UNHCR yaitaka Bangladesh kuondoa marufuku kwa mashirika yasiyokuwa ya serikali

Kusikiliza /

wakimbizi wa Myanmar

Shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR linatoa wito kwa serikali ya Bangladesh kuhakikisha kuwa misaada kutoka kwa mashirika yasiyokuwa ya seriali imeendea kutolewa kwa watu ambao hawajasajiliwa kutoka jimbo la Rakhine nchini Myanmar. Juma lililopita mashirika yasiyokuwa ya serikali yakiwemo la Medecins Sans Frontières, Action Contre La Faim and Muslim Aid UK yaliamrishwa na serikali ya Bangladesh kusitisha shughuli zao kwenye kambi ambazo hazijasajiliwa kusini mashariki mwa nchi. UNHCR inasema kuwa ikiwa agizo hilo litatekelezwa litakuwa lenye athari kubwa kwa karibu watu 40,000 ambao hawajasajiliwa walioikimbia Myanmar miaka ya hivi karibuni. Adrian Edwards ni msemaji wa UNHCR

(SAUTI YA ADRIAN EDWARDS)

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031