ICC yakaribisha hatua ya Grenada kuwa mwanachama mpya wa mahakama hiyo

bendera ya Grenada

Mahakama ya kimataifa ya uhalifu ICC imekaribisha hatua ya Grenada ambayo wiki hii imeridhia mkataba wa Roma unaotambua uwepo wa mahakama hiyo. Ikikaribisha hatua hiyo ICC imefanya tafriji maalumu mjini  Hague kama njia ya kupongeza uamuzi uliochukuliwa na Grenada kuridhia mkataba huo.

Kama ishara ya kukubalika kuwa mwanachama, rais wa mahakama hiyo Jaji Sang-Hyun Song alimkabidhi balozi wa Grenada hati maalumu inayoashiria kuwa mwanachama wa mahakama ya kimataifa. Taifa la Grenada linakuwa taifa la 115 kuridhia kwa mkataba wa Rome ambao unatambua mahakama ya kimataifa.

Kipindi Kamili
Kipindi Kamili
Loading the player ...

 

Mei 2013
T N T K J M P
« apr    
 12345
6789101112
13141516171819
20212223242526
2728293031