Hakuna Taifa pekee linaloweza kuushinda Ugaidi:Nassir

Kusikiliza /

Rais wa baraza kuu Nassir Abdulaziz Al-Nasser

 

Rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Abdulaziz Al-Nasser amesema hakuna taifa hata moja hata liwe na nguvu kiasi gani linaloweza kupambana na ugaidi peke yake. 

Akizungumza katika siku ya pili ya kongamano la kupambana na ugaidi kwenye Baraza Kuu Bwana Al-Nasser amesema jumuiya ya kimataifa imepiga hatua kubwa na kupata mafanikio katika vita dhidi ya ugaidi hali inayodhihirisha kwamba dunia ina ari na moyo wa kushirikiana hata wakati ambao inakabiliwa na changamoto kubwa. 

Ameongeza kuwa nguzo nne muhimu zinashughulikia masuala muhimu ya kupambana na ugaidi kimataifa. Ameongeza kuwa wakati umewadia wa kuwa na utekelezaji madhubuti wa miakakati iliyoweka ya vita dhidi ya ugaidi. 

(SAUTI YA AL-NASSER)

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031