Ban asikitikia ghasia za kwenye uwanja wa mpira Misri
Kusikiliza /Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moom ameelezea masikitiko yake kufuatia ghasia zilizozuka kwenye uwanja wa mpira na kusabisha watu zaidi ya 70 kupoteza maisha nchini Misri.
Katika tukio hilo lililohusisha timu mbili zenye upinzani wa jadi, watu wengi kadhaa walijeruhiwa wakati mamia wengine wakiwachwa katika hali ya kihoro.
Ghasi hizo zilizoka katika uwanja wa Jiji la Port baina ya mashabiki wa klabu ya al-Masry dhidi ya al-Ahly.
Katika taarifa yake juu ya tukio hilo, Ban amesema kuwa anaamanini mamlaka za Misri zitachukua mkondo sahihi kushughulikia kadhia hiyo.
