UM waunga mkono kampeni ya chanjo nchini Cameroon

Kusikiliza /

chanjo ya Homa ya Manjano

Umoja wa Mataifa umeunga mkono kampeni kubwa ya kutoa chanjo inayoendelea kaskazini mwa Cameroon ambapo kumeripotiwa mkurupuko wa homa ya manjano. Kampeni hiyo iliyoanza mwezi uliopita kwenye wilaya nane inalenga kuwakinga zaidi ya watu milioni 1.2 walio kwenye hatari kubwa ya kuambukizwa ugonjwa huo unaosambazwa na mbu na usio na tiba.

Shirika la afya duniani WHO linasema kuwa chanjo hiyo inalenga maeneo ambayo chanjo haikufanywa mwaka 2009 na ambapo ugonjwa huo haukuripotiwa awali.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

Kuungana

 

Mei 2012
T N T K J M P
« apr    
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031