Rais wa Baraza Kuu ataka nchi maskini zisaidiwe kufikia shabaha ya maendeleo endelevu

Kusikiliza /

 

Rais wa GA

Mashirikiano ya kimaendeleo lazima yaweka kipaumbele kuzisaidia nchi maskini kutekeleza sera zinazoangazia maendeleo endelevu.

Huo ndiyo ujumbe mahususi uliotolewa na rais wa baraza kuu la Umoja wa Mataifa Bwana Nasir Abdulaziz Al-Nasser wakati akifungua mkutano wa kimataifa wa Rio + 20, unaofanyika huko Brazil.

Amesema kuwa bado nchi masikini zinapaswa kuungwa mkono kwa kupatiwa misaada zaidi kwani bila kufanya hivyo kunaweza kukabiliwa na hali ya mkwamo kwenye ufikiaji wa dhana ya maendeleo endelevu. Amesisitiza kuwa kuna haja ya kuwa na dhamira ya dhati ili kutekeleza kwa vitendo malengo yote yaliyoanishwa na mkutano wa Rio + 20.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031