Watoto Wenye Ulemavu Wako kwenye Hatari ya Kudhulumiwa

Kusikiliza /

mtoto mlemavu

Watoto walio na ulemavu wako kwenye hatari ya kudhulumiwa mara nne zaidi kuliko wale wasio na ulemavu. Hii ni kwa mujibu wa utafiti kutoka kwa shirika la afya duniani WHO. Ripoti hiyo inasema kuwa watoto walio na ulemavu unaohusu matatizo ya kiakili na ulemavu wa viungo vya mwili wako kwenye hatari ya kudhulumiwa kimapenzi ikilinganishwa na wasio na ulemavu.

Utafiti huo uliendeshwa miongoni mwa watoto 18,374 walio na ulemavu kwenye mataifa yenye kipato cha juu yakiwemo Finland, Ufaransa , Israel, Uhispania , Sweden, Uingereza na Marekani. Dr Tom Shakespeare kutoka WHO anasema kuwa takwimu kutoka nchi zenye kipato cha wastani na cha chini hazikujumuishwa hata kama ishara ni kwamba dhuluma kwa watoto walio na ulemavu kwenye nchi hizi ni za viwango vya juu.

(SAUTI YA DR. TOM SHAKESPEARE)

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031