UM wakatibisha Muafaka wa pande tatu nchini Sudan

Kusikiliza /

 

Mark Cutts

Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Mark Cutts amekaribisha utiaji saini wa maelewano baina ya serikali ya Sudan, kundi la SPLM-North pamoja na Muungano wa Afrika, Jumuiya ya nchi za Kiarabu na Umoja wa Mataifa kuhusu msaada wa kibinadamu katika majimbo yaliyoathirika na vita ya Kordofan Kusini na Blue Nile.

Bwana Cutts amesema haya ni maendeleo muhimu sana ambayo ni lazima yatoe fursa ya kuokoa maisha ya watu kwa kuruhusu misaada kupelekwa kwa raia walioathirika na vita ambao wengi wao wamekwa hawafikiwi kwa zaidi ya mwaka sasa.

Mratibu huyo ameongeza kwamba kipaumbele hivi sasa ni kuhakikisha ugawaji wa haraka wa misaada ya kibinadamu kama inavyohitajika kwa kuzingatia muafaka walioelewana.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031