Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa kuijadili hali nchini Syria

Kusikiliza /

Baraza Kuu

Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa linatarajiwa kukutana siku ya Jumatatu ili kuijadili hali nchini Syria ambapo idadi ya watu wanaouawa inazidi kuongezeka kufuatia mikakati ya jeshi ya kukabiliana na makundi yanayoipinga serikali.

Mkuu wa haki za binadamu kwenye Umoja wa Mataifa Navi Pillay atalishauri baraza hilo kuhusu hali ilivyo kufuatia ombi kutoka kwa rais wa Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa Nassir Abdulaziz Al-Nasser.

Zaidi ya watu 5000 wameuawa tangu kuanza kwa ghasia zilizoenea kutoka kaskazini mwa Afrika hadi mashariki ya kati ambapo maafisa wa UM wameitaka serikali ya Syria kufanya mazungumzo na makundi ya upinzani.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

Kuungana

 

Mei 2012
T N T K J M P
« apr    
 123456
78910111213
14151617181920
21222324252627
28293031