabomu yaliyofanywa hii leo kwenye mji mkuu wa jimbo la Kordofan Kusini Kadugli. Kulingana na ripoti mabomu yalianguka karibu na ofisi ya shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF , kwenye shule moja na pia kwenye kituo [...]
09/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wataalam wa Umoja wa Mataifa wamesema ikiwa asilimia 2 ya mapato ya ulimwengu mzima yangetumiwa kwa kuwapa watu maskini ulinzi wa kijamii, watu wote duniani wangeweza kufurahia haki hii ya msingi ya binadam. Mtaalam wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki ya kuwa na chakula, Olivier De Schutter, na yule anayehusika na umaskini wa kupindukia na [...]
09/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Watu sita wamefariki dunia na wengine kumi bado hawajulikani waliko baada ya boti waliyokuwa wakisafiria kuzama mapema Jumatatu karibu na kisiwa cha Mayotte kilicho chini ya himaya ya Ufaransa. Hii ni ajali ya pili ya aina hiyo katika kipindi cha mwezi mmoja na inahusisha wakimbizi na wahamiaji haramu wanaotafuta maisha bora kwenye kisiwa cha Mayotte [...]
09/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa Umoja wa Mashirika ya posta duniani, UPU, Edouard Dayan amesema huduma za posta hazijadorora katika zama hizi za maendeleo ya teknolojia ya mawasiliano ya simu za mkononi na intaneti, bali zinajiendeleza na kutekeleza majukumu yake. Katika salamu zake hii leo ambapo ni siku ya posta duniani huku wadau wakikutana huko Doha, Qatar [...]
09/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Msaidizi wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya haki za binadamu, Ivan Simonovic amehitimisha ziara yake ya siku nne nchini Mali na kusema kuwa vitendo vya ukiukwaji wa haki za binadamu kaskazini mwa nchi hiyo vinaendelea ijapokuwa mwenendo na mazingira yake yamebadilika tangu kuanza kwa mgogoro kwenye eneo hilo. Ametoa mfano kuwa [...]
09/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, amekutana na Rais Francois Hollande wa Ufaransa mjini Paris na kujadili kuhusu mizozo inayoendelea nchini Syria na katika eneo la Sahel. Kuhusu mzozo wa Syria, Bwana Ban amerejelea wito wake wa kukomesha ghasia na kupatia silaha vikundi vinavyozozana, pamoja na kufanya maandalizi ya serikali ya mpito, yakiendeshwa [...]
09/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Huku siku ya kimataifa ya afya ya akili ikiaadhimishwa tarehe kumi mwezi huu shirika la afya duniani linatoa wito wa kumwalizwa kwa unyanyapaa na usumbufu wa akili ana kutaka kuwepo matibabu kwa watu wote wanaoyahitaji. Duniani kote zaidi ya watu milioni 350 wamedhoofika kiakili hali inayowazuia kufanya mambo yao kwa njia inayohitajika. Lakini kutokana na [...]
09/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Karibu watu milioni 870 wamekuwa wakisumbuliwa na hali mbaya ya utapia mlo kati ya mwaka 2010 na 2012 kwa mujibu wa ripoti mpya kuhusu njaa iliyotolewa hii leo. Ripoti hiyo yenye kichwa "Hali ya usalama wa chakula duniani mwaka 2012" (SOFI) ilichapishwa na mashirika ya Umoja wa Mataifa yakiwemo shirika la chakula duniani FAO, mfuko [...]
09/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »

Mkutano mkuu wa 25 wa Umoja wa posta duniani, UPU, umeanza leo uko Doha, Qatar ambapo balozi maalum wa UPU kuhusiana na anwani za makazi, Profesa Anna Tibaijuka amesema watu wasiokuwa na anwani wametengwa na wanashindwa kushiriki katika shughuli za maendeleo. Akizungumza katika mjadala kwenye mkutano huo wa siku tano unaoangalia hatma ya posta, Profesa Tibaijuka amesema uhaba wa [...]
08/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Taifa la Norway limetangaza kuwa litatoa jumla ya dola milioni 20 kufadhili miradi ya shirika la elimu , Sayansi na utamaduni la Umoja wa Mataifa UNESCO ikiwa ni sehemu ya kuzipa kipaumbele programu za elimu na masuala ya kitamaduni na uhuru wa kujieleza. Makubaliano ya ushirikiano huo yatatiwa sahihi na Waziri wa maendeleo ya kitaifa [...]
08/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mtaalamu maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za wahamiaji Francois Crépeau, amehitimisha ziara yake ya siku tisa huko Italia na kutaka sera za nchi hiyo za kudhibiti wahamiaji haramu zizingatie haki za binadamu. Ametoa mapendekezo Sita ya kuzingatiwa wakati wa kushughulikia wahamiaji haramu kwenye mipaka ya nje ya nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya, [...]
08/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia watoto, UNICEF limepata zaidi ya Euro Milioni Nne na Nusu kutoka Umoja wa Ulaya kwa ajili ya mradi wake wa dharura wa elimu kwa watoto wa Syria wanaoishi ukimbizini nchini Jordan pamoja na watoto wa jamii zinazotoa hifadhi. Msaada huo wa hivi karibuni unafanya mchango wa EU kufikia [...]
