UNECE Inasaidia Udhibiti wa Taarifa kuhusu Maji ya Asia ya Kati

Kusikiliza /

kongamano la UNECE

Washiriki katika warsha ya udhibiti wa masuala ya maji iliyofanyika mapema mwezi huu mjini Almaty wamepitisha sheria na muongozo wa miaka mitatu hadi mitano za kuanzisha takwimu za udhibiti wa maji katika eneo la Aral Sea Basin huko Asia ya Kati.

Tume ya Umoja wa Mataifa kwa ajili ya maendeleo ya Ulaya UNECE imesema inasaidia katika mikataba ya masuala mbalimbali ya maji kwenye eneo hilo ikiwepo ushiriki wa jamii na fursa za kupata taarifa, ajali za viwandani na athari za mazingira.

Warsha hiyo iliyoandaliwa na Bank ya dunia, ushirikiano wa maendeleo wa Uswis na UNECE iliwaleta pamoja washiriki ktoka mataifa 50 na wataalamu kutoka Afghanistan, Kazakhstan, Kyrgystan, Tajikistan, Turkmenistan , Uzbekistan, mashirika mbalimbali ya kikanda na wahisani.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031