Ban akaribisha kuanza kwa mazungumzo ya kitaifa nchini Lebanon

Kusikiliza /

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amekaribisha kuanza kwa mazungumzo ya kitaifa kati ya viongozi wa kisiasa nchini Lebanon. Kupitia kwa msemaji wake Ban amewashauri viongozi wa kisiasa nchini Lebanon kuendelea na kazi yao kwenye mpango huu muhimu wanapojiandaa kwa mkutano unaopangwa kufanyika tarehe 25 mwezi huu.

Kulingana na vyombo vya habari mkutano ulioandaliwa chini ya uenyekiti wa rais wa Lebanon Michel Sleiman mnamo Juni 11 kati ya viongozi wa kundi la Hizbollah ni wa kwanza wa kitaifa kundaliwa kwa muda wa miezi 18 iliyopita ambapo viongozi walikubaliana kujitolea na kujizuia na hotuba ambazo zinaweza kuleta chuki.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031