08/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Zaidi ya miongo miwili tangu Namibia ilipojipatia uhuru, bado taifa hilo linaendelea kuzingirwa na viwango visivyokubalika vya kutokuwepo usawa kwenye misingi ya jinsia, kabila, kikanda pamoja na tabaka, ameonya mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu umaskini uliopindukia na haki za binadamu, Magdalena Sepulveda. Akiongea baada ya kukamilisha ziara yake nchini Namibia Sepulveda amesema [...]
08/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Somalia amempongeza waziri mkuu wa nchi hiyo Abdi Farah Shirdon na kumshauri aweze kubuni serikali iliyo ya kuwajibika na yenye uwazi. Balozi Agustine Mahiga amesema kuwa uteuzi wa Waziri mkuu mpya ni hatua nyingine nchini humo kwenye mpango wa amani. Uteuzi huo wa Waziri mkuu mkuu utapelekwa bungeni [...]
08/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi wa kipalestina UNRWA limezinfdua programu mbili mpya kwenye kituo chake cha elimu ya sayansi eneo la Naour magharibi mwa Amman kama sehemu ya mikakakati yake ya kuyafanyia mabadiliko masuala ya elimu. Kwenye taarifa iliyotolewa hii leo UNRWA imesema kuwa programu hizo mbili zilizozinduliwa wakati wa maadhimisho ya [...]
08/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Sera za kuwafanya watu wastaafu mapema hazijasaidia kuongeza nafasi za ajira kwa vijana, limesema shirika la kazi duniani, ILO. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa ILO kuhusu ajira, José Manuel Salazar, mchango wa watu wazee ni mkubwa katika mazingira ya kazi kama ulivyo wa vijana. ILO imesema kuwa nchi zenye uchumi ulioendelea zinakabiliwa na changamoto mbili [...]
08/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni, UNESCO na Umoja wa Ulaya EU, zimeingia makubaliano mapya ya kubadilishana taarifa na kuimarisha ushirikiano wako katika nyanja za elimu, utamaduni, Sayansi na haki za binadamu. Makubaliano yametiwa saini kati ya Mkuu wa UNESCO Irina Bokova, Makamu Rais wa EU Catherine Ashton na kamishna wa [...]
08/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Naye mshindi wa tuzo ya amani ya Nobel mwaka huu, Tawakkol Karman, ameanzisha mbiu ya huruma kwa ajili ya Syria wakati wa kongamano hilo la demokrasia mjini Strasbourg, Ufaransa. Bi Karman ambaye ni mwandishi wa habari kutoka Yemen ameelezea pia kuvunjwa moyo na mateso wanayopitia wanadamu. Akizungumza wakati wa kufungua kongamano hilo, mshindi huyo wa [...]
08/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, ametoa wito kwa serikali kote duniani ziwasikilize raia, wakati wa hotuba yake kwenye kongamano la kimataifa kuhusu demokrasia, ambalo linaendelea mjini Strasbourg, Ufaransa. Kongamano hilo linalomalizika tarehe 11 Oktoba, limewaleta pamoja wataalam wa marekebisho na viongozi wa kimataifa ili kutambua jinsi ya kuitikia changamoto zinazoukabili ulimwengu kwa [...]
08/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kwa mara ya kwanza Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR limetoa mwongozo utakaosaidia kuwatambua na kuwasaidia wanaume waliokumbwa na visa vya kubakwa au manyanyaso ya kingono katika mazingira ya migogoro na ukimbizi. Mwongozo huo ulioandaliwa na kitengo cha usalama wa kimataifa cha UNHCR utatumiwa na wafanyakazi wa shirika hilo na wale wa [...]
08/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Tume ya haki za bindamu ya Umoja wa Mataifa wa haki za binadamu, leo imetoa ripoti ya aina yake inayoelezea bayana vitendo vya ukiukwaji wa sheria ya kimataifa wakati wa kipindi miaka kumi ya mgogoro nchini Nepal kuanzia mwaka 1996 hadi 2006. Katika utangulizi wake kwenye ripoti hiyo ya kurasa 233, Mkuu wa tume hiyo [...]
08/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ameonya kuwa mgogoro wa Syria unazidi kuongezeka na unaweza kuwa tishio kwa nchi jirani za ghuba na hata eneo lote. Akifungua mkutano wa jukwaa la kimataifa la demokrasia lilioandaliwa na Baraza la Ulaya huko Strasbourg Ufaransa, Ban amesema ongezeko la uhasama katika mpaka wa Syria na Uturuki [...]
08/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »

Wanachama wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa, leo wamelaani vikali mashambulizi ya kigaidi ambayo yalitekelezwa siku ya Jumatano katika mji wa Aleppo nchini Syria, ambayo yalisababisha vifo kadhaa na kuwajeruhi mamia ya watu. Wameelezea huzuni wao na kutoa ujumbe wa rambirambi kwa jamaa za waathiriwa wa vitendo hivyo vya kikatili. Katika taarifa kwa [...]
05/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la nishati ya atomiki, IAEA limesema Belarus imepiga hatua kubwa katika kuandaa miundombinu ya nyuklia na kuongeza kuwa iwapo itaendelea hivyo basi itaweza kujenga mtambo wa nyuklia siku za usoni. Hayo yamo katika ripoti ya shirika hilo ambayo Naibu Mkurugenzi Mkuu wake Alexander Bychkov ameikabidhi kwa Naibu Waziri Mkuu wa [...]
