Nyumbani » 09/08/2012
Entries posted on “Agosti 9th, 2012”
Kusikiliza /

Akikamilisha ziara yake ya siku nne Myanmar, Mkurugenzi wa shughuli za Ofisi ya Kuratibu Misaada ya Kibinadam, John Ging ameelezea hofu yake kuhusu hatma ya zaidi ya nusu milioni ya wakimbizi wa ndani, na kutoa wito ziheshimiwe kanuni na sheria za kimataifa za kibinadamu ili kuyawezesha mashirika ya kutoa misaada kuyafikia maeneo yaloathiriwa na mzozo [...]
09/08/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkuu wa maswala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa, Valerie Amos, ametenga dola milioni 55 kutoka kwenye mfuko wa Mfuko wa Ufadhili wa Maswala ya Dharura (CERF), ili kuimarisha operesheni za kibinadamu katika nchi nane zenye mahitaji ya kibinadam yaliyopuuzwa. Fedha zilizotengewa mataifa ya Afghanistan, Cameroon, Colombia, Jamhuri ya Demokrasi ya Congo (DRC), Ethiopia, Madagascar, [...]
09/08/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »

Jamii za kiasili kwenye milima ya kusini mwa Andean nchini Peru wanaripotiwa kuathiriwa pakubwa na mabadiliko ya hali ya hewa. Jamii hizi zinakabiliwa na hali mbaya ya umaskini suala linalochangiwa na mavuno duni. Jamii hizi zinazoishi mbali milimani hazina uwezo wa kupata hamasisho kutoka mijini kuhusu njia za kukabiliana na athari za mabadiliko ya hali [...]
09/08/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mratibu wa masuala ya kibinadamu wa Umoja wa Mataifa nchini Sudan Mark Cutts amekaribisha utiaji saini wa maelewano baina ya serikali ya Sudan, kundi la SPLM-North pamoja na Muungano wa Afrika, Jumuiya ya nchi za Kiarabu na Umoja wa Mataifa kuhusu msaada wa kibinadamu katika majimbo yaliyoathirika na vita ya Kordofan Kusini na Blue [...]
09/08/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kupuuza haki za binadamu za kimataifa na sheria za kimataifa kumechangia kuwepo kiasi kikubwa sana cha wakimbizi wa ndani nchini Syria, wakati mgogoro unapozidi kutokota, amesema mtaalam wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za watu wakimbizi wa ndani, Chaloka Beyani. Bwana Beyani ameelezea kusikitishwa kwake na hali ya takriban watu milioni 1.5, ambao wamelazimika kuhama [...]
09/08/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Msemaji wa mpango wa Umoja wa mataifa nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo MONUSCO Manodj Monoubay ametoa tangazo la kuwatahadharisha waasi wa M23 pamoja na makundi mengine yenye silaha yanayotishia salama Mashariki mwa nchi hiyo kusitisha mara moja zoezi la kuwaingiza watoto jeshini. Akizungumza na waandishi wa habari mjini Kishasa Jumatano Monoubary amesema ikiwa waasi [...]
09/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea umuhimu wa diplomasia ya kutambua mapema na kusuluhisha mizozo kwa njia ya amani kama njia ya kuzuia migogoro zaidi. Wanachama wa Baraza hilo wameelezea umuhimu wa kisiasa, kibinadamu na kimaadili, pamoja na faida za kiuchumi za kuzuia kutokea, kuongezeka au kurejelea migogoro. Katika taarifa ilotolewa kwa waandishi [...]
09/08/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Bei ya bidhaa za chakula ilipanda kwa kiasi cha asilimia 6 mwezi Julai, baada ya miezi mitatu ya kushuka bei hiyo, limesema Shirika la Kilimo na Chakula Duniani, FAO. Kipimo wastani cha viwango vya bei za bidhaa za chakula cha FAO, hupima mabadiliko ya kila mwezi katika bei za kapu la bidhaa za chakula. Kwa [...]
09/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mratibu wa Umoja wa Mataifa wa misaada ya dharura na misaada ya kibinadamu Valarie Amos amehitimisha ziara yake nchini Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Congo siku ya Alhamisi baada ya kuzuru eneo la Kanyaruchinya nje kidogo ya mji wa Goma siku ya Jumatano. Katika eneo hilo watu 30,000 wamepatiwa makao na amesema inasikitisha kuona watu hususani [...]
09/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katika muktadha huo wa kuadhimisha siku ya kimataifa ya watu wa kiasili leo, Shirika la Kimataifa la kazi duniani, ILO, limesema vyombo vya habari vya kijamii vinachangia kwa kiasi kikubwa kuendeleza haki za watu wa kiasili. Shirika la ILO limesema hili linatokana na kwamba, takriban nusu ya idadi ya watu wa kiasili kote ulimwenguni wanaishi [...]
09/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Imeelezwa kwamba huu ni wakati pekee ambao watu wa kiasili hupewa kipaumbele kwenye vyombo vya habari, ni pale wanapouawa. Hii ni dhana ya kusikitisha na ni mojawepo tu ya mifano ya malalamishi yaliyofikishwa kwa Mkuu wa Sekritariati ya Kamati ya Kudumu ya Umoja wa Mataifa kuhusu watu wa kiasili, Chandra Roy-Henriksen. Siku ya kimataifa ya [...]
09/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amewapongeza watu wa asili kwa kujitokeza kutumia vyombo vya habari vya asili na vya kisasa katika kuchagiza masuala mbalimbali yanayowahusu. Katika ujumbe wake maalum wa siku ya kimataifa ya watu wa asili Alhamisi Ban amesema kuanzia magazeti, tovuti hadi mitandao ya kijamii watu wa asili wanatoa changamoto [...]
09/08/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »