Ukiukaji mbaya wa haki za binadamu waripotiwa kuendelea nchini DRC

Kusikiliza /

ukiukaji wa haki za binadamu, DRC

Shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa UNICEF linasema kuwa ukiukaji mbaya wa haki za binadamu umeripotiwa kwenye Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo ukiwemo mauaji ya kijiji kizima na makundi yaliyojihami, ubakaji, utekaji nyara na kuwaingiza watoto kwenye jeshi.

Kote nchini DRC karibu watoto milioni moja wameathiriwa na hali mbaya ya utapiamlo huku taiafa hilo pia likikikabiliwa na ugonjwa wa kipindupindu. Hadi tarehe 23 mwezi Julai Mwaka huu visa 20,007 na vifo 481 vimeripotiwa kutokana na ugonjwa wa kipindupindu. Takriban watu milioni 2.2 kwa sasa ni wakimbizi wa ndani mashariki mwa DRC. UNICEF kwa sasa inahitaji zaidi ya dola milioni 133 kushughulikia watoto na wanawake walioathiriwa mwaka huu huku milioni 35.2 zikihitajika kwa dharura. Patrick McCormick ni msemaji wa UNICEF

(SAUTI YA PATRICK MCCORMICK)

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031