05/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Dubu, papa na miti migumu ya Madagascar ni mojawepo wa aina za wanyama kadhaa na mimea ambazo zimepenedekezwa kuongezwa kwenye orodha ya viumbe vinavyolindwa chini ya mktaba wa kimataifa kuhusu biashara katika viumbe walio katika hatari ya kuangamizwa, CITES. Zaidi ya nchi 50 zimewasilisha mapendekezo 67 kwa sekritariati ya CITES, ili sheria zinasodhibiti biashara katika [...]
05/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Mungano wa Ulaya linalohusika na msaada kwa kibinadam (ECHO) leo limetangaza msaada wake wa millioni kumi na moja kwa Shirika la Umoja wa Mataifa wa linalowasaidia wakimbizi wa Palestina (UNRWA). Msaada huo utasaida shirika la UNRWA kufanya katika shughuli zake nchini Syria, Lebanon naPalestina. Mkuu wa UNRWA, Bwana Filippo Grandi, amesema Mungano wa [...]
05/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayojihusisha na haki za binadamu imeelezea kushishtushwa kwake kutokana na ongezeko la mauwaji ya watu nchini Guetemala na tukio la hivi karibuni la kuuliwa kwa wakulima. Ripoti zinasema kuwa vurugu zilizotokea hapo alhamisi baina ya wakulima wazawa na makundi ya polisi na askari katika eneo la Magharibi mwa Guetamala, imesababisha [...]
05/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna Mkuu wa haki za binadamu Navi Pillay amelaani na kushurtumu uamuzi iliochukuliwa na bunge la Ukraine ya kuweka kusudio la kupitisga sheria ambayo inapiga marafuku vitendo vya ushoga. Mswaada huo wenye nambari 8711 kama utapitishwa na kuwa sheria utawatia hatiana wahusika wa vitendo vya ushoga vinavyofanywa hadharani kutozwa faini ama kifungo cha hadi miaka [...]
05/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kundi la wataalam huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu umaskini ulokithiri, madeni ya kitaifa na utaratibu wa usawa, limezikumbusha serikali za Muungano wa Ulaya kwamba marekebisho ya kiuchumi ni lazima yaende sambamba na wajibu wa serikali wa kulinda haki za binadamu. Hii ni kufuatia ripoti ya utafiti uliofanywa kuhusu sekta ya benki katika mataifa yote [...]
05/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Walimu milioni 1.7 zaidi wanahitajika ili kuwezesha kufikia lengo la milenia la elimu ya msingi kwa wote ifikapo mwaka 2015. Hayo ni kwa mujibu wa mashirika ya Umoja wa Mataifa, katika kuadhimisha Siku ya Walimu Duniani leo Oktoba 5. Katika ujumbe wake wa kuadhimisha siku hii, Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni, [...]
05/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchini Myanmar, idadi ya watu wanaokimbia makazi yao kwa ajili ya kutafuta chakula, huduma za afya, makazi na misaada mingine inazidi kuongezeka ikiwa ni miezi minne tangu kutokea kwa vurugu baina ya jamii tofauti kwenye jimbo la Rakhine, magharibi mwa nchi hiyo. Takwimu zilizotolewa na mamlaka katika eneo hilo zimeonyesha kuwa hivi sasa kuna watu [...]
05/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kimataifa la uhamiaji, IOM mwezi huu litazindua mradi wa miezi mitatu wenye lengo la kujenga na kuimarisha amani kwenye jumuiya za watu wanaotoka jamii tofauti nchini Afrika Kusini. IOM imepata msaada kutoka benki ya maendeleo kusini mwa Afrika, DBSA na shirika la maendeleo ya viwanda IDC na mradi utatekelezwa kwenye jimbo la Western [...]
05/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi, UNHCR, Antonio Guterres amerejelea wito wake wa kutaka nchi ziache mipaka yao wazi kwa ajili ya kupokea watu wanaokimbia migogoro na majanga mbali mbali duniani kote. Akizungumza na waandishi wa habari leo mjini Geneva , Uswisi, Guterres amesema UNHCR hivi sasa imezidiwa uwezo wa kuwapatia [...]
05/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la uhamiaji la kimataifa, IOM limeripoti kuwa zaidi ya wafanyakazi wahamiaji Elfu Sita nchini Syria wameomba kuondolewa nchini humo. Afisa wa IOM, amesema wafanyakazi hao wanatoka zaidi ya nchi 23 ikiwemo Indonesia, Ufilipino, Sudan Kusini, Ethiopia, India na Bangladesh. Mpaka sasa shirika hilo limeshasaidia wafanyakazi Elfu Mbili waliohitaji msaada kuondoka nchini Syria lakini mpango [...]
05/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la Usalama limelaani vikali shambulizi la makombora lililofanywa na wanajeshi wa Syria kwenye mji wa Akcakale, na ambalo liliwaua watu watano na kuwajeruhi wengine kadhaa. Zaidi ya watu 18, 000, hususan raia, wameuawa nchini Syria tangu migogoro baina ya serikali ya rais Bashar al-Assad na makundi ya upinzani ilipoanza, huku wengine milioni 2.5 wakiwa [...]
05/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakati kunapotokea mizozo au vita kuna athari ambazo hujitokeza zikiwemo za kuhama kwa watu, uporaji wa mali , mauaji , utekaji nyara na kadhalika. Lakini kuna athari moja ambayo kwa sasa inatajwa kuwa moja ya zana za kivita, na athari hiyo ni ubakaji au dhuluma za kimapenzi hasa kwa wanawake na watoto wasichana. Katika mjadala [...]
05/10/2012 | Jamii: Makala za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon ameipongeza Msumbiji kwa kusherehekea miaka 20 tangu kutiwa saini kwa makubaliano ya amani ya mwaka 1992 yaliyomaliza vita vya wenyewe kwa wenye vilivyoibuka mara baada ya kupata uhuru mwaka 1975. Msemaji wa Ban amemkariri Katibu Mkuu huyo wa Umoja wa Mataifa akisisitiza kuwa ofisi yake itaendeleza ushirikiano [...]
04/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-Moon ameonya uwezekano wa mgogoro wa Syria kusambaa katika maeneo jirani kutokana na ongezeko la wasiwasi wa hali ya usalama katika mpaka wa nchi hiyo na Uturuki. Onyo hilo la Ban linafuatia shambulio la makombora kutoka Syria siku ya Jumatano dhidi ya mji mmoja nchini Uturuki, lililofuatiwa na [...]
04/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »

Shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR limesema uhaba wa makazi utaendelea kuwa tatizo kubwa kwa sasa na baadaye kwa wakimbizi wa Syria nchini Lebanon. Afisa wa UNHCR anayehusika na hifadhi ya wakimbizi hao Anna Leer akizungumza mjini Tripoli, Libya amesema yeye na watendaji wengine wamebaini kuwa wakimbizi hao wamesambaa maeneo mbali mbali [...]
04/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »

Zaidi ya familia 50,000 nchini Colombia zinatazamiwa kunufaika na mpango mpya unaoendwa na Umoja wa Mataifa wenye shabaha ya kukabiliana na hali ya umaskini katika maeneo ya vijijni. Chini ya mpango huo familia hizo zinatazamiwa kufikiwa na misaada ya kifedha ili hatimaye ziendesha miradi ya ujasiliamali ambao unaelezwa unasaidia kuwavusha kutoka daraja la chini hadi [...]
04/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amemteua Bwana David Malone raia wa Canada kuwa mwangalizi wa chuo kikuu cha Umoja wa Mataifa, kufuatia majadiliano aliyofanya na Mkurugenzi Mkuu wa UNESCO Irina Bokova. Bwana Malone anatazamiwa kuwa mkuu wa sita wa chuo hicho ambacho kinawaleta pamoja wasomi kutoka sehemu mbalimbali dunia wanaotumika kama chachu [...]
04/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa umesema kuwa umefurahishwa na taarifa iliyotolewa hadharani na serikali ya Afghanistan iliyosema kuwa siyo kosa la. jinai kwa mwanamke ama mtoto wa kike kukimbia kutoka eneo lake hasa pale anapoandamwa na jambo ambalo linaweza kudhuru afya yake. Hivi karibuni mawaziri kadhaa walitoa tamko la kulaani vikali tukio la kutiwa mbaroni wanawake na [...]
04/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu Somalia, Augustine Mahiga, amesema nchi ya Somalia tayari imeanza kushuhudia mabadiliko muhimu, kufuatia kuundwa kwa bunge na uchaguzi wa rais hivi karibuni, ambao amesema ulikuwa mojawapo wa kidemokrasia zaidi barani Afrika. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Nairobi, Bwana Mahiga amesema hali ya usalama katika mji mkuu [...]
04/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Urusi imetoa mfano wa chombo cha satelaiti kwa Umoja wa Mataifa, ambacho kitawekwa hadharani kwenye sehemu ya maonyesho ya vyombo vya safari za anga za juu katika ofisi za Umoja wa Mataifa mjini Vienna, Austria. Chombo hicho kimewasilishwa na Naibu Mkuu wa shirika la safari za angani la Urusi, Roscosmos, na kushuhudiwa na mkuu wa [...]
04/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ripoti ya Benki ya dunia iliyotolewa hivi karibuni imebashiri kukua kwa uchumi wa nchi za Afrika zilizo kusini mwa jangwa la Sahara kwa asilimia 4.8 mwaka huu wa 2012 licha ya kudorora kwa uchumi wa dunia. Ripoti hiyo itolewayo mara mbili kwa mwaka baada ya kuchunguza masuala yanayotoa mwenendo wa uchumi wa Afrika imesema kiwango [...]
04/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kundi la wataalam huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu biashara na haki za binadamu, watafanya ziara nchini Mongolia kati ya Oktoba 8 na 18, ili kuchunguza athari za shughuli za biashara dhidi ya haki za binadam nchini humo. Mmoja wa wataalam hao, Margaret Jungk, amesema Mongolia ni mojawapo wa uchumi unaokuwa kwa viwango vya haraka [...]
