Nyumbani » 14/08/2012
Entries posted on “Agosti 14th, 2012”
Kusikiliza /

Kamati ya kimataifa inayohusika na kuondoa au kupinga matumizi na silaha za nyuklia, imejadili aina mpya za silaha za maangamizi ya halaiki pamoja na mifumo mipya ya silaha kama hizo, zikiwemo silaha za miyale ya Uranium. Kamati hiyo pia inajadili mpango wa kina kuhusu uondoaji wa silaha kama hizo, na uazi kuhusu mataifa kujihami kwa [...]
14/08/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Ujumbe wa Umoja wa Mataifa uliokuwa London kwenye michuano ya Olimpiki umesifu mafanikio makubwa yaliyopatikana kwenye michezo ya mwaka huu hatua ambayo wameeleza kuwa inafungua njia ya kupatikana mafanikio zaidi kwenye maeneo yanayohusu ustawi wa kijamii ikiwemo ujenzi wa amani na kupunguza matabaka ya kijinsia. Katika taarifa yake kwa vyombo vya habari, ujumbe huo umewapongeza [...]
14/08/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wakfu wa Khalifa Bin Zayed Al Nahyan ukishirikiana na Shirika la Umoja wa Mataifa linalohusika na wakipimbizi wa Kipalestina UNRWA umefaulu kuanzisha mpango unaoitwa " walishe wafungao" kwa ajili ya kuwakirimu wananchi wa Ukingo wa Gaza walioko kwenye kipindi cha mwezi wa Ramadhani. Chini ya mpango huo kiasi cha watu zaidi 28,000 wanatazamia kufaidika wakipatia [...]
14/08/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Huku watu zaidi wakiendelea kuikimbia Syria kila siku shirika la kuhudumia wakimbizi la Umoja wa Mataifa UNHCR linafanya jitihada za kuwaaandiskisha wakimbizi kutoka nchi hiyo. Uandikishaji wa wakimbizi ni muhimu kwa sababu unaawasaidia wakimbizi kupata huduma muhimu. Kituo kipya kwa sasa kimefunguliwa kaskazini mwa Lebabon kitakachosaidia kuwaandikisha karibu watu 700 kwa siku . Kwa sasa [...]
14/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM kwa ushirikiano na shirika la kuhudumia watoto la Umoja wa Mataifa wamewasaidia waathiriwa wawili wa usafirishaji haramu wa watu kutoka Kenya kurejea makwao kutoka Sudan kusini. Inaripotiwa kuwa waathiriwa hao ambao ni vijana walitolewa kwenye jamii moja kijijini kwa kazi za nyumbani lakini baadala yake walilazimishwa na kuingizwa kwenye [...]
14/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, ameelezea wasiwasi wake kuhusu hali ya chelewa chelewa inayozingira kuundwa kwa bunge jipya nchini Somalia, pamoja na matukio ya vitisho na ghasia ya hivi karibuni. Kwa mujibu wa taarifa yake, Bwana Ban amesema matukio hayo na ghasia havitakiwi kuruhusiwa kuendelea au kuhatarisha kukamilishwa kwa kipindi cha mpito [...]
14/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mratibu Mkuu wa Misaada ya Kibinadamu katika Umoja wa Mataifa, Bi Valerie Amos, amewasili nchini Syria kwenye ziara ya siku tatu, ili kukagua hali ilivyo na jinsi ya kuwasaidia watu walioathiriwa na machafuko. Mjini Damascus, Bi Amos amepanga kufanya mazungumzo na maafisa wa serikali na wadau katika utoaji wa huduma za kibinadamu, pamoja na familia [...]
14/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kampeni ya kimataifa lenye lengo la kuweka historia ya mitandao ya kijamii kwa kujaribu kuwafikia watu bilioni moja hapo Agosti 19 katika kusherehekea siku ya kimataifa ya masuala ya kibinadamu, imepita lengo lake la kwanza la kufikia watu milioni 100. Kampeni hiyo imepata msukumo mkubwa kufuatia tamasha la muziki lililofanyika Ijumaa kwenye baraza Kuu la [...]
14/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kimataifa la uhamiaji IOM linaomba msaada wa fedha ili kukabiliana na mahitaji ya haraka ya kibinadamu kwa watu 8000 wa Kiethiopia waliotawanywa na machafuko na jamii zinazowahifadhi kwenye maeneo ya Somare, wilaya ya Moyale upande wa Kenya kwenye mpaka na Ethiopia. Tathimini ya pamoja iliyoongozwa na IOM, shirika la wakimbizi UNHCR na shirika [...]
14/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »