Nyumbani » 25/06/2012
Entries posted on “Juni 25th, 2012”
Kusikiliza /

Mahakama ya kimataifa kuhusu mauaji Rwanda, (ICTR), imeihamishia kesi dhidi ya mshukiwa Aloys Ndimbati nchini Rwanda ili isikilizwe huko. Aloys Ndimbati alikuwa mkuu wa jimbo la Gisovu tokea mwaka 1990 hadi mwishoni mwa Julai 1994 yalipomalizika mauaji ya kimbari. Ndibati, ambaye bado yupo mafichoni, ameshtakiwa kwa mauaji ya kimbari, kusaidia kutekeleza mauaji hayo, kuchochea mauaji [...]
25/06/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Takwimu mpya zilizotolewa na tume ya kimataifa kuhusu biashara katika viumbe waliomo kwenye hatari ya kutokomezwa, CITES, na Idara ya Mazingira ya Afrika Kusini, inaonyesha kwamba idadi ya vifaru wanawindwa imekithiri na kufikia kiwango kipya. Idadi ya vifaru weusi mwituni inakadiriwa kuwa 5, 000 na ile ya vifaru weupe kukadiriwa kuwa 20, 000. Vifaru wa [...]
25/06/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Visa vya ubakaji na dhuluma za ngono katika kambi ya wakimbizi ya Kiziba nchini Rwanda vinapungua, lakini athari za kimwili na hisia husalia kuwa kubwa visa hivi vinapotokea. Desturi ya wakimbizi wa Kongo kwenye kambi hiyo kuvinyamazia visa hivi kila vinapotokea, inafanya mambo kuwa mabaya zaidi, kwani huendeleza kutowachukulia hatua za kisheria wale wanaovitenda, na [...]
25/06/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kikao chja 36 cha kamati ya kimataifa ya urithi wa dunia kimeanza huku shirika la Umoja wa Mataifa la elimu , sayansi na utamaduni UNESCO likiadhimisha mwaka wa 40 tangu kupitishwa mkatana wa urithi wa dunia. Kikao hicho cha kamati kimeanza Jumapili St Petersburg kukiwa na changamoto nyingi zinazokabili uhifadhi wa urithi wa dunia huku [...]
25/06/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Kuanzishwa kwa kituo maalumu kwa ajili ya kutoa mafunzo yahusuyo maendeleo endelevu ni alamu ya pekee itayokumbusha dunia juu ya mkutano wa mazingira wa Umoja wa Mataifa wa Rio +20. Kwa mujibu wa shirika la maendeleo la Umoja wa Mataifa UNDP, mapendekezo yaliyofikiwa juu ya uanzishwaji wa kituo hicho yanatoa alaamu muhimu juu ya hatua [...]
25/06/2012 | Jamii: Rio+20, Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Shirika la kimataifa la masuala ya ubaharia (IMO) limetoa wito kwa watu kote ulimwenguni kutumia njia zote za mawasiliano kuangazia umuhimu wa mabaharia katika maisha ya kila mtu, wanapochukua bidhaa muhimu ambazo zinategemewa na wote katika maisha yao ya kila siku. Katika ujumbe wake kwenye siku hii, katibu mkuu wa IMO, Koji Sekimizu amesema, inafaa [...]
25/06/2012 | Jamii: Taarifa maalumu | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Ban Ki-Moon, amelitaka Baraza la Usalama na mataifa wanachama kutafuta njia mpya za kuwalinda raia na kuhakikisha ukiukaji wa sheria za kimataifa na haki za binadamu unakabiliwa ipasavyo. Bwana Ban amesema haya katika ripoti yake ya tisa, wakati wa mjadala wa Baraza la Usalama kuhusu kuwalinda raia katika maeneo [...]
25/06/2012 | Jamii: | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amemteua Zainab Hawa Bangura ambaye kwa sasa ni waziri wa afya nchini Sierra Leone na mjumbe wake mpya kwenye masuala ya dhulama na kimapenzi kwenye mizozo. Bangura tachuka mahala pa Margot Wallstrom mwanasiasa kutoka Sweden aliye na historia ya kutetea haki za wanawake. Kupitia kwa msemaji wake [...]
25/06/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameelezea wasi wasi uliopo kufuatia kudunguliwa kwa ndege ya kijeshi ya Uturuki nchini Syria. Akizungumza kwa njia ya simu na waziri wa mambo ya kigeni nchini Uturuki Ahmet Davutoglu Ban aliipongeza Uturuki kwa moyo wa uvumilivu ambao imeonyesha na pia kuyashukuru mataifa hayo mawili kwa oparesheni ya [...]
25/06/2012 | Jamii: Hapa na pale | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Wawakilishi wa Umoja wa Mataifa Sudan Kusini, UNMISS, wametoa ripoti mpya leo ya uchunguzi wa kina uliofanywa kuhusu ghasia za kikabila kwenye jimbo la Jonglei, ambazo zilisababisha vifo vya mamia ya watu mwaka jana na mapema mwaka huu. Ripoti hiyo, yenye kichwa: Visa vya ghasia za kikabila katika jimbo la Jonglei, ripoti hiyo ya kurasa [...]
25/06/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon amekaribisha hatua ya kukamilika kwa mchakato wa uchaguzi wa Rais nchini Misri kufuatiwa kutangazwa kwa matokeo rasmi ya uchaguzi wa duru ya pili uliyofanyika Juni 16 na 17 kutolewa na tume ya uchaguzi Jumapili. Ban amewapongeza watu wa Misri kwa kuhakikisha mazingira ya amani na utulivu wakati [...]
25/06/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Dhuluma dhidi ya wanawake zimeongezeka na kufikia viwango vya kutisha, huku wanawake na wasichana wengi zaidi wakiendelea kuuawa nyumbani na wachumba wao au jamaa zao, kwa mujibu wa mtaalam wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki za binadamu, Rashida Manjoo. Mtaalam huyo wa masuala ya dhuluma dhidi ya wanawake, amesema katika mataifa mengi, nymbani ndipo mahali [...]
25/06/2012 | Jamii: Habari za wiki | Kusoma Zaidi »
Kusikiliza /

Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon ameuambia ulimwengu kwamba ingawa kongamano la kimataifa la Rio+20 limemalizika, lakini kazi ya kujenga dunia endelevu ndio kwanza inaanza. Ban amekaribisha malengo zaidi ya 700 yaliyotangazwa kwenye mkutano wa Rio na nchi, makampuni ya biashara, bank za maendeleo, vyuo vikuu na mashirika ya Umoja wa Mataifa miongoni [...]
25/06/2012 | Jamii: Habari za wiki, Rio+20 | Kusoma Zaidi »