04/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Bei ya chakula duniani ilipanda kwa asilimia 1.4 mnamo mwezi Septemba, limesema Shirika la Chakula na Kilimo, FAO. Shirika hilo la FAO limesema kuwa kiwango hicho kipya, ambacho ni ongezeko la pointi 3, kimefikiwa baada ya miezi miwili ya kutobadilika, kwa sababu ya kuimarika kwa bei ya bidhaa za maziwa na nyama. Kiwango hicho cha [...]
04/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna wa Tume ya Haki za binadamu ya Umoja wa Mataifa, Navi Pillay ameelezea kusikitishwa kwake na hatua ya Serbia ya kupiga marufuku mikutano ya hadhara iliyopangwa kufanyika Jumamosi na badala yake ameitaka serikali hiyo kufanikisha mikutano hiyo ikiwemo ule wa kujitambua wa wapenzi wa jinsia moja na watu waliobadili jinsi zao ili waweze kutekeleza [...]
04/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Zaidi ya watu Milioni 50 katika nchi saba za Afrika watapatiwa chanjo ya homa ya uti wa mgongo katika kipindi cha miezi mitatu ijayo, ikiwa ni kampeni ya pamoja inayohusisha ushirikiano wa kimataifa wa utoaji chanjo, Gavi, shirika la afya duniani, WHO, shirika la kuhudumia watoto wa la Umoja wa Mataifa, Unicef na mradi wa [...]
04/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limelaani vikali mauaji ya walinda amani wa ujumbe wa Umoja wa Mataifa Darfur, UNAMID, ambayo yalitekelezwa tarehe mbili Oktoba jioni na watu wasojulikana. Wanajeshi wanne waliuawa katika shambulizi hilo dhidi ya askari walinda doria kutoka Nigeria katika eneo la El Geneina magharibi mwa Darfur, huku wengine wanane wakijeruhiwa. [...]
04/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon amezungumza kwa njia ya simu na Waziri wa Mambo ya Nje wa Uturuki Ahmet Daoud Oglo na kumpa pole kutokana na shambulio la kombora leo alfajiri lililoua watu sita na majeruhi tisa. Inadaiwa kuwa kombora hilo lilirushwa kutoka Syria na kutua jimbo la Sanliurfa ambapo msemaji [...]
03/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ongezeko la hivi karibuni la wakimbizi huko Afrika na Mashariki ya Kati kutokana na sababu mbali mbali ikiwemo migogoro ya kisiasa limesababisha shirika la Umoja wa Mataifa la kuhudumia wakimbizi UNHCR kuyataka mataifa ulimwenguni kuwa na utashi wa kisiasa zaidi kuhudumia watu hao wenye mahitaji. Afisa mwandamizi wa UNHCR Erika Feller akizungumza katika kikao cha [...]
03/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mjumbe maalum wa Umoja wa Mataifa nchini Haiti, Mariano Fernandez leo amelieleza Baraza la Usalama la Umoja huo kuhusu mashauriano yanayoendelea na serikali ya Haiti juu ya mpango wa kuimarisha na kupanga upya shughuli za ujumbe wa kimataifa wa kurejesha utulivu nchini Haiti, MINUSTAH. Bwana Fernandez, akihutubia kikao cha Baraza la Usalama la Umoja wa [...]
03/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa umelitaka shirika la posta duniani kupanua huduma zake ili kuwafikia wateja wengi zaidi wanakuwa na ukosefu wa huduma za kifedha. Wito huo umetolewa katika chapisho jipya lililotolewa na Umoja wa shirika la posta duniani UPU. Ripoti hiyo imesema wakati dunia ikiendelea kushuhudia mabadiliko makubwa, lakini bado kuna idadi kubwa ya wananchi ambao [...]
03/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Zaidi ya mataifa 40 yanaripotiwa kupiga hatua kwa kuidhinisha ama kusaini mikataba mbalimbali ya kimataifa ikiwemo ukiwemo ule unaohusu ulinzi kwa watoto dhidi ya vitendo vya unyanyasaji na mateso mengine. Hayo yameelezwa kufikiwa wakati wa kikao cha baraza la Umoja wa Mataifa kilichofanyika New York na kuhudhuria na viongozi wa mataifa mbalimbali wanachama. Akijadilia kwa [...]
03/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Zimbabwe iko katika mwelekeo mzuri kufikia utimilifu wa utoaji huduma za matibabu kwa wagonjwa wa virusi vya UKIMWI pamoja na wale wanaougua kifua kikuu. Hatua hiyo inafuatia msaada wa fedha kutoka fuko la kimataifa la Global Fund iliyotoasi kiasi cha doka za kimarekani milioni 84. Pamoja na mambo mengine fedha hizo zinatazamia kufanikisha mpango wa [...]
03/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa kitengo cha wanawake kwenye Umoja wa Mataifa, UN Women, Michelle Bachelet, amesema kuwa taifa la India linafaa kutekeleza sheria ilizo nazo ili kulinda haki za wanawake. Bi Bachelet amesema hayo mbele ya ziara yake nchini India, ambayo amesema itaangazia kuchagiza juhudi za kuendeleza usawa wa kijinsia na kuwapa wanawake uwezo kwenye [...]
03/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baada ya hali ya kibinadamu kuendelea kuwa mbaya nchini Yemen shirika la mpango wa chakula duniani WFP limekuwa likipanua programu za kusaidia wanaotaabika. Mwanzo wa mwaka huu WFP ilipanga kusambaza misaada kwa watu milioni 1.2 . Mwezi Mei idadi hiyo ikaongezeka hadi watu milioni 1.8. Mwezi Septemba ikaongeza tena kwa watu milioni mbili hadi watu [...]
