Nyumbani » 16/07/2012
Entries posted on “Julai 16th, 2012”
Kusikiliza /

Wakati mzozo wa Syria unazidi kutokota, watu wa Syria wanaendelea kuteseka hata zaidi. Raia ambao tayari wamebaniwa katika mviringo wa ghasia, sasa pia wanalengwa na dhuluma za ngono, amesema kaimu mwakilishi maalum wa Umoja wa Mataifa kuhusu dhuluma za ngono katika maeneo ya vita, Vijay Nambiar. Amesema serikali zote zina jukumu la kuwalinda raia kutokana [...]
16/07/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Waangalizi wa Umoja wa Mataifa ambao wamefanya ukaguzi katika kijiji cha Tremseh nchini Syria siku ya jumapili, wamesema kulingana na kile walichokiona na ushahidi uliopo, mashambulizi ya Julai 12 yalilenga waasi wa kijeshi na wanaharakati. Wafanyakazi kutoka mpango wa Umoja wa Mataifa, UNSMIS, walishuhudia zaidi ya nyumba 50 kuchomwa au kuharibiwa na wamebaini kuwa damu [...]
16/07/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Nchi zilizokusini mwa jangwa la sahara ni lazime zihakikiwe kuwepo kwa ajira za kisasa na huduma za kijamii ikiwa zingetaka kuafikia maendeleo . Hii ni kulingana na ripoti mpya kuhusu hatua zilizopigwa za kupunguza umaskini duniani. Ripoti hiyo inachapishwa kila mwaka na tume muungano wa Afrika, benki ya maendeleo barani Afrika , shirika la maendeleo [...]
16/07/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi mkuu wa shirika la kupambana na ugonjwa wa ukimwi la Umoja wa Mataifa UNAIDS Michel Sidibe amelipongeza shirika la kupambana ugonjwa wa ukimwi barani Afrika la AIDS Watch Afrika (AWA) na kulitaja kuwa kiongozi katika vita dhidi ya ukimwi barani Afrika. Akihutubia zaidi ya maafisa 20 wa ngazi za juu mjini Addis Ababa nchini [...]
16/07/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi wa kitengo cha kutoa huduma kwenye shirika la kuratiibu masuala ya kibinadamu la Umoja wa Mataifa OCHA, John Ging anasema kuwa huduma nchini Syria zinakabiliwa na changamoto za ukosefu wa fedha huku kukiwa na hofu ya kukwama kwa jitihada za kuwasaidia wakimbizi nchini Syria na waliovuka na kuingia nchi jirani. Ging anasema kuwa ukosefu [...]
16/07/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Jan Eliasson, leo amesisitizia umuhimu wa ushirikiano wa karibu kati ya Umoja wa Mataia na Muungano wa Afrika katika kukabiliana na masuala kadha wa kadha muhimu, yakiwemo mzozo nchini Mali na tatizo la usalama wa chakula katika eneo la Sahel. Akiuhutubia mkutano wa 19 wa Muungano wa Afrika [...]
16/07/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Elimu, Sayansi na Utamaduni la Umoja wa Mataifa, Irina Bukova, ameelezea kusikitishwa kwake na mauaji ya raia 7 waliojitolea kuandika habari kuhusu mzozo wa Syria kati ya tarehe 10 Juni na tarehe 4 Julai. Waandishi hao ni Suhaib Dib, Mohamed Hamdo Hallaq, Samer Khalil Al-Sataleh, Ghias Khaled Al-Hmouria, Omar Al-Ghantawi, [...]
16/07/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Afisi ya Umoja wa Mataifa kuhusu madawa na uhalifu, imezindua leo kampeni ya kimataifa ya kuwahamasisha watu, ambayo inaangazia hasa zaidi kiwango na gharama ya uhalifu wa kimataifa wa kupangwa. Kampeni hiyo ambayo inatoa maelezo zaidi kuhusu uhalifu wa kimataifa, ambao unatajwa kama tishio kwa amani, usalama wa kibinadamu na maendeleo, na ambao umefanywa kuwa [...]
16/07/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Waziri wa mambo ya ndani wa Afrika Kusini, Nkosazana Dlamini-Zuma, amechaguliwa kama rais mpya wa Tume ya Muungano wa Afrika. Bi Dlamini-Zuma alimshinda mpinzani wake Jean Ping wa Gabon, ambaye amekuwa rais wa tume hiyo kwa kunyakua kura 37, huku Bwana Ping akipata kura 14 pekee. Uteuzi wa Bi Dlamini-Zuma umefuatiwa na shangwe na vigelegele [...]
16/07/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Waangalizi wa Umoja wa Mataifa nchini Syria wamesema kuwa mashambulizi yaliyofanywa kwa siku tatu mfulizo na vikosi vya serikali yalilenga kuviandama vikosi vya waasi vilivyopo katika kijiji cha Tremseh. Waangalizi hao ambao wamerejea kutoka kijiji hicho wamesema mashambulizi hayo yameacha uharibifu mkubwa ikiwemo nyumba kuchomwa moto, na idadi kubwa ya watu wamepoteza maisha. Ripoti iliyotolewa [...]
16/07/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »