Valarie Amos akaribisha kuachiliwa kwa wafanyakazi saba wa misaada Yemen

Kusikiliza /

Valerie Amos

Mkuu wa Umoja wa Mataifa wa kuratibu masuala ya kibinadamu na misaada ya dharura leo ametangaza kwamba wafanyakazi saba wa misaada waliotekwa mapema wiki hii nchini Yemen sasa wote wameachiliwa bila kudhuriwa.

Katika taarifa yake Bi Valarie Amos amesema wafanyakazi hao waliotekwa siku ya Jumanne wiki hii sasa wako mjini Sanaa na wanawasiliana na familia zao. Ameongeza kuwa anaishukuru serikali ya Yemen na wote waliohusika kufanya kazi bila kuchoka kuhakikisha watu hao waachiliwe wakiwa salama.

Amesema kitendo cha kutekwa kwa wafanyakazi hao kinadhihirisha hatari inayowakabili kila siku wafanyakazi wa misaada ambao wanawasaidia watu wanaohitaji msaada kote duniani.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

Kuungana

 

Mei 2012
T N T K J M P
« apr    
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031