03/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kazi duniani ILO limesema kuwa ajira kwa vijana linabaki kuwa changamoto kuu wakati vijana milioni 17.7 wakiwa hawana ajira au zaidi ya asilimia 16 kwenye nchi 17 kati ya nchi zilizostawi na zinazoinukia kiuchumi za G20 wakiwa hawana kazi. Kulingana na takwimu zilizowasilishwa kwenye mkutano wa kundi la nchi za G20 mjini Geneva [...]
03/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, ameelezea huzuni na mshangao wake kufuatia mauaji ya walinda amani wa Umoja wa Mataifa yalotokea Jumanne jioni katika jimbo la Darfur, magharibi mwa Sudan. Watu wasojulikana waliwaua wanajeshi wanne, na kuwajeruhi wengine wanane baada ya kuuvizia msafara wa askari wa Nigeria walinda doria, katika eneo la El [...]
03/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Hali mbaya ya uchumi imedhoofisha kwa kiasi kikubwa mazingira ya walimu kufanya kazi na hata mishahara yao . Hiyo ni kauli ya Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kazi duniani, ILO, Guy Ryder katika taarifa yake aliyoitoa kuelekea siku ya walimu duniani tarehe Tano mwezi huu. Ryder amesema uhaba wa walimu umesababisha msongamano wa wanafunzi katika [...]
03/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ikiwa imesalia miaka mitatu na miezi mitatu tu kabla ya tarehe ya kufikia malengo ya maendeleo ya milenia, bado kuna kazi nyingi ambayo inahitajika kufanywa. Hayo ni kwaa mujibu wa naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Jan Eliasson, wakati akizungumza na waandishi wa habari kuhusu mkutano wa 67 wa Baraza Kuu, ambao umehitimishwa wiki [...]
03/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ikiwa ni takribani mwezi Mmoja na Nusu umebakia kabla Sierra Leone haijafanya uchaguzi mkuu wa Rais, wabunge na madiwani, Umoja wa Mataifa kupitia Tume ya kujenga amani imepongeza maendeleo thabiti ya maelewano nchini humo na kusisitiza umuhimu wa uongozi wa kitaifa na msaada wa kimataifa ili kuepusha vitisho vyovyote vinavyoweza kurejesha mzozo nchini humo. Taarifa [...]
03/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ikiwa imesalia miaka Mitatu kufikia ukomo wa malengo ya Milenia yaliyopitishwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani mwaka 2000, Tanzania imeelezwa kuwa imechukua hatua thabiti kutekeleza malengo ya kuboresha afya ya wajawazito pamoja na kupuunguza vifo vya watoto wachanga. Taarifa hizo za kutia moyo zilitangazwa kwenye makao makuu ya Umoja [...]
02/10/2012 | Jamii: Mahojiano | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Tanzania imeripotiwa kupunguza idadi ya vifo vya wajawazito na kufikia idadi ya chini zaidi katika nchi za Afrika zilizo kusini mwa jangwa la Sahara, na hiyo ni kutokana na utekelezaji wa miradi ya ushirikiano kati ya serikali na sekta binafsi. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki Moon amesema hayo leo jijini New York [...]
02/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Jan Eliasson, amesema mjadala wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mwaka huu umedhihirisha tena umuhimu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya diplomasia, katika kuweka kanuni za kimataifa na katika kuleta pamoja nguvu za ushirikiano katika maendeleo. Akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari leo, Bwana Eliasson [...]
02/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa Mataifa kupitia shirika lake la chakula na Kilimo, FAO leo limemtunuku Waziri Mkuu wa China, Wen Jiabao leo tuzo ya juu ya Umoja huo kutokana na mchango wake wa kuongeza uzalishaji wa chakula na hivyo kusaidia kupunguza idadi ya watu mafukara duniani. Akikabidhi tuzo hiyo mjini Beijing, China, Mkurugenzi Mkuu wa FAO Jose [...]
02/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Vuk Jeremic, amezungumzia kile alichokiita nguvu za Umoja wa Mataifa akisema kuwa zitadhihirika iwapo tu nchi wanachama zitaamua hivyo Akizungumza wakati wa kufunga mjadala uliowahusisha maafisa wa ngazi za juu, rais Vuk alizitolea mwito nchi wanachama kufanya kazi kwa pamoja ili kuupa nguvu Umoja huo wa Mataifa. [...]
02/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Waziri wa mashauri ya kigeni wa Mauritius Dr. Arvin Boolell amesema kuwa ili dunia ifaulu kukabiliana na mikwamo ya kiuchumi inapaswa kuweka uratibu ambao utaziwezesha taasisi za Umoja wa Mataifa kuwa na uwezo wa kukabiliana na changamoto za kiuchumi wa dunia. Waziri huyo ambaye alikuwa akizungumza kwenye baraza kuu la Umoja wa Mataifa amesema kuwa [...]
