UM utavuna mengi ukiongeza mashirikiano yake na Umoja wa Ulaya
Kusikiliza /Umoja wa Mataifa umeelezewa umuhimu wa kuwa na mafungamano ya karibu na nchi wanchama wa Umoja wa Ulaya ambazo zinaunda jumuiya ya usalama na mashirikiano katika eneo hilo OSCE, kuwa hatua hiyo itazalisha matunda mema.
Waziri wa mambo ya nchi za Nje wa Ireland ambaye ndiye rais wa chombo hicho cha usalama kwa nchi za ulaya ameliambia baraza la usalama juu ya pande hizo kuwa na mashirikiano yenye mshiko na utengamao.
Eamon Gilmore amesema pande zote mbili zinajongeleana kwa mambo mengi, ambayo kama yatapewa uzito na kutumika ipasavyo yanaweza kufaa kukabili changamoto za kiusalama zinazoikabili dunia kwa sasa.
Jumuiya hiyo inajuka ya nchi wanachama 54 na inachukua jukumu la pekee kuhusiana na masuala ya usalama kwa kanda ya Ulaya.
