Mwakilishi wa UM akaribisha maafikiano kuhusu katiba Somalia

Kusikiliza /

 

Mwakilishi Mkuu wa Umoja wa Makataifa kuhusu masuala ya Kisiasa nchini Somalia, ameukaribisha muafaka uliosainiwa na viongozi wa Somalia kama hatua muhimu katika kulitayarisha taifa hilo kwa ajili ya kumalizika mfumo uliopo sasa wa serikali ya mpito. Katika mkutano uliofanyika mjini Nairobi, Kenya, viongozi wa Kisomali wameafikia mswada rasmi wa katiba , ambao sasa utachapishwa.

Katika taarifa yake, Mwakilishi huyo maalum, Augustine Mahiga ameelezea kufurahishwa kwake na wahusika kuja pamoja kwa moyo wa ushirikiano na maridhiano, na kukubali kwa kauli moja kuendeleza harakati hizi za kisiasa. Amesema na hakuna muda wa kupoteza.

Baada ya miongo ya vita, nchi ya Somalia imekuwa kwenye harakati za amani na maridhiano, huku taasisi zake za mpito zikitekeleza mpango wa kuhitimisha kipindi cha mpito, ambao ulikubaliwa mwezi Septemba mwaka uliopita, na ambao unaweka masuala muhimu yanayotakiwa kupewa kipaumbele kabla ya kumalizika kwa mfumo wa serikali ya mpito Agosti 20.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031