02/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Licha ya kwamba vifaa vya msaada vimeanza kuwasili kwenye maeneo yaliyokumbwa na mafuriko nchini PAKISTANI, Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM limeonya kuwa msaada zaidi unahitajika ili kukidhi mahitaji yaliyobainishwa na ofisi ya majanga nchini humo. Maria Moita kutoka IOM ambayo inaratibu usambazaji wa misaada kwa waathirika wa mafuriko, amesema shughuli za usaidizi zinakwamishwa na [...]
02/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Umoja wa mabunge duniani, IPU umeshutumu mauaji ya leo ya mbunge wa chama cha Progressive Party of Maldives, PPM nchini Maldives Afrasheem Ali. Mauaji hayo ya punde zaidi na ya kwanza kwa mbunge yameelezwa kuwa ni ya kutisha katika mfululuzo wa ghasia zilizokumba visiwa hivyo tangu kuanza kwa mzozo wa kisiasa mapema mwaka huu huu. [...]
02/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Idadi ya raia wa Syria walioandikishwa au wanaosubiri kuandikishwa kama wakimbizi nchini Jordan , Lebanon, Uturuki na Iraq sasa imepita watu 300,000 ikiwa ni mara tatu zaidi ya idadi iliyoandikishwa miezi mitatu iliyopita. Takwimu za hivi majuzi zinaonyesha kuwepo kwa wakimbizi 311,500 kutoka Syria kwenye nchi hizo nne ikilinganishwa na wakimbizi 100,000 walioandikishwa mwezi Juni. [...]
02/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la UNHCR limesema kuwa limewasaidia zaidi ya raia 25,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo kurudi makwao kaskazini mwa nchi kutoka nchi jirani ya Congo kupitia mpango wa kuwarejesha nyumbani kwa hiari uliozinduliwa mwezi Mei. UNHCR inasema inamatumaini ya kuwarejesha nyumbani wakimbizi 24,000 wengi kutoka mkoa wa Equateur ifikapo mwishoni mwa mwaka huu na [...]
02/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Zaidi ya wahamiaji 1000 kutoka nchi zilizo kusini mwa jangwa la sahara kwa sasa ambao wamekwama nchini Morocco watasafirishwa kwenda nchi zao kupitia kwa mpango unaotarajiwa kuongozwa na shirika la kimataifa la uhamiaji IOM. IOM inasema kuwa wahamiaji hao wengi kutoka Cameroon , Nigeria, Senegal na Ivory Coast huunda walisafirishwa kiharamu kwenda Morocco kwa minajili [...]
02/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kamishna Mkuu wa Shirika la Kuhudumia Wakimbizi la Umoja wa Mataifa, Antonio Guterres, ameyapongeza mataifa ya Ecuador, Honduras na Ureno kwa kujiunga kwenye mtandao wa mataifa ambayo yamechukua hatua za kukabiliana na suala la ukosefu wa uraia. Mataifa yote hayo matatu yaliusaini mkataba wa kuwatambua watu wasio na uraia wa taifa lolote katika hafla maalum [...]
02/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia haki za binadamu imeonyesha wasiwai juu ya hali ya kuendelea kutiwa matatani kwa watetezi mashuhuri wa haki za bindamu, waandishi wa habari na hata wanaharakati wa kisaisa nchini Iran na kueleza kuwa kitendo hicho ni ukandamizaji wa sauti za umma.. Afisa kutoka ofisi hiyo Rupert Colville amesema vitendo vya [...]
02/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Serikali ya Botswana imeutaka Umoja wa Afrika kuendelea na msimamo wake wa kupinga mapinduzi ya kijeshi yanayoondoa serikali madarakani kinyume cha katiba. Waziri wa Mambo ya Nje wa Botswana Phandu Skelemani akihutubia Jumatatu ambayo ni siku ya mwisho ya mjadala wa wazi wa mkutano wa 67 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New [...]
02/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Waziri wa mambo ya nje wa Tanzania, Mwana Bernard Kamillius Membe, amezungumza kwa kirefu kuhusu desturi ya kusuluhisha mizozo kwa njia ya amani kwenye hotuba aliyoisoma kwenye mkutano wa 67 wa Baraza Kuu la UMoja wa Mataifa, ambako alimwakilisha Rais Jakaya Mrisho Kikwete. Baada ya hotuba yake, Redio ya Umoja wa Mataifa ilipata fursa ya [...]
01/10/2012 | Jamii: Mahojiano, Malengo ya maendeleo ya milenia | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, ameyataka mataifa manane ambayo bado hayajatia saini mkataba dhidi ya silaha za kemikali yajiunge kwenya mkataba huo haraka iwezekanavyo, kwani silaha hizo hazina nafasi katika karne ya 21. Bwana Ban amesema hayo kwenye mkutano wa ngazi ya juu kuhusu kupinga silaha za kemikali katika makao makuu ya [...]
01/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, leo amefanya mazungumzo na waziri wa mambo ya nje wa taifa la Syria, Bwana Walid Al-Moualem, wakati wa mkutano wa 67 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa. Bwana Ban amezungumzia kuhusu mauaji yanayoendelea, uharibifu kwa kiwango kikubwa, ukiukaji wa haki za binadam, mashambulizi ya angani na [...]
01/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchi zinazoendelea bado zina changamoto kubwa katika kutokomeza umaskini na kuwa na maendeleo endelevu. Kauli hiyo imo kwenye hotuba ya Waziri wa Mambo ya Nje wa India, S. M Krishna aliyoisoma Jumatatu kwenye mkutano wa 67 wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa mjini New York, Marekani. Ametolea mfano nchi za Afrika Kaskazini na Magharibi [...]
01/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kazakhstan iko hatarini kupoteza mafanikio yake iliyopata ya kudhibiti utumwa nchini humo iwapo sheria na mbinu mpya zinazotungwa kudhibiti vitendo hivyo hazitashirikisha sekta zote zinazoguswa na vitendo hivyo kama vile serikali, mashirika yasiyo ya kiserikali, ya kimataifa na sekta binafsi. Mtaalamu wa umoja wa Mataifa kuhusu utumwa wa nyakati za sasa Gulnara Shahinian ametoa tahadhari [...]
01/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la Umoja wa Mataifa la kusaidia wakimbizi wa kipalestina, UNRWA limerejelea kauli yake ya kuitaka Syria kuweka ulinzi wa kutosha kwa wakimbizi wa kipalestina pamoja na raia wengine dhidi ya mapigano yanayoendelea nchini humo. Wito huo unafuatia shambulio la Ijumaa asubuhi kwenye kambi ya wakimbizi ya Neirab Kaskazini mwa Syria lililosababisha vifo vya wapalestina [...]
01/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Guatemala, nchi ya Amerika ya Kati kwa mara ya kwanza imechukua uenyekiti wa Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa mwezi huu wa Oktoba ambapo imeeleza bayana kuwa masuala ya amani na haki yatakuwa ajenda ya juu wakati wa kipindi hicho. Balozi wa Guatemala katika Umoja wa Mataifa Gert Rosenthal amesema suala muhimu ni [...]
01/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Licha ya udogo wao, mataifa madogo yanaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa amani na usalama duniani, amesema Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon. Bwana Ban amesema hayo kwenye kongamano kuhusu mataifa madogo, ambalo limeandaliwa na Jumuiya ya Mataifa Madogo kwenye makao makuu ya Umoja wa Mataifa mjini New York. Bwana Ban amesema, kwa [...]
01/10/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika wakati hali ikizidi kuchacha nchini Syria kwa mamia ya watu kuendelea kupoteza maisha wengine wakilazimika kuimbilia uhamishoni, hiyo ni alama inayoonyesha umuhimu wa kuwepo kwa mageuzi ndani ya Umoja wa Mataifa ili chombo hicho kiwe na uwezo wa kudhibiti hali yoyote korofi kutojitokeza. Hayo ni kwa mujibu wa wanadiplomasia wa Ulaya ambao wamekimbia kikao [...]
01/10/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nusu ya idadi ya watu kote duniani wanakaa mijini, na kadri idadi hii inavyoendelea kuongezeka, ndivyo juhudi zaidi zinafaa kufanywa ili kupunguza umaskini mijini na kuweka maendeleo endelevu. Huo ndio ujumbe wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon kwenye siku ya makazi ya mijini duniani, ambayo huadhimishwa kila Jumatatu ya kwanza ya mwezi [...]
01/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Leo ni siku ya kimataifa ya watu wazee ambapo shirika la afya duniani WHO limekaribisha mji wa Kolkata nchini India kuwa mmoja wa wanachama wake wa mtandao wa miji yenye mazingira bora kwa umri na kwa jamii. Kolkata ndio mji wa kwanza eneo la kusini na mashariki mwa Asia kuwa mwanachama wa WHO, miji mingine [...]
01/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Zaidi ya wakimbizi 700,000 wameikimbia Syria, Sudan , Mali na Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo tangu mwanzo wa mwaka huu kwa mujibu wa shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR. UNHCR inasema kuwa kuchipuka kwa mizozo mipya na kutotatuliwa kwa ile zamani kumesababisha kuongezeka kwa wakimbizi katika historia yake siku za hivi karubuni. [...]
01/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mradi mkubwa wa kimataifa wenye lengo la kuongeza uelewa zaidi wa nafasi ya mazao ya bahari katika kukabiliana na uhaba wa chakula kwa mamilioni ya wakazi maskini kwenye nchi za Afrika, Asia na Amerika ya Kusini umeanzishwa na Umoja wa Ulaya na utadumu kwa miaka mitatu chini ya usimamizi wa shirika la chakula duniani, FAO. [...]
01/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Kazi duniani, ILO Guy Ryder amesema viwango vya ajira vya kimataifa vinapaswa kuzingatiwa na kuendelezwa iwapo mataifa yanataka kujikwamua kiuchumi na kuondokana na ukosefu wa ajira wakati huu ambapo shirika hilo linakadiria kuwepo kwa zaidi ya vijana Milioni 75 duniani wasio na ajira. Ryder ambaye amechukua wadhifa huo kutoka kwa [...]
01/10/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wataalam watatu wa Umoja wa Mataifa wameelezea kushangazwa kwao na mauaji ya mwanasheria wa kutetea haki za binadamu Antonio Trejo Cabrera katika taifa la Honduras, na kukitaja kama kitendo kisichokubalika kamwe, huku kukiwepo hofu kubwa kuhusu usalama wa wanaharakati wa haki za binadamu nchini humo, hususani wale wanaoshughulikia masuala ya mizozo ya ardhi kwa njia [...]
01/10/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »