Mkutano wa RIO+20 ni muhimu kwa siku za usoni: BAN
Kusikiliza /Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki moon amesema mkutano wa Rio+20 utataoa fursa kwa siku nzuri za baadaye kwa wote kote duniani.
Akihutubia mkutano wa baraza kuu la kundi la mataifa yaliyostawi na yanayoinukia kiuchumu la G20 mjini Los Cabos nchini Mexico Ban amesema kuwa bado uchumi wa dunia hautabiriki.
Amesema kuwa sarafu ya Euro huenda ikaathiri uchumi na maisha ya watu wengi kote duniani. Ban ameongeza kuwa uchumi kwenye baadhi ya nchi zilizostawi umeshuka huku wa nchi zingine ukiwa tayari umekwama.
