Bei ya chakula imeshuka kote duniani:FAO
Kusikiliza /Bei ya chankula kote duniani imeshuka ghafla mwezi Mei kwa sababu ya kuongezeka uzalishaji, uchumi kuendelea kuyumbayumba na kupanda kwa dhamana ya dola ya Kimarekani, limesema leo shirika la Mazao na Chakula, FAO.
Kipimo cha bei ya chakula cha FAO, kinachotizama mabadiliko katika bei ya kapu la bidhaa za chakula ulimwenguni, kilishuka kwa asilimia nne mwezi Mei. Kipimo hicho kwa wastani kilifikia pointi 204, na hivyo kushuka kwa pointi 9 tokea mwezi Aprili. George Njogopa anaripoti
(RIPOTI YA GEORGE NJOGOPA)
